Uchaguzi Kenya 2022: Mfahamu Ida Odinga, Mke Raila Amollo Odinga

Ida odinga

Chanzo cha picha, Ida Odinga/ twitter

    • Author, Dinah Gahamanyi
    • Nafasi, BBC Swahili
  • Muda wa kusoma: Dakika 6

Wakenya leo wameamkia mitandaoni kumtakila kila la heri Bi Ida Odinga, mke wa kiongozi wa muda mrefu wa upinzani nchini humo Raila Amollo Odinga katika siku yake ya kuzaliwa. Sherehe ya mwaka huu ya kuzaliwa ya Ida Odinga inafanyika huku mume wake Raila Odinga akiwa tayari amewasilisha pingamizi lake mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais wa tarehe 9 Agosti, yaliyomnyima ushindi na mpinzani wake William Ruto kutangazwa mshindi.

Bw Odinga kupitia ujumbe wake wa Twitter amemtakia Bi Oda siku njema ya kuzawaliwa, ujumbe uliojibiwa na wimbi la jumbe za wakenya za kumtakia heri njema ya siku ya kuzaliwa.

Katika ujumbe wake wa Twitter ulioambatanishwa na picha Bw Odinga ameandika:''Katika kila siku yako ya kumbukumbu ya kuzaliwa kama leo, ninatafakari ni kwa jinsi gani wewe ni kitu bora zadi kilichotokea maishani mwangu. Uwezo wako, uvumilivu, busara, na sala ambavyo vimeweza kuifikisha familia hapa ilipo . Heri ya siku ya kuzaliwa mpendwa wangu Ida Betty''

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Lakini je Bi Ida Odinga ni nani hasa?

Kama umewahi kusikia '' kila nyuma ya mwanaume mwenye mafanikio nyuma kuna mwanamke '', basi msemo huu huenda kuhusishwa na Ida Odinga, mke wa mwanasiasa mkongwe wa Kenya Raila Amollo Odinga. Hii ni kutokana na mchango wake binafsi katika maisha ya kibinafsi na ya kisiasa ya Bw Odinga. Hatahivyo Bi Ida binafsi ameshiriki pakubwa katika maendeleo ya kijamii hususan katika jamii. Lakini je Bi Ida Odinga ni nani hasa?

ida Odinga

Chanzo cha picha, Ida odinga/Twitter

Maelezo ya picha, Ida Odinga

Kabla ya kuwa mke wa Odinga

Akifahamika kwa jina la kuzaliwa kama Ida Anyango Oyoo alizaliwa tarehe 27 Agosti, 1950, katika kaunti ya Migori Magharibi mwa Kenya. Alisomea masomo yake ya shule ya sekondari ya wasichana ya Ogande (Girls High School). Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Nairobi ambapo alitunukiwa shahada ya Elimu, mwaka 1974, akiwa na umri wa miaka 24. Ida alilelewa katika familia ya watoto sita. Baba yake alikuwa daktari huku mama yake akiwa muunguzi. Ida Odinga alifiwa na baba yake mzazi akiwa na umri wa miaka saba.''Tulipofiwa na baba yetu, maisha yalibadilika hayakuwa rahisi, lakini mama yetu alichukua jukumu na akatulea vyema kutujenga kuwa watu tulio sasa'' , alisema Bi Ida.

Alivyokutanana na kuoana na Bw Raila Amollo Odinga

ida Odinga

Chanzo cha picha, Ida Odinga/Twitter

Ida alikutana kwa mara ya kwanza na mume wake Raila Amollo Odinga alipokuwa akisoma katika Chuo Kikuu cha Nairobi. Aliwahi kukiri awali kwamba hakufikiria kuwa wakati mmoja angeolewa na mwanasiasa au mtu yeyote anayejihusisha na siasa. Hatahivyo alipoolewa na Bw Raila alifahamu fika kuwa anaolewa na Mhandisi kwani Odinga alikuwa akisomea uhandisi.

Ndoa na watoto

Ida aliolewa na Bw Raila Amollo Odinga tarehe 1 Septemba 1973 na, katika ndoa yao walijaaliwa watoto wanne, Fidel Odinga , Winnie Odinga, Raila Odinga Jr na Rosemary Odinga. Hata hivyo mtoto wao wa kwanza Fidel Odinga alifariki dunia mwaka 2015.

