Uchaguzi Kenya 2022: Fahamu makosa ambayo hustahili kufanya wakati wa kupiga kura

Masanduku ya kupigia kura

Chanzo cha picha, AFP

    • Author, Asha Juma
    • Nafasi, BBC Swahili

Siku ya Jumanne, Agosti 9, 2022 Wakenya zaidi ya milioni ishirini watapiga kura wakiwa wanatimiza haki yao ya kikatiba nchini Kenya, kwa kushiriki kwenye uchaguzi mkuu.

Hili ni zoezi ambalo hufanyika Jumanne ya pili ya mwezi Agosti kila baada ya miaka mitano.

Hiki ni kinyang'anyiro ambacho kinahusisha kuchaguliwa kwa rais, gavana, wabunge,wawakilishi wa wanawake na wawakilishi wa wadi.

Lakini je, kama mpiga kura, unafahamu ni kitu gani ambacho hustahili kukifanya utakapokuwa kwenye kituo cha kupiga kura?

  • Ni hatia kutumia utambulisho wa kupiga kura ambao si wako yaani kadi ya kupiga kura au kitambulisho kisicho chako.
  • Hustahili kwenda kwenye kituo cha kupiga kura ukiwa umevalia sare zinazoashiria mrengo fulani.
  • Ni makosa kuanza kushawishi watu waliopanga foleni kwa nia ya kuwataka kumpigia kura mgombea fulani.
  • Ni hatia kuanza kuhonga wapiga kura kwa ajili ya kuwataka kumchagua mgombea.
  • Pia ni hatia kuanza kupiga picha ovyo wakati zoezi la kupiga kura linaendelea.
  • Ni hatia kuanza kuchana au kuharibu karatasi ya kupiga kura hovyo bila kuruhusiwa kufanya hivyo.
  • Hairuhusiwi kuanza kupiga muhuri au kuweka alama yoyote kwenye karatasi ya kupiga kura.
  • Karatasi za kupiga kura hazistahili kuuzwa kwa yeyote.
  • Pia huruhusiwi kuanza kupeana karatasi ya kupiga kura kwa yeyote tu unayemuona bila kupewa ruhusa.

Kama mpiga kura ukishapewa karatasi ya kupiga kura unafaa kufanya uamuzi wako mwenyewe wala sio kuanza kuuliza wengine wanayempigia au nani utakayempigia kura.

Ukimaliza kupiga kura, karatasi za kupiga kura kila mmoja inastahili kuwekwa kwenye sanduku husika wala sio kuweka popote tu unapojisikia.

  • Hairuhusiwi kuweka kitu kingine chochote kwenye masanduku ya kupiga kura zaidi ya karatasi ya kupiga kura.
  • Ni makosa kuondoka na karatasi ya kupiga kura kutoka kwenye kituo cha kupiga kura.
  • Pia usiharibu chochote ambacho kinaweza kutatiza shughuli ya upigaji kura.
  • Ni makosa makubwa kupiga kura zaidi ya mara moja.
  • Ni hatia kupatikana na karatasi ya kupiga kura ukiwa nje ya eneo la kupiga kura.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Wewe ikiwa sio afisa wa Tume huru, bila ruhusa yoyote kutoka kwa afisa husika, haustahili kuondoa chochote cha kupiga kura kabla, wakati au baada ya kupiga kura.

Bila ruhusa, kuchapisha karatasi yoyote ya kupiga kura, au kile kinachoonekana kuwa karatasi hiyo au kile kinachoweza kutumika kama karatasi ya kupiga kura kunaweza kukuweka hatiani.

Sio ruhusa kuanza kusumbua wengine kwa namna yoyote ile wakati wanapiga kura. Na iwapo utakuwa unahitaji usaidizi wowote, kutakuwa na maafisa wa tume ya IEBC watakaokuwepo kujibu swali lako.

Kwa madhumuni ya uchaguzi, ni hatia kutengeneza, kuagiza, kumiliki, vifaa au matumizi yanayoweza kutumika katika utaratibu ambao karatasi ya kupigia kura inaweza kutolewa, kuathiriwa au kufanyiwa ulaghai baada ya kuwekwa kwenye sanduku la kura wakati wa upigaji kura katika uchaguzi wowote.

