Uchaguzi Kenya 2022: VPN ni nini, na unahitaji kuitumia katika mazingira gani?

VPN

Chanzo cha picha, Getty Images

    • Author, Lizzy Masinga
    • Nafasi, BBC Swahili

Mtandao pepe binafsi (au VPN) ni muunganisho salama kati ya kifaa chako na kompyuta nyingine kwenye mtandao.

Huduma za VPN ni muhimu kwa kufikia mifumo ya kompyuta yako ya kazini kwa usalama ukiwa mbali na ofisi. Lakini pia hutumiwa kwa kawaida kukwepa udhibiti wa serikali, au kuzuia kutambulika eneo mlengwa alipo na kuzuia kwenye tovuti za kupakulia filamu filamu.

Kwa mujibu wa mtandao wa teknolojia wa kaspersky, VPN hutoa fursa ya kuanzisha muunganisho wa mtandao unaolindwa unapotumia mitandao ya Umma.

VPN huwezesha kutumia mtandao kwa njia fiche na kuficha utambulisho wako mtandaoni. Hii inafanya iwe vigumu zaidi kwa washirika wengine kufuatilia shughuli zako mtandaoni na kuiba data.

Kwanini unahitaji kutumia huduma ya VPN?

Kurambaza kwenye wavuti au kufanya miamala kwenye mtandao wa Wi-Fi usio salama kunamaanisha kuwa unaweza kuwa unafichua maelezo yako ya faragha na tabia za kuvinjari.

Ndiyo maana VPN inapaswa kuwa ya lazima kwa mtu yeyote anayejali kuhusu usalama wao mtandaoni na faragha.

VPN huzingatia usalama wa mtumiaji

Chanzo cha picha, Getty Images

Je, umewahi kuingia katika akaunti yako ya benki mtandaoni kwenye ukumbi ukiwa kwenye hoteli kwa mfano ? Au labda umelipa bili ya kadi yako ya mkopo mtandaoni. Ikiwa umefanya hivi bila kuingia kwenye VPN kwanza, unaweza kuwa umefichua maelezo yako ya faragha na tabia za kurambaza kwa wadukuzi na wahalifu wa mtandaoni.

Isipokuwa tu kama umeingia katika mtandao wa faragha wa Wi-Fi ambao unahitaji nenosiri, vinginevyo data yoyote inayotumwa wakati wa vipindi vyako mtandaoni inaweza kuwa katika hatari ya kuchukuliwa na watu usiowajua wanaotumia mtandao sawa.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

VPN huficha nini?

Kwa mujibu wa mtandao wa programu ya norton ya kupambana na virusi kuhakikisha usalama wa kompyuta,VPN inaweza kuficha habari nyingi ambazo zinaweza kuweka faragha yako hatarini. Mtandao huu umeeleza mambo matano VPN ina uwezo wa kuficha.

th

1.Historia yako ya kurambaza mtandaoni

Sio siri unapoenda kwenye mtandao. Mtoa huduma wako wa mtandao na anaweza kufuatilia karibu kila kitu unachofanya kwenye mtandao.

Tovuti nyingi unazotembelea pia zinaweza kuweka historia. Vivinjari vya wavuti vinaweza kufuatilia historia yako ya utafutaji na kuunganisha maelezo hayo na anuani yako ya IP.

Hapa kuna mifano miwili kwa nini unaweza kutaka kuweka historia yako ya kuvinjari kuwa ya faragha. Labda unaugua unatafuta mtandao kwa maelezo kuhusu matibabu. Bila VPN, unaweza kuwa umeweka wazi maelezo hayo kiotomatiki na unaweza kuanza kupokea matangazo yanayolenga ugonjwa ulio nao ambayo yanaweza kuvutia umakini zaidi.

2.Utambulisho wako na mahali ulipo

Mtu yeyote anayenasa anuani yako ya IP (utambulisho wa kifaa chako) anaweza kufikia kile ambacho umekuwa ukitafuta kwenye mtandao na mahali ulipopatikana ulipotafuta.

Umelindwa dhidi ya historia yako ya utafutaji kukusanywa, kutazamwa au kuuzwa

Chanzo cha picha, Getty Images

Fikiria anwani yako ya IP kama anuani ya kurejesha ambayo ungeweka kwenye barua. Inakuongoza kwenye kifaa chako. Kwa kuwa VPN hutumia anuani ya IP ambayo si yako mwenyewe, hukuruhusu kudumisha faragha yako ya mtandaoni na kutafuta mtandao bila kukutambulisha.

Pia umelindwa dhidi ya historia yako ya utafutaji kukusanywa, kutazamwa au kuuzwa. Kumbuka, historia yako ya utafutaji bado inaweza kutazamwa ikiwa unatumia kompyuta ya umma au iliyotolewa na mwajiri wako, shule au shirika jingine.

