Habari katika picha:Hii ni Sudan halisi ninayotaka kuionyesha dunia

Twelve-year-old Alaa writes in English on the blackboard at her school in Sudan's capital, Khartoum.

Chanzo cha picha, Ola Alsheikh

Maelezo ya picha, Alaa ni mtoto mwenye umri wa miaka 12 akiandika lugha ya kiingereza kwenye ubao katika shule moja iliyoko katia mji mkuu wa Khartoum,Sudan

"Watu huku hawajazoea kumuona mwanamke ameshika kamera na kuzunguka katika mitaa kupiga picha lakini niliamua kuwa napiga picha ya kila nnachopendezewa nacho" mpiga picha Ola Alsheikh aeleza

Kuchekwa,kutokubalika au kudharaulika na watu wasiomjua ndio mambo ambayo Ola anakabiliana nayo kila mara katika mji huo wa Khartoum lakini alikataa kukatishwa tamaa.

"Nataka kuonesha maisha halisi ya Sudan kwa maana tumekuwa tunapewa picha za kusadikika na dunia yote kwa muda mrefu juu ya Sudan"Ola aliongeza.

Hizi ni miongoni mwa picha anazozipenda mpiga picha huyo

A woman hangs raw beef on a line outside

Chanzo cha picha, Ola Alsheikh

Maelezo ya picha, Nyama hii iliyokaushwa inaitwa Sharmoot ,ni miongoni mwa chakula kinachopendwa zaidi nchini Sudan na huwa inaliwa pamoja na uji.Picha hii inamuonesha mwanamke aliyekuwa anakausha nyama nyumbani kwake
A girl wearing pigtails with several multi-coloured stands with her back to the camera

Chanzo cha picha, Ola Alsheikh

Maelezo ya picha, "Mtindo wa nywele za binti huyu zilinivutia" Ola alisema.
A fruit seller stands in front of his shop window with crates of fruit visible next and behind him

Chanzo cha picha, Ola Alsheikh

Maelezo ya picha, Muuza matundar Soleiman Mohamed Toum akiuza matikitimaji,zabibu na ndizi katika duka lake lililopo kisiwani
A boy's foot is seen dribbling a football around a cone

Chanzo cha picha, Ola Alsheikh

Maelezo ya picha, "mchanganyiko wa rangi wa kijana aliyekuwa anacheza mpira wa mguu ulimvutia," Ola alisema.
A man looks in the mirror while a barber shaves his head

Chanzo cha picha, Ola Alsheikh

Maelezo ya picha, "Kinyozi mtaani ni miongoni mwa mambo mapya ambayo yameanza kuepo mjini Khartoum," Ola anasema"Kabla kulikuwa na maduka ambayo wanaume waliweza kunyoa nywele zao lakini sasa vinyozi wapo hata sokoni,mtaani au katika vituo vya daladala".
A portrait of a woman framed with white flowers

Chanzo cha picha, Ola Alsheikh

Maelezo ya picha, Mwanamitindo Nuha Malik ni rafiki yake Ola kwa muda mrefu na picha hii inaonesha mfululizo wa picha zilizopo kwenye mtandao kwenye mtandao wa instagram zikionyesha mitindo ya nywele
A man stands in front of a mural with paint and a brush in his hands

Chanzo cha picha, Ola Alsheikh

Maelezo ya picha, Mchoraji Sari Awad akionesha picha aliyochora inayowasisitiza jamii kuwa na umoja na ubinadamu
A bus is seen at the end of a long and empty colonnade painted in various colours

Chanzo cha picha, Ola Alsheikh

Maelezo ya picha, Katika picha hii Ola anasema alipenda ukimya uliotawala siku ya ijumaa na alipenda pia muonekano wa rangi katika eneo hilo pamoja na gari.
A woman stands close to a horse, holding it by its reins.

Chanzo cha picha, Ola Alsheikh

Maelezo ya picha, "Enas Siddig ni muendesha farasi anayeiwakilisha Sudan kimataifa