Maelezo ya picha, Linet Chepkorir 'Toto'Maelezo kuhusu taarifa
Author, Asha Juma & Dinah Gahamanyi
Nafasi, BBC Swahili
Huku matokeo rasmi ya uchaguzi mkuu nchini Kenya yakiendelea kutolewa, katika uchaguzi wa mwaka huu wanawake wameonekana kuibuka washindi na kujinyakulia viti mbali mbali.
Hii inajiri huku Kenya ikiwa bado haijaweza kutekeleza sheria ya theluthi mbili ya uwakilishi wa jinsia, jambo ambalo limekuwa likilalamikiwa na wanawake kwamba linawanyima wao fursa ya uwakilishi katika ngazi za uongozi.
Hatahivyo katika uchaguzi huu wanawake wameweza kujitokeza na kupata ushindi utakaowawezesha kupata fursa hiyo.
Baadhi ya waliojinyakulia viti ni sura ngeni huku wengine wakirejea au kubadilisha nyadhifa.
Akiwa mbunge mwanamke mwenye umri mdogo zaidi, Linet Chepkorir mweye umri wa miaka 24 amechaguliwa kuwa mbunge wa kiti cha uwakilishi wa wanawake yaani (Women Rep) kutoka jimbo la Bomet katika Bonde la Ufa.
'Toto' alipata umaarufu hivi maajuzi baada ya kushinda tiketi ya chama cha Muungano wa United Democratic Alliance (UDA) unaoongozwa na Naibu Rais William Ruto kwenye uchaguzi wa ngazi ya vyama na kumshinda Joyce Korir.
Atakuwa mwakilishi mdogo zaidi katika bunge la 13.
Agnes Pareiyo aweka historia kama mbunge mwanamke wa kwanza Narok
Maelezo ya picha, Agnes Pareiyo
Mwanaharakati wa kupambana na ukeketwaji wa wanawake, Bi Agnes Pareiyo amechaguliwa kuwa mbunge wa kwanza wa eneo la Narok Kaskazini.
Ni mgeni katika siasa za Kenya awali akifahamika kwa harakati zake za kupambana na ukeketaji wa wanawake ambapo mwaka 2018 aliendesha kampeni iliyoitwa END FGM ambapo wanaharakati walituma jumbe kwenye mitandao ya kijami kupitia hashtag 'DontTouch FGMLaw'.
Bi Pareiyo alizua gumzo na kuvunja ukimya wa kile kilichoonekana kama kisichowezekana katika jamii ya Kimasai kwa kuchaguliwa kuwa mbunge wa kwanza mwanamke.
Eneo bunge la Narok Kaskazini liliongozwa na marehemu William Ole Ntimama kabla ya Moitalel Ole Kenta kuchukua nafasi hiyo ambaye kwenye uchaguzi huu anawania nafasi ya ugavana wa Narok.
Mnamo 2017, aligombea kwa tiketi ya chama cha Jubilee lakini akashindwa na Kaitikei Rotiken kwenye kura za mchujo za chama.
Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?
Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya
Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake
Raila Amollo Odinga
Muungano wa Azimio la Umoja
Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.
William Samoei Ruto
Muungano wa Kenya Kwanza
Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC
George Wajackoyah
Chama cha Roots
Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito
David Mwaure Waihiga
Chama cha Agano
David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
Kupambana na ufisadi uliokithiri.
kuunda nafasi za ajira.
Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.
Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa
Ruweida Obbo
Chanzo cha picha, Captain Ruweida Obbo/FACEBOOK
Maelezo ya picha, Captain Ruweida Obbo
Ruweida Obbo, mwanamke wa kwanza rubani wa kibajuni, ndiye aliyepata ushindi wa kiti cha ubunge katika jimbo la Lamu Mashariki.
Kabla ya kuchaguliwa kwake, Ruweida Obbo al Maarufu ''Captain Ruweida'' alikuwa mbunge wa kiti cha uwakilishi wa wanawake katika Bunge la taifa.
Pia aliahidi kuendeleza uwezeshaji wa wanawake, watoto na watu wenye mahitaji maalum.
Wakati wa kampeni zake za kisiasa, Bi Obbo alikuwa ameahidi kutoa hamasa juu ya utumizi wa dawa za kulevya ambao unaendelea kuathiri vijana wengi Lamu.
Kufikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
Elimu Bure kwa wote.
Huduma ya afya bora kwa wote.
Uchumi
Kukuza sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi na uchumi wa bluu hadi asilimia 30 ya Pato la Taifa.
