Tetesi za soka Ulaya Alhamisi 27.06.2019: Maguire, Vieira, Gerrard, Arteta, Fernandes, Pogba, Cancelo

Manchester United imejiondoa katika harakati ya kutaka kumsaini beki wa Leicester na Uingereza Harry Maguire baada ya kuambiwa kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 atagharimu £100m. (Mirror)
Mkufunzi wa klabu ya Nice nchini Ufaransa Patrick Vieira, 43, Mkufunzi wa klabu ya Rangers Steven Gerrard, 39, kocha wa Manchester City Mikel Arteta, 37, wameorodheshwa miongoni mwa wakufunzi wanaotarajiwa kumrithi Rafael Benitez. (Telegraph)
Raia wa Uhispania Mikel Arteta ameungwa mkono kuchukua ukufunzi wa klabu ya Manchester City wakati kocha Pep Guardiola atakapoondoka katika klabu hiyo. (Evening Standard)

Mkufunzi wa klabu ya Burnley Sean Dyche pia analengwa na Newcastle lakini the Magpies watalazimika kuwalipa Burnley £10m kama fidia. (Daily Mail)
Manchester United itakutana na ajenti wa kiungo wa kati wa Portugal Bruno Fernandes, 24, ili kujaribu kumrai kuhamia katika klabu hiyo kwa dau la £70m kutoka klabu ya Sporting Lisbon. (O Jogo, via Talksport)
Juventus imeitaka kampuni ya vifaa vya michezo Adidas kuisaidia kifedha ili kuweza kumsaini kiungo wa kati wa Manchester United na Ufaransa Paul Pogba, 26. (Corriere dello Sport - in Italian)

Manchester City iko katika mzungumzo na Juventus kuhusu usajili wa beki wa kulia wa Ureno Joao Cancelo. (Tuttomercato, via Star)
Kiungo wa kati wa Arsenal na Uruguay Lucas Torreira, 23, anasema kuwa AC Milan haijawasiliana naye kuhusu uhamisho katika klabu hiyo ya Serie A. (Talksport)
Bayern Munich imefanya mazungumzo na Paris St-Germain na ajenti wa mshambuliaji wa Ufaransa Ousmane Dembele kuhusu uhamisho wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22. (Mirror)

Beki wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 19 Sepp van den Berg, anatarajiwa kujiunga na Liverpool kutoka kwa klabu ya PEC Zwolle. (Evening Standard)
Beki wa klabu ya Huddersfield Town na Uingereza Tommy Smith, 27, ananyatiwa na Stoke City pamoja na mabingwa wa ligi ya Uskochi Celtic. (Huddersfield Examiner)
Reading wanamnyatia winga wa Brazil Wenderson Galeno, 21, kwa mkopo kutoka Porto.(Futebol365)
TETESI ZA SOKA JUMATANO

Barcelona inakaribia kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Ufaransa na Atletico Madrid Antoine Griezmann kwa dau la £107m baada ya kifungu cha sheria cha uhamisho wake kuanza kufanya kazi tarehe mosi mwezi Julai (Telegraph)
Tottenham inakaribia kumsajili kiungo wa kati wa Lyon na Ufaransa Tanguy Ndombele, 22, kwa dau litakalovunja rekodi £60m.
Ndombele aliichezea Lyon mechi 34 ,msimu uliopita huku ikifuzu katika mashindano ya ligi ya mabingwa baada ya kumaliza katika nafasi ya tatu ya jedwali la ligi ya daraja la kwanza.. (Sun)

Spurs pia inakaribia kumsaini winga wa klabu ya Leeds United Jack Clarke 18, kwa dau la £8.5m. Clarke aliichezea klabu hiyo mara 22 msimu wa 2018-19. (Sky Sports)
Manchester United wanataka kumsaini mshambuliaji wa Sevilla na Ufaransa Wissam Ben Yedder, 28, na wataathiri kifungu cha sheria cha uhamisho wake cha £35.8m. (ABC de Sevilla)
Manchester United ina hamu ya kumsajili mshambuliaji wa Ufaransa ,15, Mathis Rayan Cherki anayeichezea klabu ya Lyon na ambaye anazivutia klabu kama vile Real Madrid, Juventus, Barcelona na Bayern Munich. (Telegraph)

