Kenya 'yaishtaki' Tanzania EAC kwa kupiga marufuku biashara ndogondogo kwa wageni

Kenya inasema hatua ya Tanzania inakiuka Itifaki ya Soko la Pamoja la EAC, hasa Ibara ya 13(1), 13(3)a, 13(5), 13(8), na 13(9), ambayo inalinda uhuru wa watu, huduma, na haki ya kuanzishwa miongoni mwa nchi washirika.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Dinah Gahamanyi & Asha Juma & Abdalla Dzungu

  1. Kenya yawasilisha malalamiko rasmi kwa EAC dhidi ya hatua ya Tanzania kupiga marufuku biashara za kigeni

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Serikali ya Kenya imeiandikia rasmi Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kupinga agizo tata la Tanzania la kupiga marufuku watu wasio raia kujihusisha na shughuli mbalimbali za kibiashara, ikionya kuwa hatua hiyo inatishia ushirikiano wa kiuchumi wa kikanda.

    Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Caroline Karugu Alhamisi alithibitisha kuwa Kenya iliwasilisha malalamiko rasmi kwa jumuiya hiyo ya kikanda, na kuitaka kuishinikiza Tanzania kupitia upya Agizo la Leseni za Biashara (Marufuku ya Shughuli za Biashara kwa Wasio Raia), 2025.

    Agizo hilo lililotolewa na Waziri wa Biashara na Viwanda wa Tanzania, Selemani Saidi Jafo Jumanne, linawawekea vikwazo wageni kujihusisha na aina 15 za biashara, linatoa adhabu kubwa ikiwa ni pamoja na faini isiyopungua TSh10 milioni (Ksh.501, 584), kifungo cha hadi miezi sita, na kufutiwa viza na vibali vya ukaazi.

    Dkt. Karugu amesema maagizo hayo “yanakiuka moja kwa moja” Itifaki ya Soko la Pamoja la EAC, hasa Ibara ya 13(1), 13(3)a, 13(5), 13(8), na 13(9), ambayo inalinda uhuru wa watu, huduma, na haki ya kuanzishwa miongoni mwa nchi washirika.

    "Agizo hili linadhoofisha malengo ya msingi ya ushirikiano wa kiuchumi wa kikanda na kurudisha nyuma kwa kiasi kikubwa mafanikio yaliyopatikana chini ya Itifaki ya Soko la Pamoja la EAC," Dkt. Karugu alisema.

    Kenya sasa inataka Sekretarieti ya EAC kuitaarifu Tanzania kuhusu wajibu wake chini ya Mkataba wa EAC na sheria za jumuiya na kushinikiza kuangaliwa upya kwa agizo hilo.

  2. Marekani kuiwekea vikwazo mamlaka ya Palestina

    Marekani inasema itaiwekea vikwazo mamlaka ya Wapalestina pamoja na chombo kinachoiwakilisha katika jukwaa la kimataifa.

    Vikwazo hivyo vinaathiri Mamlaka ya Palestina (PA) ambayo ilianzishwa na makubaliano ya amani ya Oslo, na Jumuiya ya Ukombozi wa Palestina (PLO) ambayo ilitambuliwa baada ya mchakato sawa na mwakilishi rasmi wa watu wa Palestina, kwa kuwacha ghasia na kuitambua Israel.

    Wizara ya Mambo ya Nje inasema kwamba itakataa visa, ambazo zitazuia kusafiri kwenda Marekani kwa maafisa wa Palestina. Vikwazo hivvyo vinaonekana vidogo, lakini hatua hiyo inaongeza mzozo wa kidiplomasia katika utawala wa Trump.

    Hatua hiyo inaonekana kuwa jibu la Marekani kwa mkutano wa wiki hii unaoongozwa na Ufaransa-Saudi katika Umoja wa Mataifa kutafuta uungwaji mkono wa suluhu ya mataifa mawili ya baadaye.

    Mkutano huo ulikuja huku Ufaransa, Uingereza na Canada zikijitolea kulitambua taifa huru la Palestina ambalo halina jeshi baadaye mwaka huu. Marekani ilikashifu hatua hizo na kuuita mkutano huo "maonyesho."

