Uchaguzi Kenya 2022:Utaratibu wa kupiga kura Kenya

Maelezo ya video, Fahamu utaratibu wa kupiga kura nchini Kenya

Wapiga kura nchini Kenya wanajitayarisha kuwachagua viongozi wao tarehe tisa mwezi Agosti mwaka huu .

Mojawapo ya masuala muhimu yatakayofanyika siku hiyo ni kwa wapiga kura kufahamu jinsi ya kutekeleza haki hiyo yao-kupiga kura .

Uchaguzi wa Agosti 9 utashuhudia idadi kubwa zaidi ya vituo vya kupigia kura , pamoja na wapiga kura waliojiandikisha.

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imebainisha kuwa jumla ya vituo 46,232 vimesajiliwa mwaka wa 2022, ikiwa ni ongezeko la asilimia 13.08 kutoka 2017 ambapo vituo 40,883 vilisajiliwa. Idadi ya wapiga kura waliojiandikisha pia imeongezeka kutoka 19,611,423 hadi 22,120,458 sawa na ongezeko la asilimia 12.79.

th

Mtu anapiga vipi kura?

Woman votes in Gatundu

Chanzo cha picha, EPA

•Mpiga kura anafika kituo alichosajiliwa kupiga kura. Kisha anatakiwa kutoa kitambulisho cha kitaifa au pasipoti aliyotumia kujiandikisha kupiga kura .

•Maafisa wa tume ya uchaguzi watahakiki ikiwa aliyefika amesajiliwa kupiga kura katika kituo hicho, kwa kuweka kidole chake kwenye mtambo wa kuwatambua wapiga kura kwa kutumia alama ya kidole.

•Mpiga kura atakabidhiwa karatasi sita za kupigia kura - ya rais, mbunge, gavana, seneta, mwakilishi wa wanawake na diwani (mwakilishi wa wadi) - zilizopigwa muhuri na zenye majina na vyama vya wagombeaji .

•Mpiga kura atasonga hadi eneo la faragha na kumchagua mgombea anayemtaka kwa kuweka alama ndani ya sehemu (kisanduku) iliyotengwa katika karatasi ya kura.

•Tumbukiza karatasi yako ya kura ndani ya sanduku lifaalo kwa kila kura (rais, mbunge na kadhalika).

•Kidole chako kitapakwa rangi isiyofutika kwa urahisi kuzuia watu waliopiga kura kurudia kupiga kura tena.

•Ondoka kutoka kituo cha kupiga kura.

th

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Nani anayeruhusiwa kupiga kura?

Kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi nchini kenya mtua anaruhusiwa kupiga kuwa iwapo atatosheleza vigezo vifuatavyo;

(a) ni raia mtu mzima;

(b) hajatangazwa kuwa na akili taahira; na

(c) hajatiwa hatiani kwa kosa la uchaguzi katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Raia ambaye ana sifa za kuandikishwa kama mpiga kura ataandikishwa katika kituo kimoja tu cha uandikishaji.

Mipango ya kiutawala ya uandikishaji wa wapiga kura na uendeshaji wa uchaguzi itaundwa ili kuwezesha, na haitamnyima raia anayestahiki haki ya kupiga kura au kugombea.

Kunyimwa Haki ya kupiga kura nchini Kenya

Hali ambayo inaweza kusababisha mtu kunyimwa haki ya kupiga kura nchini Kenya ni pamoja na zifuatazo:

1. Sio Raia wa Kenya

Mtu anaweza kunyimwa haki ya kupiga kura nchini Kenya ikiwa mtu huyo si raia wa Kenya. Kuna njia tatu za kuwa raia wa Kenya ambazo ni kwa kuzaliwa, kujiandikisha au kupata uraia. Uthibitisho wa kitambulisho cha kitaifa (ID) au pasipoti halali ya Kenya unahitajika ili kupiga kura nchini Kenya.

Kwa hivyo, ikiwa mtu si raia wa Kenya, hawezi kupiga kura katika uchaguzi.

2. Sio Wa Umri wa ufaao kupiga kura.

Ikiwa mtu yeyote yuko chini ya umri wa miaka kumi na minane, hastahili kupiga kura nchini Kenya. Kwa hivyo watoto wadogo hawawezi kupiga kura kwa vile umri wa kupiga kura nchini Kenya ni miaka 18 na zaidi. Ushahidi wa kuwa mtu mzima ni aidha kitambulisho cha taifa (ID) au pasipoti halali ya Kenya.

