Uchaguzi Kenya 2022: Jinsi mauaji ya afisa wa tume ya uchaguzi IEBC Chris Msando yanavyoendelea kuandama Uchaguzi wa Kenya

Chris Msando

Chanzo cha picha, Nation Media Group

Maelezo ya picha, Chris Msando, mkuu wa teknolojia katika tume ya uchaguzi ya Kenya, aliuawa miaka mitano iliyopita
    • Author, Na Dickens Olewe
    • Nafasi, BBC News, Nairobi

Uchaguzi uliotiliwa shaka Pamoja na mauaji ya kutisha ya afisa mkuu aliyesimamia teknolojia ya upigaji kura mwaka wa 2017 bado yanaikera Kenya, kabla ya uchaguzi wiki ijayo.

Mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na Mipaka amekuwa akijaribu mara kwa mara kuwahakikishia wananchi wenye wasiwasi kwamba tume yake inaweza kusimamia uchaguzi wa haki, lakini pia amekuwa akionya kuhusu kampeni iliyoratibiwa hasa kwenye mitandao ya kijamii kuwakashifu na kuwatisha wafanyakazi wake.

"Wafanyikazi wetu katika tume, hasa [wale] walio katika kitengo cha teknolojia ICT wana hofu... Ninataka tu kuwasihi wale wanowatisha kuwacha kufanya hivyo'' ,Wafula Chebukati aliwaambia wanahabari.

Ana sababu za msingi za kuwa na wasiwasi: miaka mitano iliyopita mkuu wake wa teknolojia wakati huo, Chris Msando, alitekwa nyara na kuuawa kikatili, pamoja na rafiki yake Carol Ngumbu mwenye umri wa miaka 21.

Miili yao ilipatikana vichakani viungani mwa mji mkuu, Nairobi - na hakuna mtu aliyekamatwa au kushtakiwa kwa mauaji hayo ambayo yamegubikwa na siri.

"Hakika tukiwa na huduma ya polisi yenye utaalamu wa juu na serikali yenye weledi na ufanisi nadhani tungefaa kujua ukweli kuhusu tukio hili ... Taifa halijui ni nani aliyechukua maisha ya afisa wa uchaguzi ambaye alikuwa akishughulikia sehemu nyeti sana ya uchaguzi," alisema Mkurugenzi mkuu wa shirika la haki za kibinadamu la Amnesty International Kenya akizungumza na kituo kimoja cha runinga nchini humo.

Kwa urafiki na utulivu, Msando alikuwa akitangaza katika vituo vya runinga vya hapa nchini, akionyesha hatua alizochukua kuhakikisha uchaguzi hauibiwi.

"Wapiga kura waliokufa hawatafufuka chini ya usimamizi wangu ," alisema katika mahojiano.

Alikuwa ameweka imani yake katika data za kibayometriki ili kuthibitisha wapiga kura kwa kutumia alama za vidole na mfumo wa kielektroniki kusambaza matokeo.

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Karatasi za kupigia kura zitakazotumika katika uchaguzi huo zilichapishwa nje ya nchi

Utumiaji wa teknolojia kama hiyo ulikubaliwa kufuatia kudorora kwa uchaguzi wa 2007 wakati shutuma za ujazo wa kura zilizusha ghasia za wiki kadhaa ambapo takriban watu 1,200 waliuawa na wengine 600,000 kutoroka makazi yao. Wakati huo mwenyekiti wa tume ya uchaguzi wakati huo alikiri hakuwa na uhakika ni nani aliyeshinda.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Uchaguzi huu pia unaonekana kuwa kinyang'anyiro kikali cha urais - kati ya vinara Raila Odinga, kiongozi wa upinzani wa muda mrefu ambaye anawania kwa mara yake ya tano, na Naibu Rais William Ruto.

"Teknolojia sio demokrasia"

Kufanya mambo kuwa makubwa zaidi, Rais anayeondoka Uhuru Kenyatta anamuunga mkono Bw Odinga, ambaye ni adui aliyegeuka kuwa mshirika wake, kumrithi kufuatia kuvunjika kwa uhusiano wake na Bw Ruto.

Wapiga kura pia watakuwa wakichagua magavana, maseneta, wabunge na madiwani wa bunge la kaunti.

Hata hivyo ongezeko la matumizi ya teknolojia katika kura tatu za uchaguzi tangu 2007 halijatoa uaminifu - na mwaka wa 2017 ilisababisha Mahakama ya Juu kubatilisha kura hiyo na kuamuru uchaguzi mpya.

"Licha ya kushindwa mwaka wa 2013, teknolojia zaidi ilinunuliwa mwaka wa 2017. Gharama ya uchaguzi ilipanda kutoka $10 [£8] kwa kila mpiga kura aliyejiandikisha katika uchaguzi wa kwanza hadi $25 katika uchaguzi wa marudio, na hivyo kuifanya Kenya kuwa na umaarufu wa kuandaa uchaguzi ghali zaidi barani Afrika," Nanjira Sambuli, mchambuzi wa teknolojia na utawala aliambia BBC.

"Teknolojia sio demokrasia," Bi Sambuli alisema.

