Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022:Ngoja ngoja ya muda mrefu huku kura za urais zikionyesha Raila Odinga na William Ruto wamekabana koo

Residents look at newspapers displayed at a stand in Mathare, Nairobi following Kenya's general election on 12 August 2022

Chanzo cha picha, AFP

    • Author, Dickens Olewe
    • Nafasi, BBC News

Mfumo wa kuhesabu kura nchini Kenya haujaingiliwa kwa njia yo udukuzi huku kukiwa na ukosefu wa Subira ya matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumanne, afisa mkuu wa uchaguzi amesema.

"Hakuna kitu kama hicho kilichotokea. Ni habari potofu," Afisa mkuu mtendaji wa tume ya uchaguzi Marjan Hussein Marjan alisema.

Mitandao ya kijamii imekumbwa na madai kuwa matokeo ghushi yamepakiwa huku hesabu hiyo ikithibitishwa.

Taratibu za vyombo vya habari zinaonyesha wagombeaji wawili wakuu - Raila Odinga na William Ruto - wapo katika ushindani mkali.

Lakini ni tume ya uchaguzi pekee ndiyo inaweza kutangaza mshindi - na ina siku saba kufanya hivyo.

"Tulitarajia kwamba watu wangejaribu kudukua mifumo yetu... tunaihakikishia nchi nzima kwamba mifumo yetu iko salama," Bw Marjan aliwaambia waandishi wa habari Ijumaa alasiri.

Awali mkuu wa uchaguzi Wafula Chebukati alisisitiza kuwa hakuna haja ya kuogopa kuona tofauti za idadi ya watu kutoka makundi mbalimbali ya vyombo vya habari kwani zitafanana mwishowe: "Matokeo yanatoka kwenye tovuti moja ya umma; mbinu [ya kila chombo cha habari] ni tofauti. ."

Ni nini kinaendelea katika kituo kikuu cha kuhesabia kura?

Haya yanajiri katika kituo cha kitamaduni kiitwacho Bomas katika mji mkuu, Nairobi, ambapo maafisa kutoka Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) wanashughulika na kuthibitisha matokeo.

Wanalinganisha picha za fomu za matokeo kutoka zaidi ya vituo 46,000 vya kupigia kura nchi nzima na fomu halisi zinazoletwa na maafisa kutoka kila moja ya maeneo bunge 290.

Hii ni kuhakikisha kuwa matokeo yanalingana.

Haya yanashuhudiwa na maajenti wa vyama kutoka vyama vikuu, ambao Bw Chebukati anasema wanaendelea kuchelewesha hilo kwa kuligeuza kuwa la "uchunguzi" wa matokeo.

Alisema maafisa hawapaswi kuchukua zaidi ya dakika 15 kuthibitisha matokeo.

Shughuli ya kuhesabu kura katika baadhi ya vituo pia ilicheleweshwa na kusafiri hadi Nairobi, haswa na maafisa kutoka maeneo ya mbali, kunaweza kuwa sababu zaidi ya kupunguza kasi ya mambo.

Uthibitishaji pia ulisitishwa kwa muda siku ya Ijumaa baada ya mzozo kuzuka, unaodaiwa kuhusisha mtu asiye na kibali kuonekana na kompyuta ndogo.

Maelezo ya video, Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Kitu gani kinaweza kutokea baada ya matokeo kutangazwa

Je, hesabu za vyombo vya habari zinafanywa vipi?

Vikundi vya waandishi wa habari wanaofanya kazi katika vituo mbalimbali vimekuwa na kazi kubwa ya kuweka takwimu zilizopokelewa kutoka kwa kila kituo cha kupigia kura moja baada ya nyingine.

Kila chombo cha habari kinafanya hivyo kwa kasi tofauti na kuchagua vituo vya kupigia kura kwa mpangilio tofauti.

Kufikia Ijumaa asubuhi, vyombo vya habari vya ndani vilikuwa vimepunguza kasi ya hesabu yao - ingawa sababu haiko wazi, wengine wakisema wafanyikazi walikuwa wamechoka.

Bw Chebukati alisema alitumai makundi ya wanahabari yangeungana ili kujumlisha matokeo, lakini wameamua kila moja kufanya kivyake.

Wakenya wanajisikiaje?

Kuna hali ya wasiwasi nchini kwani chaguzi zilizozozaniwa huko nyuma zilisababisha vurugu au mchakato mzima kufutwa.

Kufuatia kura ya 2007, takriban watu 1,200 waliuawa na 600,000 walikimbia makazi yao kufuatia madai ya kuibiwa kwa kura.

Mnamo 2017, hitilafu kubwa za vifaa zilisababisha Mahakama ya Juu kubatilisha matokeo na kuamuru uchaguzi wa urais urudiwe.

Viongozi wanakabiliwa na shinikizo la kurekebisha mambo wakati huu.

Nchi mara nyingi hukwama wakati wa uchaguzi, shughuli kote nchini zimepungua na shule zimefungwa angalau hadi wiki ijayo Jumatatu. Kati kati mwa Nairobi, mitaa yenye shughuli nyingi mara nyingi haina watu.

Madai ya wizi wa kura ni ya zamani kama nchi. Ilikuwa ni sehemu ya siasa hata kabla ya chaguzi za vyama vingi kuanzishwa tena katika miaka ya 1990, lakini msukumo wa uchaguzi huru na wa haki haujawahi kulegalega.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Baada ya ghasia zilizofuatia uchaguzi wa 2007, vyama vya siasa na wanaharakati walibishania matumizi ya teknolojia badala ya sajili halisi, ambayo inaweza kubadilishwa kwa urahisi, ili kuhakiki wapiga kura.

Uchaguzi wa mwaka huu ni mara ya tatu kwa teknolojia kutumika lakini bado haujafanya uchaguzi ambao haujapingwa mahakamani.

Wakati huo huo, kundi la watumishi wakuu wa umma waliwaambia waandishi wa habari siku ya Ijumaa kwamba maandalizi ya kukabidhi madaraka kwa njia laini yataanza punde tu tume ya uchaguzi itakapomtangaza rais mteule.

Tutajua matokeo lini?

Haijulikani ni lini matokeo ya mwisho yatajulikana, lakini tume ya uchaguzi imeanza kutangaza hesabu zilizothibitishwa kutoka kwa maeneo bunge 290.

Iwapo kuna kiongozi wazi wa kinyang'anyiro hicho, huenda sherehe zikazuka - lakini IEBC pekee ndiyo inaweza kufanya hivyo rasmi.

Ili kushinda kinyang'anyiro cha urais katika awamu ya kwanza, mgombea anahitaji:

• zaidi ya nusu ya kura zote zilizopigwa kote nchini

• Takribani 25% ya kura zilizopigwa katika kaunti zisizopungua 24

Vinginevyo upigaji kura unakwenda kwa duru ya pili ambayo kwa mujibu wa sheria inapaswa kufanyika ifikapo tarehe 8 Septemba.

th

Uchaguzi Kenya 2022:Unaweza pia kusoma

th