Matokeo ya Uchaguzi Kenya 2022: Madai ya kupotosha kuhusu matokeo ya uchaguzi wa urais Kenya

Wakenya wanafuatilia kwa karibu taarifa za kwa matokeo ya uchaguzi
Maelezo ya picha, Wakenya wanafuatilia kwa karibu taarifa za kwa matokeo ya uchaguzi

Huku Wakenya wakisubiri kwa hamu matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumanne, baadhi ya watumiaji wa mtandao wamekuwa wakisambaza madai ya kupotosha kuhusu matokeo na mchakato wa upigaji kura.

Tunaangazia baadhi ya madai ambayo imeshirikishwa sana mitandaoni.

Kura zilizopigwa sio zaidi ya wapiga kura katika ngome ya Odinga

Screenshot of election results posted by Dennis Itumbi

Mwanablogu anayemuunga mkono Naibu wa Rais William Ruto alichapisha fomu ya matokeo kwenye Twitter inayoonyesha idadi ya wapiga kura katika kituo cha kupigia kura katika ngome ya mpinzani wake mkuu Raila Odinga ya Kisumu magharibi mwa Kenya ilikuwa 107.7%.

"Wapiga kura waliojiandikisha katika Soko la Kondele 1 wameonyeshwa kama 362 na waliopiga kura ni 390," aliandika kwenye ujumbe wa Twitter.

https://twitter.com/OleItumbi/status/1557080010753773568

Kusoma data kwenye fomu kunatoa hisia kwamba watu wengi zaidi ya waliojiandikisha kupiga kura walipiga kura zao.

Hata hivyo, ukiangalia takwimu rasmi za wapiga kura waliojiandikisha kwenye tovuti ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka inaonyesha idadi halisi ya wapiga kura katika kituo hicho ni 632.

Hitilafu ya kiuandishi - kubadili sita na tatu - ilifanya ionekane kana kwamba watu wengi walikuwa wamepiga kura kuliko jumla ya idadi ya wapiga kura - ambayo haikuwa hivyo.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Gachagua hakutambuliwa kwa kutumia sajili la kawaida

Screenshot of tweet by Makau Mutua claiming Rigathi Gachagua was identified using the manual register

Msemaji wa Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga alidai kuwa mgombea mwezna wa Bw Ruto alifanikiwa kupiga baada ya jina lake kuangaliwa katika sajili iliyochapishwa.

Bw. Makau Mutua alidai kuwa kifaa cha kielekroniki kilichotumiwa kuwatambua wapiga kura katika kituo cha kupiga kura kilikumbwa na hitilafu,kushindwa kumtambua Bw. Rigathi Gachagua ambaye muungano wake wa kisiasa umekuwa ukipinga matumizi ya daftari la kawaida.

https://twitter.com/makaumutua/status/1556924449114492928

Ingawa kifaa hicho cha kielektroniki kilikuwa na matatizo ya kumtambua Bw Gachagua, hatimaye kilifanya kazi baada ya kusugua kidole chake kwenye nywele zake na kumruhusu kupiga kura.

Akaunti ya Twitter ambayo haihusiani na IEBC

Screenshot of Fake IEBC account

Akaunti ya Twitter inayojiita IEBC Tabulation imekuwa ikichapisha baadhi ya matokeo ya uchaguzi na kutumia nembo ya tume ya uchaguzi kama picha ya wasifu na jalada.

Akaunti hiyo ambayo sasa imesitishwa, ilikuwa imeorodhesha anwani ya tovuti ya IEBC katika maelezo yake ambayo ingepotosha zaidi watu kuwa ni akaunti halali iliyounganishwa na tume hiyo.

Ukiangalia kwa karibu utakuwa na kila sababu ya kutilia shaka uhalali wake.

Iliundwa Aprili mwaka huu na imekuwa ikichapisha maudhui ya ngono kwa wiki kadhaa.

Baadhi ya machapisho ya hivi majuzi pia yalikuwa yanaonyesha upendeleo wa wazi kwa wagombeaji fulani wa kisiasa, jambo ambalo halikutarajiwa kutoka kwa akaunti rasmi.

Imesimamishwa kwa kukiuka sheria za Twitter.

Hakukua na upigaji kura nchini Australia

Screengrab of post claiming there was voting in Australia

Ujumbe uliosambaa kwenye mitandao ya kijamii ya WhatsApp, Twitter na Facebook zilidai upigaji kura wa nje ya nchi ulifanyika Sydney, Australia na kura tayari zimehesabiwa.

Jumbe hizo zilidai wapiga kura wote walijitokeza na ulikuwa ushindi kwa Bw Odinga.

Tofauti za ujumbe huu ziliachwa Sydney.

Lakini haya yote yaliundwa kwani hakukuwa na upigaji kura unaofanyika nchini Australia.

Tume ya uchaguzi inasema zoezi la kupiga kura kwa Wakenya wanaoishi nje ya nchi linafanyika katika nchi zifuatazo: Burundi, Tanzania, Rwanda, Uganda, Afrika Kusini, Uingereza, Canada, Marekan, Sudan, Kusini,Qatar, UAE, na Ujerumani.

Australia haikuwa miongoni mwa nchi hizo,

Na ubaloi wa Kenya uko katika mji wa Canberra na walasio Sydney.

.

IEBC ina siku saba kutangaza matokeo.

Election branding
Reality Check branding