Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Majirani wa Kenya wanajifunza nini?

Uhuru
    • Author, Lizzy Masinga
    • Nafasi, BBC Swahili
  • Muda wa kusoma: Dakika 4

Shughuli ya kuhesabu kura kwa sasa zinaendelea mara baada ya vituo vya kupiga kura kufungwa huku hesabu ya kura za urais ikipewa kipaumbele.

Kura hii ni baada ya kampeni kali iliyotawaliwa na mijadala kuhusu gharama za maisha, ukosefu wa ajira na ufisadi.

Wanaogombea wakuu wa urais ni aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga na Naibu Rais wa sasa William Ruto.

Wafula Chebukati ,mwanasheria ndiye mwenyekiti wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka (IEBC) inayohusika na mchakato mzima wa uchaguzi nchini Kenya.

Wakati Kenya ikijiandaa kumpokea mshindi wa uchaguzi wa urais nchini humo, jina la Wafula Chebukati ni muhimu sana katika uchaguzi wa mwaka huu, na alitarajiwa na vyama, miungano ya kisiasa , wagombea binafsi na Wakenya kwa ujumla kuendesha uchaguzi wa haki na huru ili kuhakikisha Kenya inakuwa na amani na utulivu.

Bwana Chebukati mwenye umri wa miaka 60, sio mgeni katika wadhfa wa Mwenyekiti wa IEBC. Alikula kiapo cha kuongoza tume hiyo kwa mara ya kwanza tarehe 20 Januari mwaka 2017, alipomrithi mtangulizi wake Issack Hassan.

'Mwanaume asiyetetereka'

Huku akijiandaa kumtangaza mshindi wa urais, ni dhahiri kwamba wakili huyu mwenye ''haiba ya upole'' anafahamika na wengi kuwa mtu asiyetetereka wala kuyumbishwa anapofanya kazi yake.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Ni mtu anayeongea kwa sauti ya upole na utaratibu, lakini kwa wanaomfahamu si mtu mwenye kutafuna maneno na mara nyingi anachokiongea ndicho anachokimaanisha.

Msimamo wake umekuwa na mvuto sana kwa wanaomfuatilia na kuifuatilia taasisi anayoisimamia

Majirani wa Kenya wanasema nini kuhusu uchaguzi huu?

Wakenya na raia mbali mbali wa nchi za Afrika Mashariki wametoa maoni yao kuhusu mwenendo wa uchaguzi nchini Kenya hususani mwenendo wa kura zilivyopigwa, zinavyohesabiwa na namna matokeo yanavyotoka.

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Masuala mengine yaliyozua mjadala ambayo yameonekana kuwa funzo kwa upande wa nchi nyingine za Afrika Mashariki ni uhuru wa kutoa maoni, uhuru wa mawakala wa vyama na wagombea wa nafasi mbalimbali.

Kutobinywa kwa mitandao ya kijamii

Hali imekuwa tofauti nchini Kenya na kufuta mtazamo kuwa kudhibitiwa kwa mitandao ni jambo la kawaida katika baadhi ya mataifa ya Afrika, ambako serikali zimekuwa zikizima mitandao ya intaneti mara kwa mara au kuzuia mitandao ya kijamii.

Wanaharakati wa kutetea haki katika dijitali wanasema ni kubana taarifa, lakini serikali zinadai inasaidia kuimarisha usalama,kwa Kenya hali imekuwa tofauti sana na ilivyokuwa ikidhaniwa.

Wakati wote wa Kampeni, kupiga kura na hata sasa ambapo kura zimeendelea kuhesabiwa nchini Kenya, mitandao ya kijamii imekuwa ikiendelea kutumiwa na raia wa Kenya, jambo ambalo limewavutia wengi wanaoufuatilia uchaguzi wa Kenya kwa karibu.

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Ruka X ujumbe, 3
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 3

Ruka X ujumbe, 4
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 4

Mara nyingi wakati wa uchaguzi huwa kuna kizuizi kinachowekwa kuwazuia watu kuingia katika mitandao ya kijamii inayotumika sana.

Kwa hatua kali zaidi, serikali inaweza kuagiza kufungwa kabisa kwa huduma nzima ya intaneti.

Visa vya kufungiwa au kubanwa kwa mtandao Afrika vimekuwa vikiongezeka.

Uganda ikielekea uchaguzi mkuu wa rais na wabunge uliofanyika Januari 14, mitandao ya kijamii ilikuwa imeshafungwa tayari.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Uganda iliagiza watoaji huduma za mtandao kufunga mitandao yote ya kijamii na programu za kutuma ujumbe hadi wakati usiojulikana, kwa mujibu wa barua kutoka kwa mdhibiti wa mawasiliano nchini humo iliyonukuliwa na shirika la habari la Reuters.

"Tume ya mawasiliano Uganda inaagiza kusitisha ufikiwaji na utumiaji, wa moja kwa moja au kinyume chake, kwa mitandao yote ya kijamii pamoja na programu za kutuma ujumbe mitandaoni hadi siku isiyojulikana," Barua kutoka kwa mkurugenzi mkuu wa tume ilisema hivyo kwa watoaji huduma za mtandao.

Watumiaji walikuwa wamelalamika kwamba hawakuweza kupata mtandao wa Facebook na WhatsApp, majukwaa ya mitandao ya kijamii inayotumiwa sana katika kipindi cha kampeni kabla ya uchaguzi wa urais kwenye nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

Baadhi ya Waganda wameona kuwa Kenya imetoa funzo kwa mataifa mengine.

Ruka X ujumbe, 5
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 5

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia nchini Kenya Joe Mucheru alisema hakukuwa na dalili zozote kwamba uchaguzi huo ungefanyika katika mazingira ambayo yangehitaji hatua hiyo ya kupindukia, lakini alisema kwamba Wakenya wanapaswa kutumia mitandao ya kijamii kwa uwajibikaji.

Mucheru alisema serikali ina haki ya kuchukua hatua zozote zinazohitajika ili kuhakikisha udumishaji wa utulivu wa umma, na kuongeza kuwa Wizara yake inafanya kazi kwa karibu na ile ya Mambo ya Ndani katika kutathmini vitisho vyovyote vinavyoweza kutokea na kujiandaa kwa hali yoyote.

th

Pia unaweza pia kusoma

Uchaguzi