Chanzo cha picha, Getty Images
Mlinda lango wa Liverpool na Ubelgiji Simon Mignolet, 31, ananyatiwa na klabu ya Crystal Palace. Mwewe hao wa Uingereza wameandaa dau la £8m kumnunua Mignolet, ambaye amesalia na kandarasi ya miaka miwili .. (Evening Standard)
Hatahivyo klabu hiyo ya Anfield haiko tayari kumuuza Mignolet kwenda Palace to Palace na itamuachilia kipa huyo iwapo kitita hicho kitakubalika. (ESPN)
Mshambuliaji wa Liverpool Divock Origi, ambaye alifunga katika ushindi wa Liverpool dhidi ya Tottenham katika fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya anasakwa na klabu ya Real Betis, huku klabu hiyo ya Uhispania ikiandaa dau la £10m kumnunua mchezaji huyo wa Ubelgiji . (BeIn Sports - in French)

Mshambuliaji wa West Ham na Mexico Javier Hernandez, 31,ana mipango ya kuondoka na kuelekea Uhispania na badala yake wana nyundo hao wameamua kumsajili mshambuliaji wa Uruguay na Celta Vigo Maxi Gomez. (Evening Standard)
Leicester imeshinda harakati za kumsaini beki wa klabu ya Luton na Uingereza James Justin kwa dau la £8m ikiwashinda Aston Villa na mabingwa wa ligi ya Uskochi kupata saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21. (Mirror)

Mlinda lango wa zamani wa Itali Gianluigi Buffon, 41, yuko katika hatua za mwisho za mazungumzo ya kurudi katika klabu ya Juventus kutoka PSG ambako alikua katika kandarasi ya mwaka mmoja kama mkurugenzi wa klabu hiyo. (Sky Italia via Football Italia)
Winga wa itali na Roma Stephan El Shaarawy, 26, amekubali kujiunga na klabu ya China ya Shanghai Shenhua kwa dau la £16.11m . (Il Tempo)

Napoli huenda ikaanza kuitumia jezi nambari 10 ya aliyekuwa nyota wa Argentina Diego Maradona wakijaribu kumrai mshambuliaji wa Real Madrid na Colombia James Rodriguez kujiunga na timu hiyo. (Daily Mail)
Mshambuliaji wa klabu ya Reading na Gambia Mo Barrow ananyatiwa na klabu ya Montpellier na Rennes.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ambaye aliwahi kuichezea ya Swansea City player ya Uingereza pia ananyatiwa na klabu kadhaa za Uturuki na sasa anataka kuondoka katika wafalme hao baada ya miaka miwilii (getreading)
TETESI ZA JUMANNE

Paris St-Germain wameipatia ofa Man United ya kubadilishana na mshambuliaji wa Brazil Neymar, 27, kwa kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba. (Independent)
Arsenal itahitaji nusu ya fedha zao ilizotengewa dirisha la uhamisho kumnunua beki wa Celtic raia wa Uskochi Kierna Tierney mwenye umri wa miaka 22 huku mchezaji huyo akiwa na thamani ya £25m kutoka kwa mabingwa hao wa Uskochi.. (Telegraph)
Hatma ya kiungo wa kati wa Croatia Mateo Kovacic, 25, katika klabu ya Chelsea haijulikani huku mkopo wake katika klabu ya Real Madrid ukitarajiwa kukamilika tarehe mosi mwezi Julai. Klabu hiyo ya Stamford Bridge bado haijamuongezea kandarasi. (Goal)

