Uchaguzi wa Kenya 2022: Kusafisha vyoo na kukata mboga kulivyowafurahisha wapiga kura

Nairobi gubernatorial candidate Polycarp Igathe cleaning public toilets

Chanzo cha picha, POLYCARP IGATHE

    • Author, Na Evelyne Musambi
    • Nafasi, BBC News, Nairobi

Baadhi ya wanasiasa wameachana na maisha ya starehe wakiwa katika kampeni na kugeukia kusafisha vyoo, kukata mboga na kupika chai katika juhudi za kuwashawishi wapiga kura kuelekea uchaguzi mkuu wa Agosti 9.

Mmoja wa wanasiasa aliyewafurahisha zaidi Wakenya zaidi ni Polycarp Igathe, ambaye alivalia ovaroli, buti na glavu mpya kabla ya kuchukua ndoo ya maji na kuanza kusafisha vyo katika mji mkuu, Nairobi

Alitumia chini ya sekunde 20 kupiga deki choo kimoja huku wasafishaji wakiangalia kwa mshangao.

"Kwa muda mrefu imeonekana kama kazi chafu lakini hii ni kazi ya kuwajibika," alisema Bw Igathe.

Wasafishaji vyoo katika jiji la Nairobi wanatumia deki ya kuku kuu na ndoo kusafisha maeneo hayo ambayo wakati mwingi hutoa harufu mbaya

Bw Igathe - ambaye anagombea kiti cha ugavana wa Nairobi - pia amepigwa picha akiosha magari na kupeana vinywaji katika vilabu vya burudani nyakati za usiku.

Mbinu yake hiyo imekejeliwa na baadhi ya watu wakisema anafaa kuja kutunza watoto na kuwafanyia kazi za nyumbani

Bw Igathe alikuwa naibu gavana chibi ya Mike Sonko, lakini alijiuzulu chini ya mwaka mmoja baada ya kuchukua wadhifa huo akisema ameshindwa kupata ridhaa ya gavana ya kufanya na kazi.

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema hatua hizi ni mbinu ya kujenga uhusiano mwema kwa umma na wapiga kura wanazijua sana na haziwezekani kuwashawishi kupiga kura.

Bw Igathe ni mpinzani mkuu wa Seneta wa Nairobi Johnson Sakaja. Yeye pia hajaachwa nyuma amekuwa akitumia mbinu kama hizi kuwashawishi wapiga kura, amekuwa akishirikisha mitandaoni picha inayomuonesha akinunua samaki kando ya barabara, tomato na vitunguu sokoni badala ya kwenye maduka makubwa ya kuuza bidhaa kwa jumla.

Nairobi gubernatorial candidate Johnson Sakaja buys onions from a vendor

Chanzo cha picha, JOHNSON SAKAJA

Bw Sakaja amekuwa Seneta wa Nairobi tangu 2017 na hili ni jaribio lake la kwanza kuwania ugavana.

Mkazi wa Nairobi Anne Wambui alidakia kwamba wanasiasa hawajui masoko yanapatikana hadi kampeni zianze.

"Tunatatizika kuishi katika jiji hili lakini mtu anayenunua bidhaa katika maeneo ya bei ghali anakuja kujifanya anatuelewa anapotaka kura yetu," aliambia BBC.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Mbunge wa Kimilili Didmus Barasa amekuwa akijaribu kuwavutia wapiga kura kwa kupanda teksi za pikipiki, na kuacha gari lake la kifahari.

Pia alipanda toroli ambalo liliwekwa juu ya gari lake. Toroli ni alama ya chama chake na imekuwa ikitumiwa kuwavutia Wakenya vijana wachangamfu.

MP Didmus Barasa in a wheelbarrow

Chanzo cha picha, DIDMUS BARASA

Bw Barasa pia amepigwa picha akinywa chai pamoja na wenyeji katika kibanda cha kuuza chakula kilichokandikwa kwa udongo.

Picha zingine zinamuonyesha akitumia jiko la kienyeji la mawe tatu kumpikia chai mjane wa miaka 67- lingawa anaonekana akiwa amevalia viatu vya bei ghali.

MP Didmus Barasa makes tea at a fireplace

Chanzo cha picha, DIDMUS BARASA

Hakuwashinda kila mtu na matukio haya ya unyumba, akipata maoni yasiyofaa kwenye mitandao ya kijamii.

Aliyekuwa Seneta Boni Khalwale ambaye anagombea tena ugavana wa Kakamega, magharibi mwa Kenya, alitaka kuthibitisha stakabadhi zake za barabarani kwa kuchagua kung'arisha viatu vyake kando ya barabara.

Alikaa akila mahindi ya kuchoma huku akisubiria asafishiwe.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?
Kakamega senatorial aspirant Boni Khalwale (in yellow) eating roasted maize

Chanzo cha picha, BONI KHALWALE

Aliambatanisha picha hiyo na maneno "Kazi ni Kazi".

Haua ya Bw Khalwale bia iliwakasirisha Wakenya katika mitandao ya kijamii, kuashiria kwamba mbinu hizo za ushawishi hazifanyi kazi kila wakati.

Mbunge wa Embakasi Magharibi George Theuri alishirikisha mtandaoni picha inayomuonyesha akitembea bila viatu na kuambatanisha picha hiyo na maneno: "Napendezwa na mtaa wangu Loving every ".

MP George Theuri walking barefoot

Chanzo cha picha, GEORGE THEURI

Bw Theuri pia alivalia kaptura kwenye picha na kumfanya mmoja wa wafuasi wake kusema, "Inahitaji ujinga wa hali ya juu kuwaamini wanasiasa kama hao."

Miezi mitano iliyopita Seneta Isaac Mwaura alijizatiti zaidi kupata tikiti ya chama chake kugombea ubunge Nairobi kwa kuwasaidia wachuuzi kukata mboga.

Senator Isaac Mwaura (in yellow) chopping vegetables

Chanzo cha picha, ISAAC MWAURA

Bw Mwaura alisema anajaribu kuelewa matatizo ya wafanyabiashara wadogo katika eneo bunge lake la Ruiru lililopo viungani mwa mji mkuu.

"Cha kusikitisha...hukujua mama na baba mboga [wachuuzi wa mboga] wamekuwepo hadi sa. Ilichukua mapambazuko ya mwaka wa uchaguzi kuamshwa na ukweli huu," mtu mmoja alichapisha kwenye mtandao wa kijamii.

Hatua hiyo hata hivyo haikusaidia mwanasiasa huyo kwani alingushwa katika kinyang'anyiro cha kuwania tikiti ya chama chake.

th

Pia unawezakusoma:

th