Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Jinsi makabidhiano ya uongozi yanavyofanyika Kenya

Uhuru Kenyatta is sworn in

Chanzo cha picha, Reuters

Kenya inajitayarisha kuukaribisha utawala mpya wa serikali baada ya matunda ya mshindi wa moja kwa moja katika duru ya kwanza ya upigaji kura .

Mojawapo ya taratibu muhimu sana na ambazo zilianza mapema pindi tu matayarisho ya uchaguzi yalipokamilishwa.

Utaratibu huo umelindwa na katiba na una miongozo ya kimsingi ili kuufanikisha ni makabidhiano ya uongozi kutoka kwa rais mmoja hadi mwingine.Rais Uhuru Kenyatta ambaye amemaliza kipindi chake cha mihula miwili ya miaka 10 atakuwa akimkabidhi hatamu mrithi wake.

Kwa mujibu wa Sheria ya Makabidhiano ya Ofisi ya Rais, Serikali iliyopo madarakani inafaa kuunda kamati ijulikanayo kwa jina la Kamati ya kukabidhi madaraka ya Ofisi ya Rais ili kuendesha mchakato huo angalau siku 30 kabla ya Uchaguzi Mkuu.

Rais kenyatta tayari alishaitangaza kamati hiyo ambayo itasimamia mchakato mzima wa serikali yake kuipa madaraka serikali ijayo .

Lakini mchakato huu unahusisha nini na akina nani?

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Rais anayeondoka kupoteza mamlaka

Rais Uhuru Kenyatta alipoteza mamlaka kadhaa mnamo Agosti 9, wakati Wakenya walipoanza kupiga kura kuchagua viongozi wapya .

Rais siku hiyo aliingia kwenye awamu ya "Uongozi wa muda" maana yake atakuwa ameshikilia kiti kama kiongozi wa muda akijiandaa kumkabidhi Mkuu wa nchi ajaye.

Katiba inamnyima mamlaka fulani katika awamu hii.

Sura ya Tisa (9), Sehemu ya Pili (2), Ibara ya 134 ya Katiba ya Utekelezaji wa Madaraka ya Urais Wakati wa Uongozi wa Muda inasema Mkuu wa Nchi anayemaliza muda wake anapoteza mamlaka ya kuteua majaji wa Mahakama za Juu.

Wakati huo huo, rais anapoteza mamlaka ya kuteua afisa yeyote wa umma; kuteua au kumfukuza kazi waziri (CS), Katibu wa kudumu (PS) na maafisa wengine wa Serikali.

Pia anasalimisha mamlaka ya kuteua, kuchagua au kutengua kamishna mkuu, balozi, au mwakilishi wa kidiplomasia au ubalozi.

Rais pia amenyimwa uwezo wa kutumia nguvu ya huruma, maana yake hawezi kuwasamehe wafungwa.

Kenyatta pia ataacha mamlaka ya kutoa heshima kwa jina la wananchi na Jamhuri.

Kipindi cha "uongozi wa muda" huanza siku ambayo Wakenya watapiga kura na kinaisha wakati rais mpya aliyechaguliwa anaanza kutekeleza majukumunyake.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Maandalizi ya kuapishwa kwa rais mteule

Siku ya kuapishwa, msafara wa rais utakuwa umesimama katika makao ya rais mteule na naibu wake na watalindwa vikali na kikosi cha maafisa wa Kitengo cha (GSU) ambao watawaongoza kwenye hafla ya kuapishwa.

Msafara wa rais ambao utakuwa na idadi sawa ya magari na yale ya kawaida ya rais anayeondoka, utaelekea kwenye eneo la kuapishwa ambalo huenda likawekwa katika uwanja wa kitaifa ama ukumbi wowote utakaotangazwa kutumiwa na kamati ya makabidhiano .Rais Uhuru Kenyatta aliapishwa katika uwanja wa Kasarani.

Rais Mteule anatarajiwa kuapishwa Jumanne ya kwanza kufuatia siku ya kumi na nne baada ya tarehe ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa urais, ikiwa hakuna ombi lililowasilishwa kortini kupinga matokeo hayo, atapewa haki zote za urais anazopata mtangulizi wake hata kabla ya kula kiapo.

Wakati akielekea kwenye uwanja vya kuapishwa, rais ajaye atafahamishwa kuhusu vipengele vya serikali kama vile miundo ya serikali, taarifa za ujasusi, hali ya uchumi na maelezo kamili ya mchakato wa kuapishwa.

Kabla ya hafla hiyo, kamati ya maandalizi itatuma bendera ya rais kwa Kamati ya Sare za nchi ili kufanyiwa muundo. Bendera hiyo maalum ya rais itatengezwa kumpendeza rais mteule.

Majina ya wageni na viongozi wote watakaohudhuria hafla hiyo pia yatatumwa kwa kamati ya uongozi na rais mteule na Mkuu wa nchi anayemaliza muda wake.

Sherehe ya kuapishwa

Sherehe za kuapishwa zitaanza saa nne asubuhi hadi saa nane mchana huku eneo la hafla hiyo likifunmguliwa kwa umma mapema saa kumi na mbili asubuhi.

Mara tu Wakenya na wageni wote wanaohudhuria watakapotulia, msafara wa Rais mteule na ule wa naibu wake utaingia katika uwanja huo ukiambatana na gwaride la kijeshi ambalo litakuwa tayari watakapowasili.

Baada ya hapo rais anayemaliza muda wake atajitokeza kwa sherehe ya makabidhiano na itatanguliwa na kipindi kifupi cha maombi na burudani kutoka wasanii mbalimbali.

Jaji Mkuu atamuapisha rais mteule pamoja na Msajili wa Mahakama Kuu.

Mara tu rais mteule atakapoapishwa naibu wake vile vile atakula kiapo cha afisi ambapo Rais Kenyatta atakabidhi vyombo vya mamlaka kama vile Katiba na upanga wa mamlaka kwa rais mpya.

Naibu rais aliyeapishwa atapanda jukwaani kutoa hotuba na kisha atamwalika rais anayeondoka madarakani. Hotuba zao zitatayarishwa na kamati ya maandalizi.

Baada ya hayo, Mkuu wa Nchi anayeondoka atamkaribisha rais ajaye wa Kenya jukwaani kutoa hotuba yake. Wimbo wa taifa utapigwa huku bendera ya rais ikibadilishwa ili kuendana na utawala mpya.

Rais anayemaliza muda wake ataondoka kuelekea Ikulu ili kukabidhi rasmi ikulu kwa mrithi wake. Wakati huo huo, rais aliyeapishwa atazungushwa uwanjani kwa gari la wazi kuwasalimu Wakenya waliohudhuria na kisha atapelekwa hadi Ikulu kwa mazungumzo na rais anayeondoka madarakani.

Baada kikao kifupi , rais anayemaliza muda wake ataondoka katika majengo hayo kuashiria kuwa utawala mpya umeingia rasmi madarakani.

th

Uchaguzi Kenya 2022:Unaweza pia kusoma

th