Matokeo ya Uchaguzi Kenya 2022: Wanawake waliong’ara katika uchaguzi

Linet Chepkorir 'Toto'

Chanzo cha picha, Linet Chepkorir 'Toto'/TWITTER

Maelezo ya picha, Linet Chepkorir 'Toto'
    • Author, Asha Juma & Dinah Gahamanyi
    • Nafasi, BBC Swahili

Huku matokeo rasmi ya uchaguzi mkuu nchini Kenya yakiendelea kutolewa, katika uchaguzi wa mwaka huu wanawake wameonekana kuibuka washindi na kujinyakulia viti mbali mbali.

Hii inajiri huku Kenya ikiwa bado haijaweza kutekeleza sheria ya theluthi mbili ya uwakilishi wa jinsia, jambo ambalo limekuwa likilalamikiwa na wanawake kwamba linawanyima wao fursa ya uwakilishi katika ngazi za uongozi.

Hatahivyo katika uchaguzi huu wanawake wameweza kujitokeza na kupata ushindi utakaowawezesha kupata fursa hiyo.

Baadhi ya waliojinyakulia viti ni sura ngeni huku wengine wakirejea au kubadilisha nyadhifa.

Linet Chepkorir 'Toto'

Akiwa mbunge mwanamke mwenye umri mdogo zaidi, Linet Chepkorir mweye umri wa miaka 24 amechaguliwa kuwa mbunge wa kiti cha uwakilishi wa wanawake yaani (Women Rep) kutoka jimbo la Bomet katika Bonde la Ufa.

'Toto' alipata umaarufu hivi maajuzi baada ya kushinda tiketi ya chama cha Muungano wa United Democratic Alliance (UDA) unaoongozwa na Naibu Rais William Ruto kwenye uchaguzi wa ngazi ya vyama na kumshinda Joyce Korir.

Atakuwa mwakilishi mdogo zaidi katika bunge la 13.

Agnes Pareiyo aweka historia kama mbunge mwanamke wa kwanza Narok

Agnes Pareiyo
Maelezo ya picha, Agnes Pareiyo

Mwanaharakati wa kupambana na ukeketwaji wa wanawake, Bi Agnes Pareiyo amechaguliwa kuwa mbunge wa kwanza wa eneo la Narok Kaskazini.

Ni mgeni katika siasa za Kenya awali akifahamika kwa harakati zake za kupambana na ukeketaji wa wanawake ambapo mwaka 2018 aliendesha kampeni iliyoitwa END FGM ambapo wanaharakati walituma jumbe kwenye mitandao ya kijami kupitia hashtag 'DontTouch FGMLaw'.

Bi Pareiyo alizua gumzo na kuvunja ukimya wa kile kilichoonekana kama kisichowezekana katika jamii ya Kimasai kwa kuchaguliwa kuwa mbunge wa kwanza mwanamke.

Eneo bunge la Narok Kaskazini liliongozwa na marehemu William Ole Ntimama kabla ya Moitalel Ole Kenta kuchukua nafasi hiyo ambaye kwenye uchaguzi huu anawania nafasi ya ugavana wa Narok.

Mnamo 2017, aligombea kwa tiketi ya chama cha Jubilee lakini akashindwa na Kaitikei Rotiken kwenye kura za mchujo za chama.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Ruweida Obbo

Ruweida Obbo

Chanzo cha picha, Captain Ruweida Obbo/FACEBOOK

Maelezo ya picha, Captain Ruweida Obbo

Ruweida Obbo, mwanamke wa kwanza rubani wa kibajuni, ndiye aliyepata ushindi wa kiti cha ubunge katika jimbo la Lamu Mashariki.

Kabla ya kuchaguliwa kwake, Ruweida Obbo al Maarufu ''Captain Ruweida'' alikuwa mbunge wa kiti cha uwakilishi wa wanawake katika Bunge la taifa.

Pia aliahidi kuendeleza uwezeshaji wa wanawake, watoto na watu wenye mahitaji maalum.

Wakati wa kampeni zake za kisiasa, Bi Obbo alikuwa ameahidi kutoa hamasa juu ya utumizi wa dawa za kulevya ambao unaendelea kuathiri vijana wengi Lamu.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Gladys Wanga

Gladys Wanga

Wanga anaingia katika historia kama gavana mwanamke mwenye umri mdogo zaidi na gavana wa kwanza katika eneo la Nyanza.

Gladys Wanga amemuangusha mpinzani wake wa karibu aliyekuwa gavana wa Nairobi Dkt. Evans Kidero.

Alikuwa mwanamke wa kwanza mwenyekiti wa chama cha ODM katika eneo la Homa Bay na pia wa kwanza kuongoza Kamati ya Kitaifa ya Fedha na Mipango ya Kitaifa.

Akizungumza wakati wa kampeni zake, Wanga aliwaahidi wakazi wa Homa Bay atatumia rasilimali zilizogatuliwa kuboresha maisha ya wananchi na kuendeleza kaunti ya Homa bay.

"Kama kijana naamini nina nafasi ya kutengeneza urithi, sio ule ninaouacha bali ule ninaoishi, kwa maana ya kwamba ninapofanya vibaya naweza kuishi miaka mingi kuona ubaya, na ninapofanya kilicho sawa, ninaishi kuona mema ambayo nimefanya," alisema.

Alifichua kwamba alijihusisha na siasa akiwa na umri wa miaka mitano aliposaidia kusambaza 'chumvi' kwa wanakijiji wakati wa kampeni za uchaguzi za babake.