Chanzo cha picha, TF-Images
United itaimarisha hamu yao ya kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund na Uingereza Jadon Sancho, 19, iwapo watamuuza Pogba. (Sun)
Neymar hatoruhusiwa kurudi katika klabu yake ya zamani Barcelona kutoka PSG hadi atakapoomba msamaha kwa mabingwa hao wa Uhispania na mashabiki wake na kukubali mshahara wake kupunguzwa (El Mundo - in Spanish)
Real Madrid haitakubali maombi ya chini ya 47.7m kumuuza kiungo wa kati wa Uhispania Dani Ceballos, ambaye amevutia hamu ya klabu ya Tottenham nchini Uingereza. (AS- in Spanish)

Chanzo cha picha, Reuters
Spurs inachunguza kinda wa Denmark Andreas Skov Olsen, ambaye anaichezea klabu ya FC Nordsjaelland na ana thamani ya £15m. (Mirror)
Arsenal wanakataa ofa kutoka AC Milan kumuuza kiungo wa kati wa Uruguay Lucas Torreira, 23. (Mirror)
The Gunners wana hamu ya kumsajili winga wa klabu ya Dalian Yifang Yannick Carrasco, lakini bado hawajawasilisha ofa yoyote kwa mchezaji huyo wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 25 (Football.London)

Chanzo cha picha, Getty Images
Mkufunzi mpya wa Juventus Maurizio Sarri ana hamu ya kumsajili beki wa kulia wa Tottenham Kieran Trippier, 28, kama mchezaji ambaye anamlenga sana lakini anakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa Napoli ambao tayari wamewasiliana na mchezaji huyo.. (Mirror)
Mshambuliaji wa Real Madrid na Colombia James Rodriguez, ambaye alihudumu misimu miwili kwa mkopo akiichezea Bayern Munich, hana uhakika iwapo atasalia katika klabu hiyo ya Bernabeu msimu ujao. (Marca)
Newcastle United haina haja na mshambuliaji wa West Brom na Venezuela Salomon Rondon - ambaye alihudumu msimu uliopita akiichezea klabu hiyo ya ligi kuu ya Uingereza - licha ya uamuzi wa mkufunzi Rafael Benitez kuondoka katika klabu hiyo. (Star)

Aston Villa inataka kumnunua beki wa klabu ya Luton Town na Uingereza James Justin huku klabu ya Leicester pia ikiwa na hamu ya mchezaji huyo. (Birmingham Chronicle)
Beki wa klabu ya Manchester United na Uingereza Axel Tuanzebe, 21, ambaye alihudumu msimu uliopita kwa mkopo katika klabu ya Aston Villa anataka hakikisho kuhusu hatma yake katika klabu hiyo ya Old Trafford. (Sun)
Mchezaji anayelengwa na Arsenal Dominik Szoboszlai, 18, anafikiria kuondoka katika klabu ya Red Bull Salzburg, huku Barcelona na Borussia Dortmund zikimnyatia mchezaji huyo wa Hungary. (Football.London)
TETESI JUMATATU

Mchezaji wa Leicester City na Uingereza Harry Maguire, 26, anatarajiwa kuwa beki ghali zaidi duniani wiki hii wakati atakapojiunga na Manchester City kwa dau la £80m baada ya kukataa kujiunga na Manchester United. (Mirror)
Liverpool na Manchester United watapigania saini ya mchezaji wa Uhispania na Real Betis beki wa kushoto Junior Firpo, 22. (Marca)
Manchester United watatumia kifungo cha sheria ya kumuongezea miezi 12 Marcus Rashford katika kandarasi yake uku kukiwa na hofu kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 huenda akaondoka man United wakati mkataba wake utakapokamilika mwisho wa msimu ujao. (Sun)


Chanzo cha picha, Getty Images
Inter Milan haijaafikia kiwango cha £22.3m kumnunua mshambuliaji wa Manchester United na Ubelgiji Romelu Lukaku, 26. (La Gazzetta dello Sport, via Football Italia)
Newcastle United inatarajiwa kufanya majaribio ya mwisho kumrai mkufunzi Rafael Benitez kuongeza kandarasi yake.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 59 , ambaye kandarasi yake inakamilika mwisho wa mwezi Juni ameripotiwa kupata kazi nchini China. (Evening Chronicle)