    Kama nilivyoandika jana usiku, tukio la New York lilizidi kuitenga Marekani katika uungaji mkono wake usio na kikomo kwa jinsi Israel inavyoendeleza vita huko Gaza, jambo ambalo nchi nyingi zililaani katika mkutano huo.

    Mkutano huo uliangazia ombi la kimkakati lililoachwa na Washington ambalo kijadi limeongoza juhudi za kidiplomasia kuelekea kupatikana kwa amani ya muda mrefu kati ya Waisraeli na Wapalestina.

  3. Barcelona wakubali mkataba wa udhamini wa jezi na DR Congo

    .

    Chanzo cha picha, NurPhoto via Getty Images

    Wachezaji wa Barcelona watavalia tishati zenye alama "DR Congo - Heart of Africa" kwenye nyuma ya jezi zao za mazoezi kuanzia mwanzoni mwa msimu ujao, baada ya timu ya soka ya Uhispania kukubaliana juu ya mkataba wa miaka minne na nchi hiyo ya Afrika ya kati.

    Ushirikiano huo unaripotiwa kuigharimu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo euro 44m ($50m; £38m), ingawa klabu hiyo haijafichua kiasi ambacho itapokea.

    Mpangilio huo umekabiliwa na ukosoaji kutoka kwa baadhi ya WaCongo ambao wametilia shaka vipaumbele vya serikali yao, haswa kwa kuwa ligi yake ya kandanda ya ndani imekuwa ikikumbwa na ufadhili duni kwa miaka mingi.

    Lakini mamlaka imetetea makubaliano hayo, na kusema kuwa yatasaidia kuinua hadhi ya nchi.

    Kama sehemu ya mpango huo, uwanja wa Barcelona wa Camp Nou utakuwa mwenyeji wa kile klabu ilichokiita "maonyesho ya kina... ili kuonyesha utofauti wa kitamaduni na utamaduni wa kimichezo" wa DR Congo. Waziri wa Michezo wa nchi hiyo Didier Budimbu aliambia BBC Focus on Africa kwamba makubaliano hayo yanajumuisha kambi ya mazoezi kwa wachezaji 50 vijana wa Congo na makocha 10.

    Barcelona inasema pia itaendesha kambi za watoto katika michezo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na mpira wa vikapu, mpira wa mikono na mpira wa magongo. DR Congo imesaini mikataba kama hiyo na AC Milan ya Italia na timu ya Ufaransa AS Monaco.

    Mwezi uliopita, Budimbu alizitaja kama sehemu ya mkakati wa "kuweka upya" DR Congo kama kiongozi katika fursa za utalii na uwekezaji.

    Tangu mwaka wa 2018, mpinzani wa kanda ya DR Congo Rwanda imekuwa na mkataba wa udhamini na Arsenal ya Uingereza inayotangaza utalii nchini humo yenye kauli mbiu "Tembelea Rwanda" kwenye mikono ya shati za wachezaji.

    Timu ya Ufaransa Paris St-Germain na Bayern Munich ya Ujerumani wana mikataba sawa.

    Haya pia yameshutumiwa, hasa hivi majuzi huku Rwanda ikishutumiwa kuwaunga mkono waasi nchini DR Congo katika mzozo mbaya mashariki mwa nchi, jambo ambalo inakanusha.

    Mnamo Februari, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Thérèse Kayikwamba Wagner aliandika kwa vilabu akihoji "maadili" ya mpangilio huo.

  4. 'Marekani lazima ikubali kulipa fidia kabla ya mazungumzo ya nyuklia'

    .

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araqchi amesema Marekani lazima "ilipe fidia" kwa hasara iliyopata Iran wakati wa vita vya siku 12, huku Iran ikiendeleza msimamo mkali na kuweka masharti mapya ya kuanzisha tena mazungumzo ya nyuklia na utawala wa Trump.