Mahakama ya Juu iliamua kwamba kura hiyo ya Agosti 2017 ni "batili, batili na batili" kwani baadhi ya vituo 10,000 vilishindwa kusambaza kura.

"Hii ilikuwa idadi kubwa, pamoja na tume ya uchaguzi ilitoa visingizio walivyopotakiwa kufungua sava za kompyuta kwa ajili yakuangazia kile kilichotokea,Wakili wa kikatiba James Mamboleo aliambia BBC.

"Walisema tume lazima iwajibike kwa wananchi katika michakato yote kuanzia uandikishaji wapigakura hadi mfumo madhubuti wa usambazaji."

Uamuzi huo ulidhoofisha imani na Bw Chebukati, lakini alifaulu kusalia kazini licha ya shinikizo la kumtaka ajiuzulu.

Wakati huu tume itatumia tena makumi ya maelfu ya vifaa vya kuthibitisha wapigakura vilivyonunuliwa kwa marudio ya uchaguzi wa Oktoba 2017 na imeimarisha taratibu zake.

Watu ambao wanaweza kuthibitishwa na mfumo wa kielektroniki pekee ndio watakaopiga kura na picha ya matokeo itatumwa kidijitali kutoka zaidi ya vituo 50,000 vya kupigia kura badala ya ujumbe mfupi wa maandishi.

Hivi ndivyo itakavyofanya kazi kwa kura ya urais:

• Wapiga kura wote watalazimika kuthibitishwa kwa kutumia alama ya vidole au kitambulisho

• Baada ya upigaji kura kufungwa, picha ya fomu ya matokeo, iliyotiwa saini na afisa msimamizi na mawakala wa vyama, itasambazwa kwa njia ya kielektroniki kwa kutumia vifaa vilivyounganishwa vya kupigia kura kwa jimbo na kituo cha kitaifa cha kujumlisha kura.

• Nakala ya fomu itatolewa kwa mawakala wa vyama na kubandikwa nje ya kituo cha kupigia kura

• Vifaa vya uthibitishaji wa wapigakura vitafungwa katika vituo vya kupigia kura ili kuzuia udanganyifu

• Mshindi atatangazwa tu baada ya fomu halisi ya matokeo kupokelewa na tume ili kuthibitisha dhidi ya picha iliyotumwa mwanzoni.

"Itakuwa vigumu sana katika uchaguzi huu watu waende mahakamani kupinga matokeo tuliyonayo, kwa sababu tuko wazi kiasi kwamba hata wakitaka kwenda mahakamani wangefedheheka sana. "Mmoja wa makamishna wa tume ya uchaguzi, Justus Nyangaya, aliambia BBC.

Pia alisema kuwa kitambulisho cha wapigakura kitakuwa kikituma taarifa kwenye kituo cha kitaifa cha kujumlisha kura kila baada ya saa mbili, jambo ambalo anasema litapuuza majaribio ya kujaza masanduku ya kura.

Wafula Chebukati

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Bw Chebukati ni mwanamume aliye katika dhamira ya kujisafisha baada ya uchaguzi uliopita kubatilishwa

Akiwa bado anaonekana kuumizwa na uchaguzi uliopita, mwenyekiti wa tume ya uchaguzi pia amevitaka vyombo vya habari, vyama vya siasa na jumuiya za kiraia kufanya majumuisho yao ya kura.

"Chebukati ana nia ya kufanya marekebisho kwa kuwajibika kikamilifu kama mwenyekiti, na kuanzisha mfumo ambao utahakikisha uchaguzi huru, wa haki, wazi na unaoweza kuthibitishwa ili kujiondoa katika urithi wa mwenyekiti anayejulikana kwa chaguzi zenye mkanganyiko," mchambuzi wa kisiasa Hesbon Owila aliambia BBC.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

"Kama mtu binafsi amejifunza kutoka zamani, lakini kama Wakenya, tunaweza tu kuunga mkono lakini pia kuwa macho."

Bw Mamboleo anakubali: "Je, tume ya uchaguzi imejaribu kufuata viwango vya juu vilivyowekwa na uamuzi huo wa Mahakama ya Juu wa 2017? Kwa maoni yangu, ni ndiyo. Wameshirikisha vyama vya siasa, wagombea na umma kwa njia ambazo hatujaona. katika chaguzi zilizopita."

Wito wa haki

Kwa mujibu wa sheria, tume ya uchaguzi ina siku saba baada ya kura ya kuwatangaza washindi - na kwa kuhimiza vyombo vya habari na wengine kujumlisha matokeo Bw Chebukati anatumai kuwa uwazi utamhalalisha yeye na tume.

Bila shaka itakuwa hatua muhimu kwa Kenya ikiwa hii ingeafikiwa.

Wakati familia za Msando na Ngumbu zikiadhimisha kumbukumbu ya miaka mitano ya mauaji yao mwezi uliopita, walisema tena demokrasia ya Kenya inapaswa kuegemezwa katika utawala wa sheria - na walitumai siku moja wao pia watapata haki.

"Tunaomba kwamba siku moja tupate kujua ukweli," familia ya Msando iliandika katika kumbukumbu katika moja ya karatasi za ndani.

.

Uchaguzi Kenya 2022:Unaweza pia kusoma

.