Kwa Wakenya wengi Bi Ida Odinga, anaonekana kama mwanamke shupavu, na mwenye msimamo, aliyeweza kusimama na mume wake na familia yake katika nyakati ngumu, na hivyo kuwa na sifa ya kuitwa 'mama Ida'. Sifa hii inatokana na kwamba kwamba, Bi Ida alilazimika kuwalea watoto wanne peke yake wakati mume wake alipofungwa na serikali ya zamani ya Rais Moi mwaka 1982.

Familia ya Odinga

Chanzo cha picha, Raila odinga/Twitter

Maelezo ya picha, Familia ya Ida Odinga na Raila Odinga, kutoka (kushoto), Marehemu Fidel Odinga na mke wake, Winnie Odinga, Raila Odinga Jnr na mke wake na Rosemary Odinga. Katikati ya Ida Odinga na Raila Odinga ni mjukuu

Ida Odinga kama mke wa Raila Amollo Odinga

Akifahamika na wengi nchini Kenya kama 'Mama' Ida Odinga, ni mwanamke ambaye kila mara amekuwa akionekana hadharani akiambatana na mume wake na kuonyesha uungaji mkono wa hali ya juu kwa mume wake Raila Odinga hususan katika mikutano ya kisiasa, kila mara mume wake anapowania urais wa Kenya.

Mara kwa mara husikika kwenye majukwaa ya kisiasa na kampeni akimpigigia debe Raila kuwa yeye ndiye anayefaa kuwa Rais wa Kenya.''Ninaufahamu upendo alionao Raila kwa nchi hii'', alisika wakati mmoja akisema Bi Ida katika kampeni za hivi karibuni.

Japo kitaaluma Mama Odinga ni mfanyabiashara, mwanaharakati na Mwalimu, lakini umaarufu wake zaidi umetokana na jinsi anavyosimama kidete katika harakati za kumuunga mkono Bwana Raila Amollo Odinga katika siasa na azma yake ya kuongoza taifa la Kenya. Hii imekuwa ikidhihirika katika mikutano ya kisiasa ambapo huambatana na mumewe na kuwarai wapiga kura wamchague mumewe kama Rais wa Kenya.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

' Si mke, mama,wala mwanasiasa tu'

Bi Odinga sio mke wa mwanasiasa tu. Binafsi ameonyesha kuwa mwanamke mwenye ushawishi hususan kwa wanawake wenzake na bado ni mhimili imara katika jamii, akiwa mstari wa mbele kutetea nafasi ya wanawake katika maendeleo ya jamii.

Bi Odinga alianzisha vuguvugu lililowahamasisha wanawake kuwachagua wanawake wenzao katika mwaka 1991, na kufahamika kama sura ya ukaidi katika utawala wa chama kimoja nchini Kenya. Pia ni mmoja wa wanawake wa kwanza kuongoza kampuni kubwa ya biashara ya usambazaji wa gesi nchini Kenya.

Bi Ida Odinga ambaye ni mwalimu kitaaluma anaamini mwanamke anapaswa kuelimika: "Ni vizuri kuwa mke mwema, lakini ni vyema kuwa mwanamke aliyeelimika. Kuwa mwanamke sio nafasi tu kuwa katika fursa ya utiifu---ni nafasi ya nguvu ," "Na ninamfanya yeye [Raila Odinga] imara kwa kuwa imara ."aliiambia BBC ilipomtembelea nyumbani kwake kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2017, wakati Bw Odinga alikuwa mgombea wa

Mwaka 2010, katika taarifa iliyochapishwa katika gazeti la The Standard ilimtaja miongoni mwa wanawake maarufu zaidi nchini Kenya.

ida Odinga

Chanzo cha picha, Ida odinga/Twitter

Kwa miaka mingi, amekuwa akijihusisha katika miradi mingi sana, ikiwemo miradi ya kampeni ya uelewa kuhusu saratani ya matiti na fistula. Hali kadhalika amekuwa mshauri wa wanafunzi kadhaa wa kike na pia mdhamini mkubwa katika kujenga maktaba ya kisasa katika shule yake ya zamani ya sekondari. Bi Ida Odinga aliweza kuchangisha shilingi milioni 176.9 kwa ajili ya ujenzi wa maktaba ya wanafunzi 500.

