Sheria ya ushuru mpya wa redio kwa madereva yazua ghadhabu Zimbabwe

Chanzo cha picha, Bloomberg via Getty Images
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa ametia saini kuwa sheria muswada tata unaowataka madereva wote kununua leseni ya redio kabla ya kupata bima ya gari.
Kumekuwa na kilio kutoka kwa baadhi ya madereva kwani sasa watalazimika kulipa $92 (£68) kila mwaka ili kusikiliza redio kwenye magari yao.
Kuanzishwa kwa hatua hiyo ni sehemu ya mpango wa kupanua vyanzo vya mapato kwa shirika la utangazaji la serikali lakini wakosoaji wanasema ada ya leseni ni kubwa mno, hasa kutokana na hali ngumu ya kiuchumi.
Kiongozi wa upinzani Nelson Chamisa alisema sheria hiyo mpya "ni ya kibabe kupita kiasi, inachukia raia na haina huruma kabisa".
Akijibu wasiwasi wa madereva kwenye mitandao ya kijamii, Nick Mangwana, afisa mkuu katika wizara ya habari, alisema sheria hiyo mpya ni "lazima" na "ya haki".
Kuna takribani magari milioni 1.2 yaliyosajiliwa nchini lakini ni 800,000 tu kati yao yanalipa bima, kulingana na vyombo vya habari vya ndani.
Shirika la Utangazaji la Zimbabwe (ZBC) linalopata hasara linategemea mapato ya ada ya leseni pamoja na ruzuku ya serikali, Pia huzalisha baadhi ya mapato kupitia utangazaji.
Unaweza kusoma;












