Maelezo ya picha, Uzalendo wa kikabila umezua mtafaruku baina ya Wakenya
Wakati Kenya inapojiandaa kwa uchaguzi mkuu wa Agosti 9, mwandishi wa BBC Dickens Olewe anaandika kwamba migawanyiko wa kikabila kwa muda mrefu imekuwa jinamizi katika siasa za taifa - ingawa kuna ishara hali hii sasa inaweza kubadilika.
Asubuhi yenye baridi kali tarehe 20 Januari 1994 nilikaribishwa darasani kwa dhihaka.
Sikumbuki mengi yaliyosemwa lakini maneno haya yamesalia katika kumbukumbu yangu.
Jaramogi Oginga Odinga, makamu wa rais wa kwanza wa Kenya ambaye baadaye alikuwa kigogo wa siasa za upinzani, alikuwa amefariki.
Licha ya kwamba tulikuwa katika shule ya msingi, sote tulikuwa na uelewa kuhusu siasa zinazoegemea misingi ya kikabila, kwa hivyo mwanafunzi mwenzangu alijua kifo hicho kilikuwa na athari kubwa ya kisiasa kwa jamii ya Wajaluo.
Kejeli za kikabila zilikuwa jambo la kawaida katika viwanja vya michezo vya shule na hata madarasani, ambapo baadhi ya walimu walitumia dhana potofu kusifia au kukemea tabia za wanafunzi.
Hii ilionekana, na bado inaonekana kama ucheshi usio na madhara, lakini wakati mwingine hubadilika kuwa mbaya.
Wakati mwingine wa kushangaza ulikuja miaka minane baadaye wakati msichana mwenye umri wa miaka minne mwenye kujiamini aliponijia katika siku yangu ya kwanza ya kujitolea katika shirika la kusaidia familia maskini jijini Nairobi, na kuuliza swali moja kwa moja kwa Kiswahili: "Wewe ni kabila gani?"
Hakufurahishwa na jibu langu, hasa kwa sababu baadaye niligundua kwamba kabila langu lilikuwa sehemu ya mjadala mkali na wenzake - maslahi yao ambayo yanawezekana yalichochewa na mazungumzo ya kisiasa ya wakati huo.
Udadisi wa utotoni ulikuwa mzuri, lakini nilihisi usumbufu. Maadili ya kijamii yalinifundisha kuchukia maswali kama hayo, haswa yanapowekwa wazi. Pia nilikuwa na wasiwasi jibu langu lingemaanisha nini kwake.
Siasa za Kenya zimetawaliwa na ushindani kati ya makabila yake zaidi ya 40, lakini ni makali zaidi kati ya makabila makubwa zaidi.
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Kenya ilipata uhuru wake kutoka kwa Uingereza mwaka 1960
Wanasiasa mara nyingi hutumia chuki za kihistoria na tofauti za kitamaduni kuchochea vurugu ili waweze kushinda uchaguzi.
Mkakati huu wa kipuzi ni wa zamani na matokeo yake ya kusikitisha yanaendelea kushuhudiwa kote duniani.
Nchini Kenya, ukabila umetumika kwa njia ya upendeleo - wakati mwingine ndiyo sifa pekee inayozingatiwa kwa kazi, kura katika uchaguzi, au hata kupata upendeleo wa kawaida kutoka kwa mtu aliye na mamlaka.
Imetumiwa kama silaha ya kuwadhalilisha na kuwahangaisha wengine - hali inayozaa fikra ya kuzingirwa kwa wale wanaobeba mzigo huo, na hisia ya kustahiki miongoni mwa wanaonufaika nayo.
Siasa kwa hivyo inakua kigezo muhimu, badala ya kushughulikia masuala muhimu ambyo yana athari ya moja kwa moja kwa wananchi.
Kenya ilishuhudia ghasia mbaya za kikabila kufuatia mzozo wa uchaguzi wa mwaka 2007, wakati zaidi ya watu 1,500 waliuawa, mamia ya wengine kujeruhiwa na takriban watu 600,000 kulazimika kutoroka majumbani mwao.
Vurugu hizo huenda ziliathiri Kenya vibaya tangu uhuru.
Nchi ambayo kwa kiwango kikubwa ilikuwa na amani, na hata kutoa hifadhi kwa maelfu ya wakimbizi kutoka nchi tofauti barani, ilijigeukia yenyewe. Maumivu ya wakati huo bado yanaendelea.