Kuza bidhaa za "Zilizotengezwa Kenya" kwa kusaidia ukuaji wa biashara ndogo ndogo na za kati.
Mpango wa "Kaunti Moja, Bidhaa Moja" kutegemea utengenezaji kama injini ya uundaji wa utajiri na ajira.
Ufisadi
Kuboresha kwa haraka mamlaka ya kisheria na kiutawala.
Kuongeza kasi ya kurejesha mapato ya rushwa na uwepo wa fedha haramu.
Kutovumilia rushwa.
Madeni
Kupunguza kasi ya ulimbikizaji wa madeni.
Boresha sera za usimamizi wa madeni.
Kuendeleza mazungumzo ya msamaha wa madeni.
Ajira
Kutumia vizuri idadi kubwa ya vijana kwa ustawi
Kuboresha tija katika sekta ya viwanda na kusaidia uzalishaji wa ajira katika sekta hiyo.
Wekeza katika teknolojia zinazoibukia ambazo zitatoa fursa za ajira kwa vijana wa Kenya.
Kawi
Punguza gharama ya umeme.
Tathmini ushuru na kodi za bidhaa za petroli.
Kuongeze utafutaji wa mafuta na gesi kwenye nchi kavu na baharini.
Afya
Huduma ya afya bora kwa wote.
Kukuza uzalishaji wa ndani wa dawa na pembejeo nyingine zinazohusiana na afya.
Kuboresha mazingira ya kazi na malipo ya wataalamu wa afya.
Uhalifu na usalama
Kuhakikisha utekelezaji madhubuti wa mageuzi ya polisi.
Kuwafunza angalau maafisa sita wa polisi katika kila kituo cha polisi kushughulikia uhusiano wa polisi na vijana.
Boresha sheria na sera kuhusu usalama na usalama mtandaoni.
Elimu
Kutoa elimu bure kuanzia chekechea hadi chuo kikuu.
Toa mlo mmoja kwa siku kwa watoto wa chekechea na madarasa ya mwanzo ya shule za msingi
Kukuza uhusiano wa kufanya kazi kati ya taasisi za elimu na utafiti na viwanda.
Usambazaji wa maji
Wekeza na kukuza uvunaji wa maji ya mvua na udhibiti wa mafuriko.
Kupanua miundombinu ya mabwawa na umwagiliaji.
Kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa kila shule na boma
Gharama ya maisha
Tathmini gharama ya mafuta, unga na nishati katika siku 100.
Kuongeza uwezo wa kusambaza umeme na kupunguza upotevu wa gridi kutoka asilimia 23 hadi 10.
Weka mazingira wezeshi ya kupata chakula, mavazi, malazi na mahitaji mengine ya kimsingi kwa bei nafuu.
Roots Party of Kenya
Vipaumbele
Kuendesha serikali yenye faida kupitia kuhalalisha na kudhibiti utumiaji wa bangi kiviwanda
Kuunda majimbo 8 ambayo yatasimamiwa na serikali zao za shirikisho.
Sitisha katiba, ili kuwapa Wakenya fursa ya kuchagua sheria inayowafaa.
Uchumi
Uchumi wa saa 24 wa zamu ya saa nane, siku nne kwa wiki.
Kuongeza bajeti ya serikali kupitia mapato ya fedha za kigeni kutokana na mauzo ya katani ya viwandani.
Pata mapato kupitia ufugaji wa nyoka na kuuza nje nyama ya mbwa.
Ufisadi
Kuanzisha hukumu ya kifo inayotumika kwa watu wanaopatikana na hatia ya rushwa.
Kutovumilia rushwa.
Madeni
Lipa deni la Kenya haraka kwa mapato kutoka kwa kuhalalisha na usafirishaji wa bangi ya viwandani.
Mkopo huo utalipwa kwa awamu 30 kati ya Januari 2021 hadi Julai 2035.
Epuka madeni kwa kutumia mapato yaliyopatikana kutokana na kuhalalisha bangi ili kuongeza mapato ya serikali.
Ajira
Unda fursa za Uwekezaji na ajira kwa kuhalalisha bangi
Kawi
Tumia katani ya Viwanda kuzalisha nishati ya kibayolojia.
Kupunguza gharama ya nishati kwa kupunguza kodi na kushughulikia mzigo wa madeni.
Afya
Huduma za afya na lishe ya bure kwa wazee, walio katika mazingira magumu na wajawazito.
