Korea Kaskazini: Binti wa Kim Jong Un anayetajwa kama 'mrithi wake ajaye' ni nani?

North Korean leader Kim Jong Un talks with his daughter Kim Ju Ae at a banquet to celebrate the 75th anniversary of the Korean People's Army in Pyongyang, 7 February 2023

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Kim Ju Ae alionekana kwa mara ya kwanza hadharani mnamo 2022 - katika picha hii, na baba yake wakiwa kwenye karamu ya maadhimisho ya miaka 75 ya Jeshi la Watu wa Korea, Februari 2023
    • Author, Luis Barrucho
    • Nafasi, BBC World Service

Binti mdogo wa kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, ndiye mwenye "uwezekano zaidi" wa kumrithi , kwa mujibu wa shirika la ujasusi la Korea Kusini, National Intelligence Service (NIS). Lakini je tunajua nini kuhusu Kim Ju Ae, na ni kwa kiasi gani anaweza kuchukua nafasi ya baba yake siku moja?

Kim Jong Un ni msiri sana kuhusu familia yake na ni machache machache sana yanayojulikana kuhusu familia yake.

Alimtunza kwa siri mkewe, Ri Sol Ju, kwa muda baada ya harusi yao - hakuonekana hadharani kwa mara ya kwanza hadi ilipofika mwaka 2012.

Vyombo vya habari vya Korea Kusini viliripoti kuwa walifunga ndoa mwaka 2009 na kupata mtoto mwaka 2010. Pia anafikiriwa kuwa ndiye mama wa Kim Ju Ae, ambaye alizaliwa miaka michache baadaye.

Mara ya kwanza kwa Kim Ju Ae kutajwa hadharani ilikuwa mwaka 2013, baada ya nyota wa mpira wa kikapu wa Marekani Dennis Rodman kufanya ziara ya utata nchini Korea Kaskazini.

Rodman alisema kuwa alitumia muda na familia ya Kim, akipumzika kando ya bahari na "kumpakata mtoto wao", ambaye alimuita Ju Ae.

An undated photo released by the official North Korean Central News Agency (KCNA) on 05 January 2024 shows Kim Jong Un and Ju Ae inspecting a missile launcher production facility in an undisclosed location in North Korea

Chanzo cha picha, EPA-EFE/REX/Shutterstock

Maelezo ya picha, Kim Jong Un na Kim Ju Ae wakikagua kituo cha utengenezaji wa makombora katika eneo lisilojulikana Korea Kaskazini, Januari 2024

Hata vyombo vya habari vya Korea Kaskazini "vinamtambua kama binti wa Kim Jong Un, bila kutaja jina au umri wake", anasema Fyodor Tertitskiy, ambaye anatafiti siasa za Korea Kaskazini katika Chuo Kikuu cha Kookmin mjini Seoul. "Hakuna kitu kingine kinachojulikana, angalau kwa umma," anaongeza. Anakadiria kuwa yuko kati ya umri wa miaka 10 na miaka 13.

Katika mkutano wa faragha mwaka jana, NIS iliwaambia wanasiasa wa Korea Kusini kwamba Kim Ju Ae hakuwahi kuandikishwa katika kituo rasmi cha elimu na alikuwa akisomea nyumbani mjini Pyongyang. Iliongeza kuwa alifurahia burudani kama vile farasi, kuogelea na kuteleza kwenye barafu.

Mmoja wa watu waliohudhuria mkutano huo baadaye aliwaambia waandishi wa habari kwamba Kim Jong Un anafurahia hasa ujuzi wake wa kuendesha farasi.

NIS ilisema alikuwa na kaka mkubwa na ndugu mdogo ambaye jinsia yake haijathibitishwa. Hawajawahi kuonekana hadharani.

Kuonakana hadharani

Kim Jong Un and Kim Ju Ae visiting the Kwangchon Chicken Farm near Pyongyang, January 2024

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Kim Jong Un na Kim Ju Ae wakitembelea shamba la kuku la Kwangchon karibu na Pyongyang, Januari 2024
Hauhitaji Whatsapp
BBC Swahili sasa kwenye WhatsApp

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Bonyeza hapa kujiunga

Mwisho wa Whatsapp

Kim Ju Ae alijitokeza hadharani mnamo Novemba 2022 alipohudhuria jaribio la kombora na baba yake na tangu wakati huo ameonekana akiwa kando yake mara kadhaa, katika matukio ya kijeshi na yasiyo ya kijeshi.

Hivi karibuni, katika sherehe ya mkesha wa mwaka mpya katika uwanja wa Pyongyang Mei 1, yeye na baba yake walibusiana kwenye shavu.

Mwezi Disemba, walihudhuria uzinduzi wa kombora la masafa marefu la Hwasong-18 la Korea Kaskazini (ICBM), ambalo ni kombora la masafa marefu zaidi katika silaha za nchi hiyo. Pia alikuwa pamoja naye kwa uzinduzi wa satelaiti ya upelelezi ya Malligyong-1 mnamo Novemba. Pyongyang ilidai kuwa itampa Kim Jong Un mtazamo wa ikulu ya White House.

Mnamo Februari 2023 Radio Free Asia iliripoti kuwa serikali ya Korea Kaskazini ilikuwa ikiamuru mtu mwingine yeyote aitwaye Kim Jun Ae kubadilisha jina lake, ambalo lilisemekana ni la kawaida linapokuja suala la utawala wa kiimla.

Waangalizi wa Korea Kaskazini pia wanabaini kuwa Kim Ju Ae sasa anatajwa kama binti "anayeheshimika", badala ya "mpendwa". Kivumishi "kuheshimiwa" kimehifadhiwa kwa ajili ya heshima zaidi ya Korea Kaskazini.