Kuweka alama yoyote kwenye karatasi yoyote ya kupigia kura kwa mtu yeyote isipokuwa yeye mwenyewe.

Kupiga kura katika uchaguzi wowote wakati huna haki ya kupiga kura.

kujifanya kuwa hajui kusoma au kuandika ili kusaidiwa katika kupiga kura.

Kujifanya kuwa na ulemavu wa macho au ulemavu mwingine wowote ili kusaidiwa katika kupiga kura.

Ukimaliza kupiga kupiga kura, unachotakiwa kufanyani kuondoka kituoni kwa utulivu na kwenda nyumbani kwako kusubiri matokeo.

Kufanya makosa na kupatikana na hatia utawajibika kulipa faini isiyozidi shilingi milioni moja au kifungo kisichozidi miaka sita au vyote kwa pamoja.

Zoezi hili la kupiga kura litafanyika katika vituo 46,229 vilivyotambuliwa rasmi kama vya kupigia kura na Tume huru ya uchaguzi na mipaka (IEBC) na watakaochaguliwa wakiwa ni pamoja na wafungwa na raia wa Kenya wanaoishi kwenye nchi za nje katika balozi za Kenya.

Wafula Chebukati
Maelezo ya picha, Mwenyekiti wa Tume ya IEBC Wafula Chebukati

Makosa ya wajumbe na wafanyakazi wa Tume

Mjumbe wa Tume, mfanyakazi au mtu mwingine mwenye jukumu la kutekeleza kwa mujibu wa sheria yoyote inayohusiana na uchaguzi ni pamoja na:

Kuweka kumbukumbu ya hati yoyote ambayo unajua au una sababu nzuri ya kuamini kuwa ni uwongo, au haamini kuwa ni kweli.

Kumruhusu mtu yeyote ambaye utamfahamu au kuwa na sababu za msingi za kuamini kuwa anaweza kusoma au kuandika kupiga kura kwa namna iliyotolewa kwa watu wasiojua kusoma na kuandika.

Kumruhusu mtu yeyote ambaye unafahamu au kuwa na sababu za msingi za kuamini kuwa si mwenye ulemavu wa macho au mtu mwenye ulemavu kupiga kura kwa njia iliyoelezwa kwa watu wenye ulemavu wa macho au watu wenye ulemavu wowote ule.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Kwa makusudi kumzuia mtu yeyote kupiga kura kituoni.

Kwa makusudi kukataa kuhesabu karatasi yoyote ya kupigia kura.

Kwa makusudi kutaa kuhesabu karatasi yoyote iliyopigiwa mgombea

Kuingilia mpiga kura katika upigaji kura wake kwa siri.

Utakapohitajika chini ya Sheria ya Uchaguzi (Na. 24 ya 2011) au sheria nyingine yoyote kutangaza matokeo ya uchaguzi, na kushindwa kutangaza matokeo ya uchaguzi.

Isipokuwa kwa mwanachama, afisa au mtu aliyeidhinishwa kufanya hivyo, ni makosa kutoa tamko au tangazo rasmi la matokeo ya uchaguzi.

Bila sababu za msingi kufanya jambo lolote katika misingi ya kukiuka wajibu rasmi.

Kushirikiana na chama chochote cha siasa au mgombea kwa madhumuni ya kufaidi isivyostahili chama cha siasa au mgombea

Kukiuka sheria kwa makusudi ili kutoa faida isivyostahili kwa mgombea au chama cha siasa kwa upendeleo, kikabila, kidini, jinsia au masuala yoyote kinyume cha sheria.

Kushindwa kuzuia au kutoa taarifa kwa Tume au mamlaka nyingine yoyote husika, kutendeka kwa kosa la uchaguzi lililofanywa chini ya Sheria hii.

Kutenda kosa na kupatikana na hatia, utawajibika kulipa faini isiyozidi shilingi milioni moja au kifungo kisichozidi miaka mitatu au vyote kwa pamoja.

th

Pia unawezakusoma:

th