Boresha matibabu na udhibiti wa Alzheimer's, saratani, ugonjwa wa kupooza kwa ubongo na kifafa kwa kutumia moja ya bidhaa za katani za viwandani.
Kutanguliza utafiti na maendeleo katika kampuni za dawa zinazomilikiwa na Kenya.
Uhalifu na usalama
Kuwalipa polisi vizuri ili kupunguza rushwa.
Elimu
Wape wazazi chaguo la masomo ya nyumbani na kurahisisha mchakato wa usajili.
Boresha mfumo wa elimu wa CBC nchini Kenya.
Usambazaji wa maji
Kuboresha miundombinu ya majisafi na majitaka.
Gharama ya maisha
Tengeneza fursa za ajira na uwekezaji.
Punguza kodi na gharama ya nishati.
Chama cha Agano
Vipaumbele
Unda taasisi zitakazomaliza ubadhirifu wa fedha na kukomesha ufisadi.
Hakikisha kwamba haki za wasio na sauti na waliotengwa zinazingatiwa.
Punguzo la ushuru kwa Wakenya kusaidia kudhibiti gharama ya maisha.
Uchumi
Kupeleka bajeti kwa halmashauri za vijiji badala ya Hazina na Ikulu.
Weka mazingira mazuri kwa sekta binafsi na watu binafsi kuanzisha biashara.
Ufisadi
Fanya ripoti za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kuwa ushahidi wa msingi wa matumizi mabaya ya ofisi na msingi wa kuwashtaki watumishi wa umma walio wafisadi
Kesi zote za ufisadi zitashughulikiwa ndani ya miezi mitatu.
Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa kupewa mamlaka ya kuendesha mashtaka.
Madeni
Majadiliano kwa lengo la kupanga upya ulipaji wa deni na wakopeshaji.
Tumia fedha zilizopatikana kutokana na shughuli za kifisadi kulipa madeni ya nje.
Kurejesha fedha zilizofichwa nje ya nchi ili kusaidia kulipa deni la nje .
Ajira
Tekeleza sheria ya maudhui ya humu nchini kwa kuongeza kiwango cha juu cha kandarasi zinazotolewa kwa makampuni ya kigeni hadi zaidi ya $8.5 milioni (Ksh1 bilioni).
Punguzo la kodi kwa makampuni yanayoajiri wanawake na vijana.
Kuharakisha utekelezaji wa mpango wa Kanda Maalum ya Kiuchumi ili kuhimiza wageni,makampuni ya kuanzisha viwanda vya utengenezaji nchini Kenya.
Kawi
Kusaidia matumizi ya nishati ya jua nje ya gridi ya taifa.
Kufanya nishati kuwa bei nafuu kwa kushughulikia rushwa katika sekta ya nishati.
Afya
Unda tume ya kitaifa ya afya ili kudhibiti kupanda kwa gharama za afya.
Kutoa ruzuku kwa michango ya Mfuko wa Kitaifa wa Bima ya Afya kwa kila familia Kenya.
Uhalifu na usalama
Kuboresha maisha na mazingira ya kazi ya polisi.
Fanya vikosi vya usalama kuwa vya kisasa ili kuendana na uhalifu wa kisasa.
Punguza msongamano wa magereza na kuboresha hali ya maisha na kazi ya maafisa wa magereza
Elimu
Kuanzisha kipengele cha maadili katika mtaala.
Elimu ya bure katika ngazi zote.
Walimu wawezeshwe kidijitali kufanya kozi za kujiongeza masomo
Usambazaji wa maji
Maeneo kame kupokea maji ya bomba kwa ajili ya umwagiliaji.
Kuondoa tozo dhidi ya vifaa vyote vya kuvuna maji ya mvua.
Kukuza upandaji miti upya.
Gharama ya maisha
Msamaha wa jumla wa 50% kwa PAYE kwa Wakenya wote.
Kenya Kwanza Alliance
Vipaumbele
Tenga $427 milioni (Ksh50 bilioni) kila mwaka ili kutoa mikopo kwa biashara ndogo ndogo na za kadri kwa njia rahisi na inayotegemeka
Kurekebisha Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili kubadilisha mchango kwa familia/nyumba badala ya watu binafsi.
Mtandao wa bure ndani ya miaka mitano.
Uchumi
Komesha ushuru unaorudiwa
Fanya leseni ya biashara na eneo kuwa haki.
Weka sera thabiti ya ulinzi wa huduma za kifedha ili kuwalinda Wakenya dhidi ya wakopeshaji walaghai.
