Ndege ya abiria 18 yaanguka katika mji wa Goma mashariki mwa DR Congo

Chanzo cha picha, @ELIEZAIREUSHIN
Takriban watu 24 wanaaminika kufariki baada ya ndege waliokuwa wakiabiri kuangukia katika mji wa Goma mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Gavana wa jimbo la Kivu kaskazini Nzanzu Kasivita Carly amesema kwamba watu wamefariki lakini hakutoa idadi kamili .
Ndege hiyo ilianguka juu ya nyumba katika eneo jirani la Mapendo baada ya kushindwa kupaa katika uwanja wa ndege wa mji huo , aliongezea.
Wakaazi wa eneo hilo ni miongoni mwa waathiriwa wa ajali hiyo, kulingana na vyombo vya habari vya eneo hilo.
Ndege hiyo aina ya Doenier 228 ilikuwa ikimilikiwa na kampuni binafsi ya Busy Bee.

Chanzo cha picha, Reuters
Ilitarajiwa kuelekea Beni yapata kilomita 350 kutoka kaskazini mwa Goma, wakati ilipoanguka dakika moja baada ya kupaa kulingana na chanzo kimoja katika mji wa Goma kilichozungumza na BBC.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
Ajali za ndege hutokea mara kwa mara nchini DR Congo , kutokana na viwango vya chini vya usalama na kutorekebishwa kwa ndege hizo.
Ndege zote za kibiashara za taifa hilo zimepigwa marufuku kufanya biashara katika Muungano wa Ulaya.














