Mlipuko watokea nje ya ubalozi wa Marekani huko Norway – Polisi

Chanzo cha picha, Reuters
Polisi nchini Norway wamezingira eneo linalozunguka ubalozi wa Marekani mjini Oslo baada ya mlipuko kuripotiwa katika eneo hilo.
"Idadi kubwa ya maafisa wa usalama" imetumwa katika eneo hilo takriban saa 1:00 usiku wa manane (GMT), polisi walisema.
"Polisi wanafanya mazungumzo na ubalozi na hakuna majeraha yaliyoripotiwa," ilisema taarifa hiyo.
"Kwa sasa hakuna taarifa kuhusu hasa kilichotokea au ni nani anayeweza kuhusika," polisi waliongeza.
Michael Dellemyr, ambaye anaongoza kundi la polisi waliofika eneo la tukio, aliambia mtangazaji wa Norway NRK kwamba mlipuko huo ulitokea kwenye mlango wa umma wa jengo hilo.
Ubalozi ulipata uliharibiwa kidogo, ripoti za vyombo vya habari zinasema.
Ubalozi wa Marekani upo katika wilaya ya Morgedalsvegen ya Oslo, yapata kilomita 7 (maili nne) nje ya katikati mwa jiji.
Soma zaidi:

