Miss Universe 2019: Anasema dhana ya kuwa ngozi nyeusi sio kigezo cha urembo yapaswa kukoma

Chanzo cha picha, Getty Images
''Nilikua katika ulimwengu ambao mwanamke anayefanana na mimi, kwa rangi ya ngozi yangu na aina ya nywele zangu, anaonekana si mrembo''.
''Ninafikiri ni wakati sasa hali hiyo ikomeshwe.''
Huo ni ujumbe wa mshindi mpya wa michuano ya Miss Universe Zozibini Tunzi, kutoka Afrika Kusini.
Zaidi ya wanawake 90 kutoka duniani kote walishiriki kwenye mshindano hayo yaliyofanyika Atlanta nchini Marekani siku ya Jumapili.
Zozibini alimshinda Madison Anderson wa Puerto Rico na Aofia Aragon wa Mexico.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa Instagram ujumbe

Waliofaulu kuingia fainali ya mashindano hayo waliulizwa maswali kuhusu maada mbalimbali kama vile mazingira, maandamano na mitandao ya kijamii.
Katika swali lake la mwisho, mshiriki Zozibini mwenye miaka 26 aliulizwa kuhusu jambo gani tunapaswa kuwafundisha wasichana wa leo.
Jibu lake lilikuwa uongozi.
''Ni kitu ambacho kinakosekana kwa wasichana na wanawake kwa muda mrefu- si kwa sababu hatutaki, lakini kwa sababu jamii inavyotaka tuwe,'' alisema.
''Ninafikiri ni viumbe wenye nguvu sana duniani, na kuwa tunapaswa kupatiwa kila fursa.
''Na hicho ndicho tunachopaswa kuwafundisha mabinti wadogo.''
Washiriki wengine wakimpongeza kwa makofi Zozibini Tunzi

Chanzo cha picha, EPA
Zozibini ni mwanamke wa kwanza mweusi kushinda kwenye mashindano hayo tangu Lila Lopes aliponyakua taji hilo mwaka 2011.
Hashtag #MissUniverse ilisambaa kwenye mtandao wa Twitter na hata akapata salamu za pongezi kutoka kwa Oprah Winfrey.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1

Watu kadhaa walieleza umuhimu mkubwa wa wanawake weusi wakiwa na nywele za asili kushinda taji hilo la urembo.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 3


Chanzo cha picha, Kev Wise
Washindi wa taji la Miss Universe kutoka Afrika
Miss Universe 1999: Alishinda Mpule Keneilwe Kwelagobe kutoka nchini Botswana
Miss Universe 2011:Alishinda Leila Lopes wa Angola
Unaweza pia kutazama