Ufisadi
Kuzipa uhuru taasisi zinazohusika na vita dhidi ya rushwa.
Taarifa za wafanyabiashara wanaofanya biashara na serikali kuwekwa wazi.
Shirikiana na nchi nyingine kusaidia kurejesha mali zilizoibiwa.
Madeni
Kuimarisha uwezo wa serikali wa kukopesheka kutoka nje na kuongeza upatikanaji wa mikopo nafuu, na kuacha vyanzo vya mikopo vya ndani kwa sekta binafsi.
Ajira
Wekeza kwenye kilimo ili kutengeneza ajira zaidi.
Anzisha Kituo cha Maendeleo ya Biashara cha MSME katika kila kata na bustani ya viwanda.
Kuanzisha kituo cha ukuzi wa biashara katika kila taasisi ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi.
Kawi
Weka mfumo wa kisheria wa kulinda hazina ya uimarishaji wa mafuta.
Unda vivutio vya kupitishwa kwa mifumo ya usafiri wa umma ya umeme katika miji na miji yote.
Kuharakisha maendeleo ya rasilimali ya kawi ya mvuke
Afya
Huduma ya afya ya msingi inayofadhiliwa kikamilifu.
Kuanzisha mfuko wa kitaifa wa magonjwa sugu.
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wa lazima.
Uhalifu na usalama
Imarisha uangalizi wa polisi na kuteua mchunguzi atakayezingatia ukiukwaji wa haki za binadamu kwa vijana.
Bima ya maisha kwa maafisa wa polisi iwapo watafariki wakiwa kazini.
Mfuko wa hisani wa kuchangia familia za maafisa walioaga dunia na wagonjwa mahututi.
Elimu
Lipia mafunzo ya ualimu kazini.
Tathmini mfumo wa sasa wa maendeleo ya kitaaluma kulingana na mitihani.
Kupunguza pengo la sasa la upungufu wa walimu 116,000 ndani ya miaka miwili ya kifedha.
Usambazaji wa maji
Maji yatapewa kipaumbele kwa ruzuku ya mradi/ufadhili wa masharti nafuu.
Hamisha mwelekeo kutoka kwa mabwawa makubwa hadi kwenye miradi ya maji ya kijamii huku msisitizo ukiwa katika kuvuna na kurejeleza
Gharama ya maisha
Kuongeza tija ya kilimo ili kupunguza gharama ya maisha.
Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.
End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?
Gladys Wanga
Wanga anaingia katika historia kama gavana mwanamke mwenye umri mdogo zaidi na gavana wa kwanza katika eneo la Nyanza.
Gladys Wanga amemuangusha mpinzani wake wa karibu aliyekuwa gavana wa Nairobi Dkt. Evans Kidero.
Alikuwa mwanamke wa kwanza mwenyekiti wa chama cha ODM katika eneo la Homa Bay na pia wa kwanza kuongoza Kamati ya Kitaifa ya Fedha na Mipango ya Kitaifa.
Akizungumza wakati wa kampeni zake, Wanga aliwaahidi wakazi wa Homa Bay atatumia rasilimali zilizogatuliwa kuboresha maisha ya wananchi na kuendeleza kaunti ya Homa bay.
"Kama kijana naamini nina nafasi ya kutengeneza urithi, sio ule ninaouacha bali ule ninaoishi, kwa maana ya kwamba ninapofanya vibaya naweza kuishi miaka mingi kuona ubaya, na ninapofanya kilicho sawa, ninaishi kuona mema ambayo nimefanya," alisema.
Alifichua kwamba alijihusisha na siasa akiwa na umri wa miaka mitano aliposaidia kusambaza 'chumvi' kwa wanakijiji wakati wa kampeni za uchaguzi za babake.
Wanga pia angeandamana na babake kwa shughuli za kisiasa na mikutano.
Kawira Mwangaza
Chanzo cha picha, Kawira Mwangaza/FACEBOOK
Maelezo ya picha, Kawira Mwangaza gavana mteule kaunti ya Meru
Mwakilishi wa wanawake wa Meru Kawira Mwangaza, ameshangaza wengi kwa kuwabwaga vigogo wa kisiasa Mithika Linturi na gavana anayeondoka Kiraitu Murungi kwenye kinyang'anyiro cha kumchagua gavana wa kaunti ya Meru.
Mwangaza, ambaye alishindana kama mgombea huru amefanikiwa kuibuka na ushindi baada ya kutawala siasa za humu nchini kwa miaka mingi.