    Katika mahojiano na gazeti la Financial Times lililochapishwa Alhamisi, Julai 31, Abbas Araqchi alisema kuwa Iran haiko tayari kurejea katika hali ya "kawaida" ya siku za nyuma baada ya vita vya siku 12 na Israel, ambapo Marekani pia ilishiriki licha ya kuwa katika mazungumzo na Iran.

    Marekani lazima ieleze ni kwa nini ilitushambulia katikati ya mazungumzo... na lazima ihakikishe kwamba hili halitatokea tena katika siku zijazo. Ni lazima pia ilipe fidia kwa uharibifu iliosababisha," alisema katika mazungumzo hayo yaliyofanyika mjini Tehran.

    Bw. Araghchi, ambaye ni mjumbe mkuu wa Iran katika mazungumzo ya nyuklia, alithibitisha kuwa kulikuwa na mabadilishano ya ujumbe kati yake na mjumbe wa Marekani Steve Whittaker wakati na baada ya vita hivyo, na kulingana na yeye, Iran iliuambia upande wa Marekani kwamba "suluhisho la ushindi" kwa pande zote lazima lipatikane ili kutatua mzozo wa miaka mingi wa mpango wa nyuklia.

    Machaguo ni kidogo, lakini inawezekana," alisema. "Nahitaji kuwashawishi maafisa wangu wakuu kwamba ikiwa tutaingia kwenye mazungumzo, upande wa pili uwe umekuja na nia ya kweli kufikia makubaliano ya ushindi kwa pande zote."

    Soma zaidi:

  5. Ujerumani yasema 'mchakato' wa kulitambua taifa la Palestina 'lazima uanze sasa'

    .

    Chanzo cha picha, EPA

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Johann Wadephul anasema mchakato wa kulitambua taifa la Palestina "lazima uanze sasa".

    Lakini, aliongeza, kwamba "kwa Ujerumani, kutambuliwa kwa taifa la Palestina kuna uwezekano mkubwa kuwa mwisho wa mchakato huo".

    Anasema suluhisho la nchi mbili lililojadiliwa linasalia kuwa "njia pekee ya kufikia suluhu endelevu" kwa mzozo huo, na kuwawezesha "watu wa pande zote mbili kuishi kwa amani, usalama na heshima." Taarifa hiyo ilitolewa kabla ya ziara ya Wadephul nchini Israel na maeneo ya Palestina.

  6. Habari za hivi punde, Trump anasema 'njia ya haraka ya kumaliza' mgogoro wa Gaza ni Hamas kujisalimisha na kuwaachilia mateka

    Donald Trump anasema "njia ya haraka zaidi ya kumaliza Migogoro ya Kibinadamu huko Gaza ni Hamas KUJISALIMISHA NA KUWAACHA MATEKA!!!" katika chapisho kwenye Jukwaa lake la mtandao wa kijamii.

    Kama tulivyoripoti, Trump aliwaambia waandishi wa habari huko Uskochi mapema wiki hii kwamba kulikuwa na "njaa ya kweli" huko Gaza, baada ya Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu kusisitiza kwamba hakuna kitu kama hicho.

    Pia alisema kuwa hatua ya Canada ya kutambua taifa la Palestina inaweza kuhatarisha mpango wa kibiashara na Marekani.

  7. Wizara inayoongozwa na Hamas yasema watu 91 waliuawa wakitafuta msaada siku iliyopita

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Watu 91 wameuawa walipokuwa wakitafuta msaada huko Gaza katika siku iliyopita, wizara ya afya inayosimamiwa na Hamas inasema.

    Katika taarifa ya hivi punde, wizara hiyo inasema kuwa jumla ya watu 111 wameuawa katika saa 24 zilizopita. Huku watu wengine 820 wakijeruhiwa, imeongeza.

    Inaleta jumla ya watu waliouawa Gaza tangu Israel ilipoanzisha kampeni ya kukabiliana na mashambulizi ya Hamas tarehe 7 Oktoba 2023 hadi watu 60,249, wizara hiyo inaongeza.

    Katika taarifa tofauti, wizara hiyo inasema watu wawili wamekufa kwa utapiamlo katika siku iliyopita, na kufanya idadi ya vifo vinavyotokana na njaa tangu kuanza kwa vita kufikia 159.

  8. Marekani na Israel zajibu uamuzi wa Canada wa kulitambua taifa la Palestina

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Marekani Donald Trump ameonya kuwa uamuzi wa Canada wa kulitambua taifa la Palestina unaweza kufanya mazungumzo ya makubaliano ya kibiashara na Marekani kuwa magumu zaidi.

    Israel pia imeikosoa Canada, ikiita hatua hiyo "zawadi" kwa Hamas. Katika ujumbe wake kwenye mtandao wa X-Net, Wizara ya Mambo ya Nje ya Israel ilisema: "Kutambua taifa la aina hiyo kutaathiri juhudi za kufikia usitishaji vita huko Gaza na pia kutazuia mchakato wa kuwaachilia mateka waliosalia.

    Waziri wa Ulinzi wa Israel Israel Katz pia amesema kuwa mipango ya kulitambua taifa la Palestina "inawapa ujasiri Hamas na kuimarisha msimamo wake".

    Haya yanajiri huku Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina Mahmoud Abbas akielezea uamuzi wa Canada wa kulitambua taifa la Palestina kama "uamuzi wa kihistoria".

    Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina pia ilitangaza katika taarifa yake kwenye mtandao wa X-Net: "Uamuzi huu wa kijasiri ni hatua muhimu katika njia ya uadilifu, amani na utimilifu wa haki ya muda mrefu isiyoweza kuondolewa ya watu wa Palestina ya kujitawala".

    Canada ni nchi ya tatu ya uchumi mkubwa kufanya uamuzi kama huo katika siku za hivi karibuni.

    Waziri Mkuu wa Canada Mark Carney amesema kuwa nchi yake italitambua jimbo la Palestina mwezi Septemba.

    Huku Canada ikiitambua Palestina, itakuwa nchi ya tatu wanachama wa G7 kufanya hivyo katika siku za hivi karibuni.

    Wiki iliyopita, Ufaransa pia ilitangaza kuwa italitambua rasmi taifa la Palestina.

    Robo tatu ya wanachama wa Umoja wa Mataifa, 144 kati ya wanachama 193 wa shirika hilo, wanatambua taifa la Palestina.

    Zaidi ya mwaka mmoja uliopita, Norway, Uhispania na Jamhuri ya Ireland zilitangaza rasmi kwamba wanaitambua Palestina kama taifa.

    Soma zaidi:

  9. Mashambulizi ya Urusi yaua watu wanane, maafisa wamesema

    .

    Chanzo cha picha, Roman Petushkov/Global Images Ukraine

    Watu wanane wameuawa na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa katika msururu wa ndege zisizo na rubani na makombora ya Urusi ambayo yalishambulia wilaya kadhaa za Kyiv na kuangusha jengo la ghorofa usiku kucha, maafisa wa Ukraine wamesema.

    Mvulana mwenye umri wa miaka sita na mama yake walikuwa miongoni mwa waliofariki, kwani zaidi ya maeneo kumi katika mji mkuu yalishambuliwa.

    Mlio wa sauti ya juu wa ndege zisizo na rubani za Urusi ulisikika kwa masaa mengi juu ya jiji hilo, ukikatizwa na sauti kubwa ya mara kwa mara ya shambulio la kombora.

    Mashambulizi ya Urusi yameendelea licha ya kitisho cha Rais wa Marekani Donald Trump kuweka vikwazo vikali dhidi ya Moscow ikiwa Vladimir Putin hatakubali kusitishwa kwa mapigano ifikapo tarehe 8 Agosti.

    Soma zaidi:

  10. Makumi ya raia wauawa wakitafuta chakula huko Gaza – hospitali

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Zaidi ya Wapalestina 50 wameuawa na wengine 400 kujeruhiwa walipokuwa wakisubiri chakula karibu na kivuko kaskazini mwa Gaza siku ya Jumatano, hospitali moja inasema, wakati mjumbe maalum wa Marekani Steve Witkoff akiwasili Israel.

    Picha zilionyesha majeruhi wa tukio karibu na kivuko cha Zikim wakichukuliwa kwa mikokoteni kupelekwa hospitali ya al-Shifa katika Jiji la Gaza.

    Shirika la Ulinzi la Raia la Gaza linaloendeshwa na Hamas lilisema kuwa wanajeshi wa Israel walifyatua risasi kwa umati wa watu waliokusanyika karibu na malori ya misaada.

    Jeshi la Israel lilisema wanajeshi walifyatua "risasi za onyo" lakini "halikuwa na habari kuhusu majeruhi yoyote".

    Witkoff anatarajiwa kukutana na maafisa wa Israel ambao wanafikiria kuchukua hatua dhidi ya Hamas baada ya mazungumzo ya kusitisha mapigano na kuwaachilia mateka kukwama wiki iliyopita.

    Soma zaidi:

  11. Wajumbe 2 wa vuguvugu linalojiita 'FBI' Kenya mahakamani kwa kuhusishwa na ugaidi

    g

    Chanzo cha picha, DCI

    Maafisa wa upelelezi wamemkamata na kumfikisha mahakamani Patrick Nyambaka Osoi, mwanachama mwanzilishi wa vuguvugu la Kupambana na Ukatili na Kutoadhibi makosa (FBI), wakati wa operesheni iliyoratibiwa vyema kando ya Barabara ya Lang'ata jijini Nairobi.

    Taarifa ya Ofisi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini Kenya (DCI) inasema, Osoi alikabiliwa na mashtaka chini ya sheria ya kuzuia Ugaidi, ya mwaka 2012, na kwa kuwa na bunduki, miongoni mwa makosa mengine.

    Kwa sasa anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Muthaiga jijini Nairobi huku akisubiri uamuzi wa mahakama juu ya amri za kizuizi zilizopangwa kufanyika Alhamisi.

    Katika tukio jingine, Jackson Kuria Kihara, almaarufu Cop Shakur, pia alikamatwa katika kitongoji cha Kahawa West kuhusiana na makosa hayo hayo. Wakati wa kukamatwa, alipatikana akiwa na kofia nyekunduyenye alama ya 'FBI'.

    Kihara atafikishwa mahakamani anatarajiwa kufikishwa katika Mahakama ya Kahawa leo.

  12. Idadi ya vifo ya maandamano ya kupinga gharama ya Petroli Angola yaongezeka huku madaktari wakizidiwa

    g

    Chanzo cha picha, EPA

    Haya ni wimbi kubwa la maandamano ambayo nchi hiyo imeshuhudia katika miaka ya hivi karibuni.

    Takriban watu 22, akiwemo afisa wa polisi, wameuawa na wengine 200 kujeruhiwa katika maandamano ya kupinga kupanda kwa bei ya mafuta yaliyoanza Jumatatu, Waziri wa Mambo ya Ndani Manuel Homem amesema.

    Polisi wanasema zaidi ya watu 1,200 pia wametiwa mbaroni katika kile kilichoanza kama mgomo wa madereva wa teksi kupinga kupandishwa kwa bei na kisha kushika kasi na kuwa moja ya wimbi kubwa la maandamano ambayo nchi hiyo imewahi kuyashuhudia katika miaka ya hivi karibuni.

    Biashara, pamoja na maduka makubwa, zimesalia kufungwa na watu wengi wamechagua kukaa nyumbani.

    Madaktari katika hospitali za umma katika mji mkuu, Luanda ambao hawakutaka kutajwa majina waliiambia BBC kuwa huduma za dharura zimezidiwa katika muda wa saa 24 zilizopita.

    Siku ya Jumatatu na Jumanne milio ya risasi ya hapa na pale ilisikika katika jiji lote.

