Uganda haijakubali kuchukua watu waliofukuzwa kutoka Marekani, afisa wa ngazi ya juu asema

Chanzo cha picha, Reuters
Afisa mkuu wa Uganda alikanusha Jumatano ripoti ya vyombo vya habari vya Marekani kwamba nchi hiyo imekubali kuwachukua watu waliofukuzwa kutoka Marekani, akisema haina vifaa vya kuwahudumia.
Iikinukuu nyaraka za ndani za serikali ya Marekani, shirika la habari nchini humo, CBS News liliripoti Jumanne kwamba Washington imefikia makubaliano ya kuwahamisha Uganda na Honduras kama sehemu ya harakati zake za kuongeza kasi ya kuwafukuza wahamiaji katika nchi ambazo hawana uraia.
"Kwa ufahamu wangu hatujafikia makubaliano kama haya," Okello Oryem, waziri wa maswala ya kigeni aliiambia Reuters kwa ujumbe mfupi wa simu."Hatuna vifaa na miundombinu ya kuwahudumia wahamiaji haramu kama hao nchini Uganda.
"Serikali ya Honduras haikujibu mara moja ombi la Reuters la maoni juu ya ripoti hiyo.Rais Donald Trump analenga kuwafukuza mamilioni ya wahamiaji walioingia Marekani kinyume cha sheria na utawala wake umetaka kuongeza uhamisho hadi nchi za tatu , ikiwa ni pamoja na kuwatuma wahalifu waliopatikana na hatia nchini Sudan Kusini na Eswatini.
Ripoti ya CBS ilisema makubaliano na Uganda na Honduras yalitokana na kifungu cha sheria ya uhamiaji ya Marekani ambayo inaruhusu watu wanaotafuta hifadhi kuhamishwa hadi nchi za tatu ikiwa serikali ya Marekani itaamua mataifa hayo yanaweza kusikiliza madai yao kwa haki.
Soma zaidi:















