Moja kwa moja, Moto mkubwa waunguza mnara wa Jiji la Kuwait

Mashambulizi makali yamekumba maghala ya mafuta mjini Tehran, huku baadhi wakiambia BBC kwamba ilikuwa ni kana kwamba usiku umegeuka mchana.

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Mlipuko watokea nje ya ubalozi wa Marekani huko Norway – Polisi

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Polisi nchini Norway wamezingira eneo linalozunguka ubalozi wa Marekani mjini Oslo baada ya mlipuko kuripotiwa katika eneo hilo.

    "Idadi kubwa ya maafisa wa usalama" imetumwa katika eneo hilo takriban saa 1:00 usiku wa manane (GMT), polisi walisema.

    "Polisi wanafanya mazungumzo na ubalozi na hakuna majeraha yaliyoripotiwa," ilisema taarifa hiyo.

    "Kwa sasa hakuna taarifa kuhusu hasa kilichotokea au ni nani anayeweza kuhusika," polisi waliongeza.

    Michael Dellemyr, ambaye anaongoza kundi la polisi waliofika eneo la tukio, aliambia mtangazaji wa Norway NRK kwamba mlipuko huo ulitokea kwenye mlango wa umma wa jengo hilo.

    Ubalozi ulipata uliharibiwa kidogo, ripoti za vyombo vya habari zinasema.

    Ubalozi wa Marekani upo katika wilaya ya Morgedalsvegen ya Oslo, yapata kilomita 7 (maili nne) nje ya katikati mwa jiji.

    Soma zaidi:

  2. Moto mkubwa waunguza mnara wa jiji la Kuwait

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Ni siku nyingine tena tunapokutana, tukiwa tayari kukuletea habari kuhusu mzozo wa Mashariki ya Kati, ambao sasa umeingia wiki yake ya pili.

    Maghala ya mafuta mjini Tehran yameshambuliwa, maafisa wa Lebanon wanasema watu wanne wameuawa katika shambulio la Israel kwenye hoteli moja mjini Beirut, na Israel inasema iliwashambulia "makamanda wakuu" wa Kikosi cha Lebanon cha Wakurdi, ambacho ni tawi la operesheni za nje ya nchi la IRGC.

    Mataifa ya Ghuba pia yamekuwa yakiripoti makombora na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani.

    Moto mkubwa umeteketeza mnara huko Kuwait, ambapo jeshi linasema limekuwa likikabiliana na "wimbi la ndege zisizo na rubani za adui zilizovamia anga ya nchi hiyo".

    "Baadhi ya vituo vya raia vimeharibika kutokana na vifusi na vipande vya silaha vilivyoanguka wakati wa operesheni ya kuzuia ndege za adui," msemaji rasmi wa Wizara ya Ulinzi amenukuliwa akisema katika chapisho kwenye mtandao wa X, lililoshirikishwa na jeshi la Kuwait.

    Jeshi la anga la nchi hiyo "linaendelea kushambulia maeneo fulani angani ya maadui", msemaji huyo anasema, huku jeshi likiwahimiza raia na wakazi "kufuata maagizo ya usalama na usalama".

    Soma zaidi:

  3. Hujambo na karibu katika matangazo yetu mubashara ya tarehe 08/03/2026.