Ubakaji wa mtoto wa miaka 6 ulioitamausha India

Locals carry the body of the six-year-old who was brutally raped and murdered

Chanzo cha picha, Manoj Dhaka

Maelezo ya picha, Ubakaji wa mtoto wa miaka 6 ulioitamausha India

Polisi nchini India wanawahoji watu kadhaa kufuatia kisa cha ukatili cha ubakaji wa mtoto wa miaka sita katika jimbo la kaskazini mwa nchi la Haryana.

Mwili wake ulipatikana Jumapili karibu na kwenye nyumba yao ambapo alidaiwa kutekwa usiku wa tarehe 8 mwezi Disemba.

Kiwango cha majeraha ya mtoto huyo kimewatamausha watu nchini India,

Mamayake mtoto huyo aliiambia BBC kuwa kile wanataka ni haki.

Locals gathered to protest around the girl's body as the family refused to cremate her

Chanzo cha picha, Manoj Dhaka

Maelezo ya picha, Ubakaji wa mtoto wa miaka 6 ulioitamausha India

"Yamepita masaa 24 na bado polisi hajamshika yeyote," alisema.

Polisi wamewakamata watu watatuakutoja kwa familia ya mume wake kuhojiwa lakini hakuna mtu alishikwa hadi sasa.

Serikali imebunia kikosi cha uchunguzi kufuatia shinikizo kutoka kwa mamlaka ili kuwakamata wale waliotekeleza kitendo hicho.

Wenyeji wakiwemo wanaharakati na viongozi wa kisiasa wamekusanyika katika kijiji hicho kuandamana.