Mwaka 2021, alipewa tuzo ya kutambua uungaji mkono wake mkubwa katika masuala ya afya, elimu, wanawake, amani, pamoja na uwezeshwaji wa watoto wavulana na wasichana. Tuzo hiyo iliandaliwa na taasisi ya Hekima Kaka.

'Haiba na muonekano'

ida Odinga

Chanzo cha picha, Ida Odinga Twitter

Si ajabu Bi Ida Odinga akaitwa mama kutokana na haiba na muonekano wake hasa anapokuwa hadharani. Kauli zake mara kwa mara zimekuwa zenye mvuto kutokana na uwezo alionao wa kuifanya hadhila yake iamini kile anachokisema sawa na mama anapokuwa nyumbani.

''Ni mama mchangamfu sana unapokutana naye kwa mara ya kwanza utadhani mnafahamiana'', aliiambia makala hii Bi Atieno Omondi, mkazi wa Migori.

Kutokana na ukweli kwamba ameweza kusimama kidete na mume wake Raila Odinga, hasa katika nyakati ngumu za misukosuko ya kisiasa, na kuweza kuitunza familia yake wakati mumewe Odinga alipofungwa miaka mitano na utawala wa rais wa zamani Daniel Arap Moi, baadhi ya Wakenya wanamuona kama mama mwenye msimamo, na anayefaa kuitwa Mama.

''Kusema kweli Mama Ida ana haiba yenye mvuto na akisimama kuongea lazima utamsikiliza…sauti yake kuna vile inavutia kumsikiliza, ni mama mwenye heshima zake'', aliiambia BBC Juliet Mwendwa mkazi wa Nairobi.

'Ni rahisi kubainika ndani ya umati wa watu'

Iwapo umekua ukifuatilia mavazi ya Bi Ida, huenda ukakubalia nami kwamba , Bi Ida Odinga ni mwanamke ambaye bila shaka hutatatizika kumuona na kumbaini kwenye umati wa watu, kutokana na kimo chake pamoja na mavazi nadhifu anayoyavaa yenye rangi unazoweza kuziona hata anapokuwa miongoni mwa umati wa watu.

Mtindo wake wa mavazi ni wa stara, kuanzia mavazi ya Kiafrika ya batiki hadi vitenge hususan pale anapoonekana mbele ya umma kwenye mikutano ya hadhara ya kiasa ambapo mara nyingi huambarana na mumewe Raila Amollo Odinga.

Ni mwanamke anayejali mavazi anayovaa, kutokana na ukweli kwamba kila mara anapojitokeza hadharani huonekana mwanamke nadhifu.

Ida Odinga

Chanzo cha picha, Ida Odinga/Twitter

Maelezo ya picha, katika matuko ya umma hususan katika mikutano ya kampeni Bi Ida odinga hupendelea kuvaa zaidi mavazi ya stara yyenye rangi za kuvutia
ida Odinga

Chanzo cha picha, Ida Odinga/Twitter

Maelezo ya picha, Sio rahisi kutomtambua Mama Ida Odinga miongoni mwa umati wa watu, kutokana na kimo na mtindo wake wa mavazi
Ida Odinga

Chanzo cha picha, Ida dinga/Twitter

Mbali na mikutano ya kisiasa, akiwa katika shughuli za kawaida katika ofisi yake, Bi Ida huvaa mavazi mbali mbali, kama vile, suti za sketi na koti na mavazi mengine yasiyo rasmi awapo nyumbani kwake.

Akizungumza na BBC Bi Ida Odinga, awali alisema kuwa iwapo mume wake atachaguliwa na hivyo kuwa Mke Rais atahakikisha kuwa watoto wa kike wanapata elimu na maisha bora, na kuhakikisha afya ya wanawake na Wakenya kwa ujumla inazingatiwa.

Uchaguzi Kenya 2022:Unaweza pia kusoma

Elex