3.Eneo ulipo wakati wa kurambaza

Unaweza kulipia huduma za utiririshaji zinazokuwezesha kutazama mambo kama vile michezo ya kitaaluma.

Unaposafiri nje ya nchi, huduma huenda isipatikane. Kuna sababu nzuri za hili, ikiwa ni pamoja na masharti ya mikataba na kanuni katika nchi nyingine.

Hata hivyo, VPN itakuruhusu kuchagua anuani ya IP katika nchi yako.

Hiyo inaweza kukupa ufikiaji wa tukio lolote linalooneshwa kwenye huduma yako ya utiririshaji.

4.Kifaa chako

VPN inaweza kusaidia kulinda vifaa vyako, ikiwa ni pamoja na kompyuta ya mezani, kompyuta ya mkononi na simu dhidi ya kuchunguzwa.

Vifaa vyako vinaweza kuwa walengwa wakuu wa wahalifu wa mtandao unapofikia intaneti, hasa ikiwa uko kwenye mtandao wa umma wa Wi-Fi.

Kwa kifupi, VPN husaidia kulinda data unayotuma na kupokea kwenye vifaa vyako ili wavamizi wasiweze kutazama kila hatua yako.

5. Shughuli zako za mtandaoni - kudumisha uhuru wa mtandao

Kumbuka, VPN hulinda dhidi ya mtoa huduma wako wa mtandao kuona historia yako na kutazama namna unavyovinjari. Kwa hivyo umelindwa ikiwa wakala wa serikali atamtaka mtoa huduma wako wa mtandao kusambaza rekodi za shughuli zako za mtandaoni.

Ikizingatiwa kuwa mtoa huduma wako wa VPN hajaandika historia yako ya kuvinjari (baadhi ya watoa huduma za VPN huweka), VPN yako inaweza kusaidia kulinda uhuru wako wa mtandao.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

VPN na matumizi ya sasa

Kwa mujibu wa GlobalWebIndex , idadi ya watumiaji wa VPN duniani kote iliongezeka zaidi ya mara nne kati ya mwaka 2016 na 2018.

Katika nchi kama vile Thailand, Indonesia na China, ambapo matumizi ya intaneti yalizuiwa na kuchunguzwa, mtumiaji mmoja kati ya watano wa mtandao hutumia VPN.

Nchini Marekani, Uingereza na Ujerumani, idadi ya watumiaji wa VPN iko chini karibu 5%, lakini inakua. Mojawapo ya vichocheo vikubwa vya utumiaji wa VPN katika miaka ya hivi karibuni limekuwa hitaji linaloongezeka la yaliyomo na vizuizi vya ufikiaji wa kijiografia.

Kwa mfano, huduma za kutiririsha video kama vile Netflix au YouTube hufanya video fulani kupatikana katika nchi fulani pekee. Ukiwa na VPN za kisasa, unaweza kutumia anuani yako kwa njia iliyojificha ili uonekane kuwa unavinjari kutoka nchi nyingine, kukuwezesha kufikia maudhui uyatakayo ukiwa popote.

Je, VPN ni salama?

Ni muhimu kutambua kwamba VPN hazifanyi kazi kama programu ya kina ya kupambana na virusi.

Ingawa zinalinda IP yako (utambulisho wako) na kuficha historia yako ya kurambaza, muunganisho wa VPN haulindi kompyuta yako dhidi ya kuingiliwa.

Ili kufanya hivyo, hakika unapaswa kutumia programu ya kuzuia virusi. Kwa sababu kutumia VPN peke yake hakukulindi dhidi ya Trojans, virusi, roboti au programu hasidi nyingine.

Mara tu programu ya kuharibu inapoingia kwenye kifaa chako, inaweza kuiba au kuharibu data yako, iwe unatumia VPN au la.

Kwa hiyo ni muhimu kwamba utumie VPN pamoja na programu ya kina ya kupambana na virusi ili kuhakikisha usalama wa juu wa kifaa chako.

VPN ni salama tu kama sera za matumizi na uhifadhi wa data za mtoaji wake. Kumbuka kwamba huduma ya VPN huhamisha data yako kwa seva zao na seva hizi huunganishwa kwenye mtandao kwa niaba yako.

Ikiwa watahifadhi kumbukumbu za data, hakikisha kwamba iko wazi ni kwa madhumuni gani kumbukumbu hizi zimehifadhiwa.

Watoa huduma wakubwa wa VPN kawaida huweka faragha yako kwanza kabisa. Kwa hivyo unapaswa kuchagua mtoa huduma unayemwamini.

th

Pia unawezakusoma:

th