3. Mtu asiyekuwa na akili timamu

Kuwa na akili timamu maana yake mtu anaweza kufikiri, kuelewa na kujiamulia. Watu wazima kwa ujumla hufikiriwa kuwa na akili timamu isipokuwa hali zibadilike. Kwa hivyo, mtu asiye na akili timamu anaweza kunyimwa haki ya kupiga kura nchini Kenya.

4. Kutiwa hatiani kwa Kosa la Uchaguzi

Kunyimwa haki ya kupiga kura nchini Kenya kunatumika kwa yeyote aliyepatikana na hatia ya makosa ya uchaguzi katika kipindi cha miaka mitano iliyotangulia.

5. Mahali pabaya pa kujiandikisha

Ikiwa mpiga kura atajiwasilisha katika kituo cha kupigia kura ambacho ni tofauti na alichojiandikisha, basi anaweza kunyimwa haki ya kupiga kura. Kila mpiga kura anapaswa kuhakikisha kuwa anajitokeza katika kituo cha kupigia kura alichojiandikisha.

6. Kujisajili kama mpiga kura mara mbili

Iwapo mtu atagundulika kuwa amejiandikisha mara mbili katika rejista ya wapiga kura, basi mtu huyo anaweza kunyimwa haki ya kupiga kura.

7. Hana Kitambulisho

Wakati wa siku ya uchaguzi, ikiwa mtu hana kitambulisho chake cha kitaifa (ID) au pasipoti halali ya Kenya aliyojiandikisha nayo, au ikiwa mojawapo ya hati hizi ina kasoro, anaweza kunyimwa haki ya kupiga kura.

8. Hakuna Jina Katika Daftari la Wapiga Kura

Ikiwa jina la mtu halipo kwenye rejista ya wapiga kura, basi mtu huyo anaweza kunyimwa haki ya kupiga kura. Kwa hivyo, ni muhimu kujiandikisha kama mpiga kura wakati wa mchakato wa usajili wa wapiga kura.

9. Kizuizi cha Wakati/Muda

Ikiwa mtu atajiwasilisha kwenye kituo cha kupigia kura nje ya saa alizopangiwa za kupiga kura wakati wa siku ya uchaguzi, anaweza kunyimwa haki ya kupiga kura.Hata hivyo hilo linaweza pia kutegemea muda ambao upigaji kura ulianza katika kituo hicho ama wakati kituo husika kilifunguliwa.Tume ya uchaguzi hutoa mwongozo kuhusu hali ambazo zinaweza kulazimisha muda kuongezwa katika baadhi ya vituo.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Kura iliyoharibika ni ipi?

Kuna sababu nyingi ambazo husababisha kura kuharibika na hivyo kutohesabiwa.

Kuu zaidi huwa ni mpiga kura kuweka alama kwa njia isiyofaa wakati wa kuchagua mgombea au chama anachokitaka.

IEBC inasema mpiga kura anatakiwa kuweka "alama kwenye nafasi iliyotengwa kwa jina la chama/mgombeaji au picha ya chama unachokichagua."

Mpiga kura anafaa "kuweka alama kwa mgombeaji mmoja tu." Hufai kuweka alama yoyote nyingine kwenye karatasi ya kura.

Alama unayoweka inaweza kuwa alama ya ndio (✓), mkasi (✕), au hata alama ya kidole. Hata hivyo, huruhusiwi kuandika jina lako au kuweka sahihi yako kama alama ya kumchagua mgombea unayemtaka. Iwapo utafanya makosa bila kukusudia wakati wa kuweka alama yako kwenye karatasi ya kura na utambue hilo kabla ya kutumbukiza karatasi yako kwenye sanduku, unaweza kupewa karatasi nyingine ya kura. Unaweza kupewa karatasi mpya ya kura mara mbili pekee.

Baada ya kumaliza kuweka alama, unafaa kuikunja karatasi katikati -kutoka kushoto kwenda kulia ili kuweka siri uliyemchagua halafu utumbukize karatasi hiyo kwenye sanduku lifaalo.

Tume ya uchaguzi imepiga marufuku kurandaranda katika kituo baada ya kupiga kura. Vile vile, ni hatia kupiga picha katika kituo cha kupiga kura au kupiga picha karatasi za kura.

th

Uchaguzi Kenya 2022:Unaweza pia kusoma

th