Uingereza yakodi ndege kuwaondoa raia wake nchini Oman
Taarifa tulizopokea muda mfupi uliopita zinasema kuwa serikali ya Uingereza imekodisha ndege ya kibiashara kutoka Oman kuwasaidia raia wa Uingereza wanaotaka kuondoka Mashariki ya Kati.
Ndege inatarajiwa kuondoka mjini Muscat leotarehe 4 Machi saa tano usiku saa za ndani (19:00 GMT), na itawapa kipaumbele watu walio hatarini zaidi.
Ofisi ya Mambo ya Nje inasema raia wa Uingereza ambao wamejiandikisha kuwa wapo UAE na kwa sasa wako Oman wanapaswa kujaza fomu maalumu haraka iwezekanavyo, ikiwa wangependa kuabiri ndege hiyo.
Ofisi hiyo aidha imeomba watu kutofika uwanja wa ndege hadi watakapofahamishwa na Ofisi ya Mambo ya nje.
Inaongeza kuwa itaendelea kushirikiana na mashirika ya ndege kutafuta njia zaidi za kurejea watu nyumbani Uingereza.