    "Tumepokea waandamanaji wengi wakiwa na majeraha mabaya, ikiwa ni pamoja na majeraha mengi. Cha kusikitisha ni kwamba wengine wamefariki. Tunahofia huenda idadi ya waliofariki ikawa kubwa kuliko takwimu rasmi zinavyopendekeza," daktari mmoja alisema.

  13. Marekani yawawekea vikwazo zaidi ya watu 115, mashirika na meli zenye uhusiano na Iran

    g

    Chanzo cha picha, Reuters

    Katika mojawapo ya vikwazo vikali zaidi ilivyowekewa Iran tangu mwaka 2018, Wizara ya fedha ya Marekani imeweka zaidi ya watu na taasisi 115 zinazohusiana na sekta ya mafuta na meli ya nchi hiyo kwenye orodha yake ya vikwazo.

    Katika kujibu tangazo la vikwazo hivyo, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghai amekitaja kitendo hicho kuwa ni kiovu na cha kulaaniwa vikali.

    Mohammad Hossein Shamkhani, mtoto wa Ali Shamkhani, mshauri mkuu wa kiongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran anayesimamia mtandao wa usafiri wa baharini, pia anasemekana kuwa katika orodha hiyo.

    Marekani pia ilimuwekea vikwazo Ali Shamkhani mnamo 2020.

    Habari zinazohusiana na Ali Shamkhani, mshauri wa kisiasa wa Ayatollah Khamenei, ambaye alijeruhiwa siku ya kwanza ya shambulio la Israel dhidi ya Iran, zilivutia watu wengi.

    Sasa, kwa kumuidhinisha mwanawe, Wizara ya Marekani inasema kuwa Mohammad Hossein Shamkhani "anatumia ushawishi wa baba yake" kusafirisha mafuta, bidhaa za petroli, na mizigo mingine kutoka Iran na Urusi hadi kwa wanunuzi duniani kote.

    Kulingana Marekani, Mohammad Hossein Shamkhani anapata makumi ya mabilioni ya dola kama faida kila mwaka.

    Wizara ya Fedha ya Marekani ilitangaza kuwa tangu mwanzo wa utawala wa Donald Trump, Marekani imezidisha kampeni yake ya "mashinikizo ya juu" dhidi ya Iran, kwa kutumia "zana na uwezo" wake wote katika suala hili.

    Kwa vikwazo vya leo, idadi ya watu binafsi, mashirika na meli zenye uhusiano wa Iran au Iran zinazolengwa na vikwazo vya Marekani mwaka huu vinafikia zaidi ya 500.

    Unaweza pia kusoma:

  14. Onyo latolewa baada ya makopo ya vinywaji vya kuongeza nguvu Marekani kujazwa vodka

    h

    Chanzo cha picha, US Food & Drug Administration

    Mamlaka ya Marekani inawaonya watumiaji wa vinywaji vya kuongeza nguvu vya Celsius kuangalia mikebe yao baada ya baadhi kujazwa vodka kimakosa.

    Mamlaka ya Chakula na Dawa ya Marekani (USFDA) ilitoa onyo kuhusu kinywaji hicho cha Astro Vibe Blue Razz.

    Mchanganyiko huo ulikuja baada ya msambazaji wa vifungashio kusafirisha kimakosa makopo tupu ya Selsiasi kwa kampuni ya kutengenezea vodka High Noon, ambayo ilizijaza pombe.

    High Noon pia inakumbuka baadhi ya vifurushi vyake vya Beach Variety ambavyo vilitoka kwa njia sawa ya uzalishaji. Hakuna magonjwa au matukio mabaya ambayo yameripotiwa kwa bidhaa zilizoathiriwa, USFDA iliongeza.

    "Wateja wanashauriwa kutupa kinywaji cha nishati cha Celsius Astro Vibe, makopo ya Toleo la Sparkling Blue Razz yaliyo na misimbo ya vifurushi vilivyoathiriwa na wasitumie kilevi hicho" USFDA ilisema.