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Wati wengi bado wanalilia haki kufuatia vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi wa mwaka 2007
akati wa uchaguzi huu, baadhi ya familia zinapanga kuhamia katika maeneo yalio na watu wengi wa kabila lao ili kuepuka kudhulumiwa, ilhali wanandoa wa makabila mchanganyiko mara nyingi hukabiliana na changamoto kubwa kuamua ni wapi pangekuwa salama zaidi.
"Kenya ina historia ya kusikitisha ya uhasama ambao haujawahi kusuluhishwa, yapata miaka 50, na bado huchochea ghasia na wanasiasa wamekuwa wazua hofu kati ya jamii," Sam Kona, kamishna katika Tume ya Uwiano na Utangamano wa Kitaifa (NCIC), aliambia BBC.
"Watu hawaoni ukweli kwamba haya ni mashindano ya kugombea madaraka kati ya wasomi, na mara yanapoisha, wasomi wanatangamano bila kujali ikiwa walishinda au la," aliongeza.
Bw Kona alisema mivutano miongoni mwa jamii katika kaunti sita ambazo NCIC imezitaja kuwa maeneo hatari katika uchaguzi ujao ni kwa sababu ya "kukosa fursa za kupatanisha".
Alidokeza kuwa Kenya ilipitisha katiba mpya mwaka wa 2010, na kuunda majimbo 47 - na magavana wao - ili kukomesha kadhia ya mshindi-kuchukua-yote.
Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?
Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya
Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake
Raila Amollo Odinga
Muungano wa Azimio la Umoja
Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.
William Samoei Ruto
Muungano wa Kenya Kwanza
Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC
George Wajackoyah
Chama cha Roots
Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito
David Mwaure Waihiga
Chama cha Agano
David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
Kupambana na ufisadi uliokithiri.
kuunda nafasi za ajira.
Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.
Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa
Iliahidi kuwa majimbo yote yataangaziwa kwa usawa, na yatapokea kiasi cha haja cha mgao wa bajeti ya kitaifa kupanga maendeleo yao wenyeweili kuepusha hitaji la vikundi tofauti kushindania kwa rasilimali.
"Cha kusikitisha ni kwamba baadhi ya Wakenya bado wanaona urais kuwa chanzo kikuu cha mamlaka - hali inayosababisha mvutano," Bw Kona alisema, akiongeza kuwa NCIC imeimarisha juhudi za kuendeleza amani katika maeneo yanayoweza kukumbwa na ghasia.
Mtaalamu wa masuala ya utawala John Githongo alilazimika kutoroka nchini mwaka wa 2005 kwa sababu alichukuliwa kuwa msaliti na baadhi ya watu wa jamii yake ya Wakikuyu baada ya kufichua kashfa kubwa ya ufisadi katika utawala wa Rais wa wakati huo hayati Mwai Kibaki, Mkikuyu mwenzake.
Aliiambia BBC kwamba uhamasishaji wa kikabila haukuonekana wazi katika kampeni hii ya uchaguzi, haswa kwa sababu Naibu Rais William Ruto ameufanya kama mchuano kati ya "familia za kikabila" na "wanaharakati".
Anamshirikisha mpinzani wake mkuu, Raila Odinga, mwanasiasa mkongwe wa upinzani na mtoto wa makamu wa kwanza wa rais wa Kenya, katika kundi la zamani, pamoja na Rais Uhuru Kenyatta, mtoto wa rais wa kwanza. Huku akijionyesha kama bingwa wa "hustlers" - jina linalohusishwa na Wakenya maskini.
Bw Odinga amekosoa utumiaji wa neno hilo na anachukulia kama jaribio la kugawanya Wakenya kulingana na matabaka, na ameelekeza kampeni yake katika ujumbe wa umoja.
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Wagombea wawili wakuu wa urais wamekuwa na miungano inayobadilika kila mara
Lakini katika mabadiliko makubwa kutoka kwa kampeni za awali, wagombeaji wakuu hao wawili wamejibizana kuhusu sera zao za kiuchumi na kijamii.
Hili halishangazi kwani uchaguzi huu unakuja katikati ya mzozo wa gharama ya maisha, uliozidishwa na ukosefu mkubwa wa ajira na deni kubwa la taifa.
Katika hatua ya kuingilia kati hali hiyo wiki chache kabla ya uchaguzi, serikali ya Rais Kenyatta ilitangaza kuwa unga wa mahindi - unaotumiwa kutengeneza chakula kikuu nchini, ugali - utapewa ruzuku ili kupunguza bei yake.
Bw Ruto anachukulia hatua hiyo kama jaribio la kuimarisha nafasi ya Bw Odinga katika uchaguzi huo.
Bw Kenyatta anamuunga mkono Bw Odinga katika uchaguzi huu , ingawa Bw Ruto ni naibu wake.