Wanga pia angeandamana na babake kwa shughuli za kisiasa na mikutano.

Kawira Mwangaza

Kawira Mwangaza

Chanzo cha picha, Kawira Mwangaza/FACEBOOK

Maelezo ya picha, Kawira Mwangaza gavana mteule kaunti ya Meru

Mwakilishi wa wanawake wa Meru Kawira Mwangaza, ameshangaza wengi kwa kuwabwaga vigogo wa kisiasa Mithika Linturi na gavana anayeondoka Kiraitu Murungi kwenye kinyang'anyiro cha kumchagua gavana wa kaunti ya Meru.

Mwangaza, ambaye alishindana kama mgombea huru amefanikiwa kuibuka na ushindi baada ya kutawala siasa za humu nchini kwa miaka mingi.

Bi Mwangaza, aliyekuwa mbunge kwa mara ya kwanza, alitangaza nia ya kumwondoa madaraka gavana wa Meru, Kiraitu Murungi mwaka wa 2019.

Mwakilishi huyo wa kike, ambaye pia ni mwanzilishi na askofu wa Kanisa la Baite Family Fellowship, alimteua Isaac Mutuma, kasisi wa Kanisa hilo kama mgombea mwenza wake.

"Nimemtambua Isaac Mutuma kama mgombea mwenza wangu katika kinyang'anyiro cha Agosti. Hii ni timu ya watu wenye ujuzi wa hali ya juu na watumishi wa watu. Siwezi kuteua bila maombi," alisema.

Katika ulingo wa kisiasa, Bi Mwangaza ameonyesha umahiri wake katika ujuzi alionao wa kuhamasisha watu mashinani.

Bi Mwangaza ameahidi kuwapa wakazi wa Meru uongozi bora kupitia matumizi ya busara ya pesa za umma.

Pia ameshinda uungwaji mkono wa kasisi Kiambi Atheru, ambaye alikuwa amepanga kuwania ugavana kwa mara ya pili mwaka huu, baada ya kushindwa mwaka wa 2017.

Wavinya Ndeti

TH

Chanzo cha picha, @WAVINYA_NDETI

Wavinya Ndeti alijiunga na siasa mwaka wa 2007 akigombea na kuchaguliwa kuwa mbunge wa eneo bunge la Kathiani chini ya Chama Cha Uzalendo (CCU).

Katika kushinda kiti hicho, Ndeti alikuwa mwanamke pekee aliyewakilisha eneo bunge hilo tangu uhuru.

Ndeti aliteuliwa katika serikali kuu ya muungano kama Waziri Msaidizi wa Vijana na Michezo chini ya Helen Sambili.

Ndeti, ni mmoja wa wanachama waanzilishi wa Muungano wa Mageuzi na Demokrasia - CORD, ulikuwa muungano wa vyama vingi vya kisiasa vilivyojengwa kwa karibu na Raila Odinga, Kalonzo Musyoka, na Moses Wetangula, kuwania uchaguzi mkuu wa Kenya wa 2013.

Ndeti, aliwania kiti cha Gavana wa Machakos kwa tiketi ya CCU mwaka wa 2013. Alimchagua aliyekuwa waziri wa Maji na Maliasili Mutua Katuku kama mgombea mwenza wake.

Katika uchaguzi wa mwaka huu uliofanyika Agosti 9, Wavinya ndeti amejitosa kwenye kusaka kiti cha ugavana kupitia chama cha Wiper na Gavana wa Machakos anayeondoka Alfred Mutua wa chama cha Maendeleo Chap Chap, alimuunga mkono kwenye ugombea wake.

"Ninakubali kwa ukarimu kuidhinishwa na gavana anayeondoka Dkt. Alfred Mutua na ninathamini kujitolea kwake kwa umma kunipigia kura. Ni faida kubwa kwetu na inatusaidia sana kuonyesha imani kuwa timu yetu pekee ndiyo inayohitaji kuongoza Kaunti," alisema alipoidhinishwa.

Wavinya ndiye ndiye mzaliwa wa mwisho kati ya watoto 10 wa Ndeti, lakini kati ya hao wote, ni yeye tu na marehemu kaka yake, Ignatius Dick Ndeti walioingia kwenye siasa. Dick Ndeti alikuwa diwani wa Athi River baada ya babake.

Susan Kihika amwangusha kigogo Lee Kinyanjui

Suzane

Chanzo cha picha, Kenya Parliament

Maelezo ya picha, Susan Kihika

Seneta wa Nakuru Susan Kihika wa chama cha United Democratic Alliance (UDA) amemwangusha kigogo Lee Kinyanjui wa chama cha Jubilee katika kinyang'anyiro cha ugavana kaunti ya Nakuru.

Susan Wakarura Kihika alichaguliwa katika bunge la seneti mwaka wa 2017.

Katika uchaguzi wake, aliteuliwa kuwa kinara wa wengi wa chama cha Jubilee.

Alishikilia wadhifa huo hadi tarehe 11 Mei 2020 ambapo nafasi yake ilichukuliwa na Seneta Irungu Kangata.

Ni mmoja wa viongozi waliojiondoa katika chama cha Jubilee pamoja na naibu rais baada ya makubaliano ya maridhiano kati ya Rais Uhuru na kiongozi wa ODM Raila Odinga.

th

Pia unawezakusoma:

th