    Unaweza pia kusoma:

  15. Kupunguzwa kwa misaada kutawasukuma Wanigeria katika mikono ya wanamgambo wa Boko Haram, WFP yaonya

    h

    Chanzo cha picha, Kyla Herrmannsen / BBC

    Maelezo ya picha, Hiki ni chakula cha mwisho kwa maelfu ya watu wanalioikimbia na Boko Haram huko Gwoza

    Kupunguzwa kwa kasi kwa misaada ya kibinadamu kaskazini-mashariki mwa Nigeria kunaweza kuwa faida kwa moja ya vikundi vya wapiganaji hatari zaidi ulimwenguni, Boko Haram, mashirika ya misaada yameonya.

    Kupungua kwa ufadhili katika miezi ya hivi karibuni kumelilazimisha Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) kupunguza msaada wake, na sasa umeisha kabisa.

    "Itakuwa rahisi zaidi kwa wanamgambo kuwarubuni vijana kujiunga nao na kusababisha ukosefu wa usalama katika eneo lote," Trust Mlambo, mkuu wa operesheni katika eneo la WFP, aliiambia BBC.

    Likiwa kundi maarufu duniani kote kwa kuwateka nyara zaidi ya wasichana 200 wa shule kutoka mji wa Chibok zaidi ya muongo mmoja uliopita, Boko Haram liliwateka maelfu ya watu wakati wa uvamizi wao na kuwalazimisha zaidi ya milioni moja kutoka kwa makazi yao ya vijijini.

    Hapo awali Boko Haram lilikuwa kundi la Kiislamu la kidini lililoanzishwa mwanzoni mwa miaka ya 2000 ambalo lilikuwa linapinga elimu ya Magharibi. Iliendelea kuanzisha operesheni za kijeshi mwaka 2009 kwa lengo la kisiasa la kuunda dola ya Kiislamu, na kusababisha ghasia katika eneo lote ikiwa ni pamoja na katika nchi jirani kama vile Cameroon, Chad na Niger.

    Limeorodheshwa kuwa mojawapo ya makundi mabaya zaidi ya wanajihadi duniani, na kundi lililogawanyika liliahidi utiifu kwa kundi la Islamic State mwaka 2015.

    Unaweza pia kusoma:

  16. Canada yajiunga na Ufaransa na Uingereza katika mpango wa kulitambua taifa la Palestina

    g

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Mark Carney akitangaza mipango ya Canada ya kulitambua taifa la Palestina

    Waziri Mkuu wa Canada Mark Carney amesema Canada inapanga kulitambua taifa la Palestina mwezi Septemba, na kuwa taifa la tatu la G7 kutoa tangazo hilo katika siku za hivi karibuni.

    Carney alisema hatua hiyo inategemea mageuzi ya kidemokrasia, ikiwa ni pamoja na Mamlaka ya Palestina kufanya uchaguzi mwaka ujao bila Hamas.

    Matamshi yake yanakuja siku moja baada ya Uingereza kutangaza kulitambua taifa la Palestina mwezi Septemba isipokuwa Israel ikikubali kusitisha mapigano na masharti mengine na hii inakuja wiki moja baada ya Ufaransa kufichua mpango sawa na huo.

    Wizara ya mambo ya nje ya Israel ilipinga tangazo la Canada, na kuliita "zawadi kwa Hamas". Nchi nyingi - 147 kati ya nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa - zinalitambua rasmi taifa la Palestina.

    Carney alisema Canada italitambua rasmi taifa la Palestina katika Mkutano Mkuu ujao wa Umoja wa Mataifa.

    Alitaja kupanuka kwa makazi ya Waisraeli katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, hali mbaya ya kibinadamu huko Gaza, na mashambulizi ya tarehe 7 Oktoba 2023 dhidi ya Israel na Hamas kama sababu za mabadiliko makubwa yaliyosababisha mabadiliko makubwa katika sera za kigeni ya Canada.

    "Kiwango cha mateso ya binadamu huko Gaza hakivumiliki na kinazidi kuzorota kwa kasi," Carney aliwaambia waandishi wa habari siku ya Jumatano.

    Unaweza kusoma;

  17. Habari za asubuhi, karibu katika taarifa zetu za mubashara