Katika kesi ya Kim Jong Un, kwa mfano, alitajwa kama "mshirika aliyeheshimiwa" tu baada ya hadhi yake kama kiongozi ajaye kuimarishwa.

Kim Jong Un and Kim Ju Ae discuss North Korea's military reconnaissance satellite programme, May 2023

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Kim Jong Un na Kim Ju Ae wajadili mpango wa satelaiti ya kijeshi ya Korea Kaskazini, Mei 2023

Kuna uwezekano akawa mrithi ?

Korea Kaskazini imejitenga sana na haijulikani kwa ulimwengu wa na wengi wanajiuliza kwanini kuonekana kwa Kim Ju Ae karibu na baba yake imekuwa mara kwa mara.

Raia wa Korea Kaskazini wanaambiwa kuwa Kims anatoka kwenye damu takatifu, ikimaanisha tu hao ndio watu wanaweza kuongoza nchi na baadhi ya wachambuzi wanasema kuwa kumtambulisha kwa umma katika umri mdogo kama huo inaweza kuwa njia ya kiongozi wa Korea Kaskazini ya kuhakikisha kuwa binti yake anajiimarisha muda mrefu kabla ya kuchukua madaraka.

Hakuna pendekezo kwamba huenda kurithishwa kwake mamlaka kukatokea wakati wowote hivi karibuni, na uvumi wa zamani kwamba Kim Jong Un alikuwa katika hali mbaya ya afya umetupiliwa mbali.

Kim Jong Un and Kim Ju Ae viewing a military parade at Kim Il Sung Square to mark the 75th anniversary of the founding of the Korean People's Army (KPA), February 2023

Chanzo cha picha, KCNA/EPA-EFE/REX/Shutterstock

Maelezo ya picha, Kim Jong Un na Kim Ju Ae katika gwaride la kijeshi katika uwanja wa Kim Il Sung kuadhimisha miaka 75 tangu kuanzishwa kwa Jeshi la Watu wa Korea, Februari 2023

Wengine wanasema inaweza pia kuwa njia ya Kim Jong Un kuashiria kwamba yeye ni baba anayejali familia katika jamii iliyotawaliwa na mfumo dume.

"Pamoja na viongozi wa zamani Kim Jong Il na Kim Il Sung, kulikuwa na propaganda nyingi zinazolenga jukumu la kiongozi wa Korea Kaskazini kama mtu wa mama na baba," anasema Edward Howell, mhadhiri wa siasa katika Chuo Kikuu cha Oxford na mtaalam wa rasi ya Korea. "Kwa hiyo nadhani ishara hii pia imeendelea kwa kumuonyesha na baba yake hadharani."

Tangu kuanzishwa kwa Korea Kaskazini mwaka 1948, imekuwa ikitawaliwa na wanaume wa familia ya Kim na iwapo Kim Ju Ae atamrithi baba yake, atakuwa mwanamke wa kwanza kuiongoza nchi hiyo.

Lakini "kuwa na mwanafamilia wa damu ya Kim ni muhimu sana kwa uongozi wa Korea Kaskazini iwapo ni mwanamke, ni bora kuliko kuwa na mtu ambaye sio kutoka wa familia ya Kim," Howell anasema.

Kim Jong Un and Kim Ju Ae visiting the Kwangchon Chicken Farm near Pyongyang, January 2024

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Kim Jong Un na Kim Ju Ae wakitembelea ufugaji wa kuku la Kwangchon karibu na Pyongyang, Januari 2024

Anaamini pia kuna mgombea mwingine anayeweza kumrithi Kim Jon Un - dada wa kiongozi huyo, Kim Yo Jong, ambaye alitajwa kwa mara ya kwanza katika vyombo vya habari vya serikali mwezi Machi 2014.

Anashikilia nafasi ya juu katika chama tawala cha Wafanyakazi wa Korea.

"Yeye ana umri mkubwa zaidi kuliko Kim Ju Ae na ni wazi ana uzoefu zaidi katika siasa za Korea Kaskazini," anasema. "Kwa hivyo iwe ni binti au dada, wanaweza kuwa wote ni wanawake, lakini kuwa na Kim ni jambo muhimu zaidi."

NIS ya Korea Kusini pia ilisema bado inafikiria "uwezekano wote" kwani kuna "mambo mengi" yanayoendelea nchini humo.

Kim Jong Un and Kim Ju Ae watch a missile drill at an undisclosed location, March 2023

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Kim Jong Un na Kim Ju Ae wakiangalia mazoezi ya makombora katika eneo lisilojulikana, Machi 2023

Fyodor Tertitskiy anaamini kuwa Kim Jong Un amekuwa "akiujaribu umma na maoni ya wasomi kuhusu uwezekano wa kurithi" kwa kumuonyesha Kim Ju Ae hadharani - jambo ambalo anasema halifanyiki hadi pale mrithi atakapothibitishwa.

Anakiri kwamba ni mapema kuzungumzia mrithi wa Kim Jong Un.

"Kama atasema, atakufa akiwa na umri sawa na baba yake, akiwa na umri wa miaka 70, hiyo itakuwa mwaka 2054. Hata kama tunadhani kwamba taifa la Korea Kaskazini litaishi hadi wakati huo katika hali yake ya sasa, jamii huenda isiwe sawa na ilivyo sasa," anasema.

"Pia, mtu anapaswa kutambua kwamba kuna tofauti kati ya kukubali usawa wa jinsia kwa ujumla na kumkubali mtawala wa kike," anaongeza.

Imetafsiriwa na Dinah Gahamanyi