Real Betis wana hamu ya kumsajili mshambuliaji wa Liverpool na Ubelgiji Divock Origi, 24. (Estadio Deportivo, in Spanish)
Klabu ya Brighton imekubali kumsajili winga wa Ubelgiji Leandro Trossard, 24, kutoka Genk kwa dau la £18m. (Sky Sports)
Mchezaji anayelengwa na Liverpool Nicolas Pepe anawaniwa na InterMilan kwa dau la £80m.

Chanzo cha picha, Getty Images
Timu hiyo ya Ligi ya Serie A Inter Milan ni miongoni mwa klabu nyingi zilizo na hamu ya kumsajili winga huyo mwenye umri wa miaka 24 kutoka Lille na Ivory Coast . (L'Equipe, in French)
Mkufunzi wa Man United Ole Gunnar Solskjaer amewasilisha ombi la kibinafsi kwa afisa mkuu mtendaji -mwenyekiti Ed Woodward kuharakisha ili kumsajili kiungo wa kati wa Lisbon na Portugal Bruno Fernandes , 24, (Record, in Portuguese, subscription required)

Wakati huohuo Manchester United wako katika harakati za kumsaini winga wa Uhispania mwenye umri wa miaka 16 Mateo Mejia kwa dau la £600,000 kutoka klabu ya Real Zaragoza. (Sun)
Arsenal inafikiria kumuuza Lucas Torriera, 23, baada ya AC Milan kuwasilisha ombi lao la kwanza kwa kiungo huyo wa Uruguay. (Sport Mediaset, in Italian)
Mkufunzi wa Leicester Brendan Rodgers ameambiwa kwamba anapoteza wakati kujaribu kumsaini kiungo wa kati wa Uskochi mwenye umri wa miaka 26 Callum McGregor kutoka klabu yake ya zamani Celtic. (Scottish Daily Mail)

Klabu ya Uholanzi ya AZ Alkmaar imethibitisha mazungumzo na kiungo wa kati wa Southampton Jordy Clasie, 27. (Daily Echo)
Burnley wamemwambia beki Ben Gibson,26, anaweza kuondoka mwisho wa msimu huu.
Anston Villa ambao wamepanda daraja la ligi ya Premier pamoja na Sheffield United ni miongoni mwa kundi la klabu zilizo na hamu ya kumsaini mchezaji huyo wa Uingereza kwa dau la £15m. (Teamtalk)
Aston Villa wanatarajiwa kuanza mazungumzo ya kumsajili beki wa Bournemouth Tyrone Mings,26. Mchezaji huyo wa Uingereza alikuwa kiungo muhimu katika kupandishwa daraja kwa Villa wakati alipoichezea klabu hiyo kwa mkopo msimu uliopita.. (Birmingham Mail)
TETESI ZA SOKA JUMAPILI

Chanzo cha picha, Getty Images
Inter Milan wanataka kumsaini mshambuliaji wa Manchester United Romelu Lukaku, 26, lakini watalazimika kumuuza mshambuliaji wao wa sasa Muargentina Mauro Icardi,26 kufadhili mkataba wa Lukaku. (Guardian)
Real Madrid wanampango wa kumnunua Paul Pogba kutoka Manchester United msimu huu wa joto kabla ya kumsaini mchezaji nyota wa Tottenham na Denmark Christian Eriksen, 27. (Goal)
Tottenham watamchukua winga wa Uhispania wa miaka 22 Marco Asensio kama sehemu ya makubaliano ya uhamisho wa Eriksen kwenda Madrid . (Sun)
Kocha wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer ameiambia klabu hiyo imuuza Pogba kwa klabu itakayoweka dau kubwa zaidi, japo Juventus wameonesha nia ya kutaka kumnunua. (Star)

