Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022:Raila Odinga apinga matokeo ya uchaguzi

Chanzo cha picha, Various
- Author, Abdalla Seif Dzungu
- Nafasi, BBC Swahili
- Muda wa kusoma: Dakika 2
Kiongozi wa Muungano wa Azimio nchini Kenya Raila Odinga amepinga matokeo ya uchaguzi uliomtangaza naibu wa rais William Ruto kuwa ndiye rais Mteule.
Raila amesema kwamba hakubaliani na matokeo hayo kwasababu mwenyekiti wa tume hiyo alikiuka katiba kabla ya kumtangaza mshindi
Amesema kwamba makamishna wa tume hiyo hawakukubaliana kuhusu hesabu ya mwisho ya matokeo hayo yaliompatia ushindi William Ruto.
''Takwimu zilizotangazwa na Chebukati ni batili kwa maoni yetu, hakuna mshindi kisheria, aliyetangazwa kihalali wala rais mteule''.
Hatahivyo Raila Bw Odinga aliwataka wafuasi wake kudumisha amani na utulivu huku muungano huo ukifuata njia za kikatiba za kubatilisha matamshi ya Bw Chebukati.
''Jana, demokrasia yetu changa ilikumbwa na msukosuko mkubwa, kwa sababu hiyo, Kenya inakabiliwa na mgogoro mkubwa wa kisheria na kisiasa kutokana na matendo ya Wafula Chebukati''.
''Tunafuatilia njia za kisheria na za amani. Tuna hakika kwamba haki itatendeka. Tunaelewa kuwa ni Bw Chebukati pekee ndiye aliyepata kujumlisha kura za urais. Aliwanyima makamishna wote kupata taarifa hizo'', aliongezea Raila akizungumza na vyombo vya habari jijini Nairobi.
Haipatikani tena
Tazama zaidi katika FacebookBBC haihusiki na taarifa za kutoka mitandao ya nje.Mwisho wa Facebook ujumbe
Matamshi yake yanajiri muda mfupi tu baada ya makamishna wanne kati ya saba wa tume ya uchaguzi kujitenga na matokeo wakidai kwamba yalikumbwa na 'kiza kinene'.
Makamishna hao wakiongozwa na naibu mwenyekiti wa tume hiyo Juliana Cherera wamesema kwamba hawakukubaliana kuhusu matokeo yaliotangazwa na Wafula Chebukati.
Walisema kwamba hesabu iliotolewa na Chebukati ya asilimia 100.1 haikuingiliana na jumla ya matokeo ya urais ya wagombea wote wanne.
Akizungumza na waandishi wa habari Raila aliongezea kwamba mwenyekiti huyo hakujadiliana na makamishna wenzake kuhusu matokeo hayo kabla ya kuyatangaza.

- MATAYARISHO:Uchaguzi Kenya 2022: Je Kenya iko tayari kwa uchaguzi mkuu?
- YA MSINGI:Uchaguzi Kenya 2022: Kwa nini uchaguzi wa Kenya mwaka huu ni muhimu?
- MIUNGANO:Uchaguzi Kenya 2022: Musalia Mudavadi kujiunga na naibu rais William Ruto itabadilisha siasa za Kenya?
- UNAYOFAA KUJUA:Uchaguzi Kenya 2022: Je Naibu wa rais wa Kenya William Ruto anakabiliwa na changamoto gani katika kumteua naibu wake wa rais?
- UCHAMBUZI:Uchaguzi wa Kenya 2022: Je hatua ya Rais Kenyatta kumuunga mkono Raila Odinga itamsaidia au kumharibia?
- WASIFU:William Ruto: Muuza kuku aliyepanda ngazi hadi kuwa naibu wa rais wa Kenya
- RAILA ODINGA:Uchaguzi Kenya 2022: Siwezi kuwa kibaraka wa mtu yeyote-Raila Odinga