Bi Mwangaza, aliyekuwa mbunge kwa mara ya kwanza, alitangaza nia ya kumwondoa madaraka gavana wa Meru, Kiraitu Murungi mwaka wa 2019.
Mwakilishi huyo wa kike, ambaye pia ni mwanzilishi na askofu wa Kanisa la Baite Family Fellowship, alimteua Isaac Mutuma, kasisi wa Kanisa hilo kama mgombea mwenza wake.
"Nimemtambua Isaac Mutuma kama mgombea mwenza wangu katika kinyang'anyiro cha Agosti. Hii ni timu ya watu wenye ujuzi wa hali ya juu na watumishi wa watu. Siwezi kuteua bila maombi," alisema.
Katika ulingo wa kisiasa, Bi Mwangaza ameonyesha umahiri wake katika ujuzi alionao wa kuhamasisha watu mashinani.
Bi Mwangaza ameahidi kuwapa wakazi wa Meru uongozi bora kupitia matumizi ya busara ya pesa za umma.
Pia ameshinda uungwaji mkono wa kasisi Kiambi Atheru, ambaye alikuwa amepanga kuwania ugavana kwa mara ya pili mwaka huu, baada ya kushindwa mwaka wa 2017.
Wavinya Ndeti
Chanzo cha picha, @WAVINYA_NDETI
Wavinya Ndeti alijiunga na siasa mwaka wa 2007 akigombea na kuchaguliwa kuwa mbunge wa eneo bunge la Kathiani chini ya Chama Cha Uzalendo (CCU).
Katika kushinda kiti hicho, Ndeti alikuwa mwanamke pekee aliyewakilisha eneo bunge hilo tangu uhuru.
Ndeti aliteuliwa katika serikali kuu ya muungano kama Waziri Msaidizi wa Vijana na Michezo chini ya Helen Sambili.
Ndeti, ni mmoja wa wanachama waanzilishi wa Muungano wa Mageuzi na Demokrasia - CORD, ulikuwa muungano wa vyama vingi vya kisiasa vilivyojengwa kwa karibu na Raila Odinga, Kalonzo Musyoka, na Moses Wetangula, kuwania uchaguzi mkuu wa Kenya wa 2013.
Ndeti, aliwania kiti cha Gavana wa Machakos kwa tiketi ya CCU mwaka wa 2013. Alimchagua aliyekuwa waziri wa Maji na Maliasili Mutua Katuku kama mgombea mwenza wake.
Katika uchaguzi wa mwaka huu uliofanyika Agosti 9, Wavinya ndeti amejitosa kwenye kusaka kiti cha ugavana kupitia chama cha Wiper na Gavana wa Machakos anayeondoka Alfred Mutua wa chama cha Maendeleo Chap Chap, alimuunga mkono kwenye ugombea wake.
"Ninakubali kwa ukarimu kuidhinishwa na gavana anayeondoka Dkt. Alfred Mutua na ninathamini kujitolea kwake kwa umma kunipigia kura. Ni faida kubwa kwetu na inatusaidia sana kuonyesha imani kuwa timu yetu pekee ndiyo inayohitaji kuongoza Kaunti," alisema alipoidhinishwa.
Wavinya ndiye ndiye mzaliwa wa mwisho kati ya watoto 10 wa Ndeti, lakini kati ya hao wote, ni yeye tu na marehemu kaka yake, Ignatius Dick Ndeti walioingia kwenye siasa. Dick Ndeti alikuwa diwani wa Athi River baada ya babake.
Susan Kihika amwangusha kigogo Lee Kinyanjui
Chanzo cha picha, Kenya Parliament
Maelezo ya picha, Susan Kihika
Seneta wa Nakuru Susan Kihika wa chama cha United Democratic Alliance (UDA) amemwangusha kigogo Lee Kinyanjui wa chama cha Jubilee katika kinyang'anyiro cha ugavana kaunti ya Nakuru.
Susan Wakarura Kihika alichaguliwa katika bunge la seneti mwaka wa 2017.
Katika uchaguzi wake, aliteuliwa kuwa kinara wa wengi wa chama cha Jubilee.
Alishikilia wadhifa huo hadi tarehe 11 Mei 2020 ambapo nafasi yake ilichukuliwa na Seneta Irungu Kangata.
Ni mmoja wa viongozi waliojiondoa katika chama cha Jubilee pamoja na naibu rais baada ya makubaliano ya maridhiano kati ya Rais Uhuru na kiongozi wa ODM Raila Odinga.