Aliyoyasema Trump baada ya mkutano wake na Rais Zelensky

Chanzo cha picha, PA Media
Muda mfupi uliopita, Donald Trump alizungumza kwenye Fox News, akitoa maoni yake kwa mara ya kwanza tangu rais wa Marekani na mwenzake wa Ukraine Volodymyr Zelensky kukutana katika Ikulu ya White house Jumatatu, pamoja na washirika wengine wa Ulaya.
Trump anasema anapanga mkutano kati ya kiongozi wa Urusi Vladimir Putin na Zelensky ambao hautamjumuisha hapo awali.
"Ikiwa hiyo itafanikiwa, basi nitakwenda na kuufunga," anasema.
Anasema anatumai Zelensky "ataonesha kubadilika" katika mazungumzo.
Trump anasisitiza kuwa wanajeshi wa Marekani hawatakuwa Ukraine kama sehemu ya dhamana ya usalama inayotafutwa na Kyiv.
Mataifa ya Ulaya kwa upande mwingine yanaweza kuwa na wanajeshi nchini Ukraine kama sehemu ya makubaliano, Trump anasema.
Pia anasema washirika wa Ukraine na Nato wanapaswa kuachana na juhudi za kuifanya Ukraine ijiunge na muungano wa usalama na kurejesha Crimea, ambayo Urusi iliikalia mwaka 2014.
"Mambo yote mawili hayawezekani," anasema.
Anasema mazungumzo yake na Putin jana haikufanyika mbele ya washirika wa Ulaya na Nato. "Nilidhani hiyo itakuwa ni dharau kwa Rais Putin," anasema.