Chanzo cha picha, Reuters
Tottenham inatarajia Juventus itaweka dau la kumnunua beki wa kulia Kieran Trippier, 28, na wako tayari kumuuza kiungo huyo wa kimataifa kwa karibupauni milioni 25. (Telegraph)
Paris St-Germain wameiambia Barcelona kuwa hawamuuzi Neymar, 27 kwa udi na uvumba. (Mail)
Real Madrid wanampango wa kusaini Ian Kylian Mbappe,26 kutoka PSG msimu ujao lakini wanataka mchezaji huyo raia wa Ufaransa kutoa ombi la kutaka uhamisho. (AS)

Chanzo cha picha, Reuters
Atletico Madrid wanamtaka beki wa Arsenal Mhispania Hector Bellerin, 24, na wako tayari kumwachilia winga Vitolo, 29, kama sehemu ya mkataba wa usajili wake. (Telegraph)
Chelsea hawajaamua kumuuza mlinzi wao Mfaransa Kurt Zouma, 24, kwa Everton hadi watakapopata kocha mpya. (Star)
The Blues wanajiandaa kuilipa Derby pauni milioni 4 zinazohitajika kutimiza masharti ya mkataba wa Frank Lampard kabla hawajakamilisha mchakato wa kumuajiri kama kocha wao mpya wiki ijayo. (ESPN)
Chelsea wamempatia kipa Petr Cech la kiufundi na mshauri wa michezo wakiwa na matumaini kuwa atashirikiana kwa karibu na Lampard. (Guardian)

Chanzo cha picha, AFP
Klabu ya Shanghai Greenland Shenhua kutoka China imetoa ofa ya pauni milioni 17.8 kumnunua Willian, 30, lakini mchezaji huyo wa Brazil huenda asikubali kujiunga nao kwasababu bado anataka kusalia Chelsea. (UOL Esporte, via Metro)
Mpango wa Arsenal wa kumnunua winga wa Ubelgiji Yannick Carrasco au mshambuliaji wa Bournemouth Ryan na Uskochi Fraser huenda umekwama. (Evening Standard)
Meneja mpya wa Juventus Maurizio Sarri amesema hana mpango wa kumsaini kiungo wa kati wa Italia Jorginho, 27, kutoka Chelsea. (Sun)

Chanzo cha picha, Getty Images

Tetesi Bora Ijumaa
Juhudi za kocha Ole Gunnar Solskjaer kuimarisha kikosi chake huenda zikagonga mwamba kwa sababu Manchester United ni klabu ambayo hutoa ofa ya chini kwa wachezaji wanaotaka kuwasajili. (Evening Standard)
Solskjaer anataka kumuuza kiungo wa kati wa Man Utd Mfaransa Paul Pogba, 26, bada ya kufahamishwa kuwa ana pauni milioni 100 ya kuwasajili wachezaji wapya msimu huu. (Star)

Chanzo cha picha, Reuters
Mchezaji nyota wa kimataifa wa Brazil Neymar, 27, hana mpango wa kuchezea tena Paris St-Germain. (Sport - in Spanish)
Real Madrid wameweka dau la euro milioni 130 kumnunua Neymar, kutoka PSG, mshambuliaji wa Wales Gareth Bale, 29, au mshambuliaji wa Colombia James Rodriguez, 27. (Mundo Deportivo - in Spanish)
Manchester City wanapigiwa upatu kuipiku Man Utd katika usajili wa Harry Maguire, 26, kutoka Leicester kwa kima cha pauni milioni 65 baada ya kiungo huyo wa England kupita vipimo vya matibabu. (Star)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kiungo wa kati wa Atletico Madrid Mhispania Rodri, ameamua kujiunga na Man City badala ya Bayern Munich na kuhamia City kawa malipo ua £62m. (Kicker - in German)
Everton wameanza maungumzo na Chelsea kuhusu usajili wa Kurt Zouma kwa mkataba wa kudumu baada ya mlinzi huyo wa Ufaransa, 24, kucheza Goodison Park msimu uliopita kwa mkopo katika. (Telegraph)












