Maelezo ya picha, William Ruto na Uhuru kenyatta wakati wa kampeni za uchaguzi wa 2013Maelezo kuhusu taarifa
Author, Alutalala Mukhwana
Nafasi, Mchambuzi Kenya
Mwaka wa 2013, tarehe 4 mwezi Machi , serikali mpya ya Jubilee, maarufu "Uhuruto ", ilichukua mamlaka baada ya uchaguzi mkuu.
Utawala huo mpya Uhuru Kenyatta pamoja naye Naibu Rais William Ruto, uliwapa matumaini chungu nzima wafuasi wao kwamba maisha ya Wakenya yangebadilika kuwa bora zaidi.
Wao Uhuru na mwenzake Wiilliam Ruto walionyesha ukuruba mkubwa hadharani na hilo likatia shani uhusiano wao na kuwaongezea matumaini maradufu Wakenya kuwa maisha yao yangelikuwa bora zaidi.
Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?
Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya
Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake
Raila Amollo Odinga
Muungano wa Azimio la Umoja
Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.
William Samoei Ruto
Muungano wa Kenya Kwanza
Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC
George Wajackoyah
Chama cha Roots
Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito
David Mwaure Waihiga
Chama cha Agano
David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
Kupambana na ufisadi uliokithiri.
kuunda nafasi za ajira.
Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.
Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa
Kabla ya mwaka huo, kwa miaka mitatu mtawalia iliyotangulia, uchumi wa Kenya ulikua kwa viwango vya asilima 5.8,4.4 na 4.5.
Ahadi za serikali ya Jubille kwa Wakenya
Rais Kenyatta akihutubia wabunge Aprili 16 mwaka wa 2013, alianisha, ahadi za serikali yake ifuatavyo: Uongozi ulio wa haki, ukweli na uwazi, kulinda na kutetea haki na uhuru wa raia, kupambana na kumaliza ufisadi, kutekeleza na kufanikisha ugatuzi ili kutimiza katiba mpya, kazi milioni moja kwa vijana kila mwaka, uwajibikaji katika utendakazi kwa umma, barabara za lami pamoja na kusambaza nguvu za umeme na huduma za maji kwa raia wote.
Idadi kubwa ya raia wa Kenya ni vijana walio chini ya umri wa miaka thelathini na mitano, nao waliahidiwa viwanja kumi na sita kote nchini katika nyanja ya michezo, kando na nafasi za kazi milioni moja kila mwaka.
Je serikali ilifanikiwa kutekeleza ahadi zake kwa Wakenya?
Chambilecho wahenga, ahadi ni deni, na dawa yake ni kulilipa. Je, serikakali ya Jubilee, kwa hatamu zote mbili sasa, imelipia ahadi zake? Je, kupigwa kumbo Naibu Rais William Ruto, kumeadhiri vipi kulipwa au kulipwa deni hili.?
Baada ya hatamu ya kwanza, mwaka wa 2017 serikali ya Jubilee ilirejeshwa mamlakani kwa awamu ya pili. Mara hii, serikali ikaahidi kwamba sasa ajenda zake zingekuwa nne: Chakula tosha kwa raia wake, nyumba na makazi kwa bei nafuu, viwanda na mwisho matibabu kwa wote kwa bei nafuu.
Maelezo ya picha, William Ruto na Uhuru kenyatta wakati wa kampeni za uchaguzi wa 2013
Kwa kupunguza ajenda yake, ni ishara tosha kwamba serikali ilikuwa imeshindwa kutimiza ahadi za mwaka 2013? Mathalan: Nafasi za kazi milioni moja hazikupatikana, madai ya visa vya ufisadi bado yaliripotiwa hata kwa viwango vikubwa zaidi kama vile Eurobond, sakata ya Afya House, na kadhalika.
Viwango vya riba viliruka juu zaidi hivi kwamba raia wamekuwa wakitatizika kukopa mikopo ya kujiendeleza kibiashara. Deni la umma hivi sasa limeruka hadi trilioni 8.02 ikilinganishwa na trilioni 6.7 mwezi Juni 2013 miezi mitatu tu baada ya Jubilee kuchukua usukani.
Kufikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
Elimu Bure kwa wote.
Huduma ya afya bora kwa wote.
Uchumi
Kukuza sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi na uchumi wa bluu hadi asilimia 30 ya Pato la Taifa.
Kuza bidhaa za "Zilizotengezwa Kenya" kwa kusaidia ukuaji wa biashara ndogo ndogo na za kati.
Mpango wa "Kaunti Moja, Bidhaa Moja" kutegemea utengenezaji kama injini ya uundaji wa utajiri na ajira.
Ufisadi
Kuboresha kwa haraka mamlaka ya kisheria na kiutawala.
Kuongeza kasi ya kurejesha mapato ya rushwa na uwepo wa fedha haramu.
Kutovumilia rushwa.
Madeni
Kupunguza kasi ya ulimbikizaji wa madeni.
Boresha sera za usimamizi wa madeni.
Kuendeleza mazungumzo ya msamaha wa madeni.
Ajira
Kutumia vizuri idadi kubwa ya vijana kwa ustawi
Kuboresha tija katika sekta ya viwanda na kusaidia uzalishaji wa ajira katika sekta hiyo.
Wekeza katika teknolojia zinazoibukia ambazo zitatoa fursa za ajira kwa vijana wa Kenya.
Kawi
Punguza gharama ya umeme.
Tathmini ushuru na kodi za bidhaa za petroli.
Kuongeze utafutaji wa mafuta na gesi kwenye nchi kavu na baharini.
Afya
Huduma ya afya bora kwa wote.
Kukuza uzalishaji wa ndani wa dawa na pembejeo nyingine zinazohusiana na afya.
Kuboresha mazingira ya kazi na malipo ya wataalamu wa afya.
Uhalifu na usalama
Kuhakikisha utekelezaji madhubuti wa mageuzi ya polisi.
Kuwafunza angalau maafisa sita wa polisi katika kila kituo cha polisi kushughulikia uhusiano wa polisi na vijana.
Boresha sheria na sera kuhusu usalama na usalama mtandaoni.
Elimu
Kutoa elimu bure kuanzia chekechea hadi chuo kikuu.
Toa mlo mmoja kwa siku kwa watoto wa chekechea na madarasa ya mwanzo ya shule za msingi
Kukuza uhusiano wa kufanya kazi kati ya taasisi za elimu na utafiti na viwanda.
Usambazaji wa maji
Wekeza na kukuza uvunaji wa maji ya mvua na udhibiti wa mafuriko.
Kupanua miundombinu ya mabwawa na umwagiliaji.
Kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa kila shule na boma
Gharama ya maisha
Tathmini gharama ya mafuta, unga na nishati katika siku 100.
Kuongeza uwezo wa kusambaza umeme na kupunguza upotevu wa gridi kutoka asilimia 23 hadi 10.
Weka mazingira wezeshi ya kupata chakula, mavazi, malazi na mahitaji mengine ya kimsingi kwa bei nafuu.
Roots Party of Kenya
Vipaumbele
Kuendesha serikali yenye faida kupitia kuhalalisha na kudhibiti utumiaji wa bangi kiviwanda
Kuunda majimbo 8 ambayo yatasimamiwa na serikali zao za shirikisho.
Sitisha katiba, ili kuwapa Wakenya fursa ya kuchagua sheria inayowafaa.
Uchumi
Uchumi wa saa 24 wa zamu ya saa nane, siku nne kwa wiki.
Kuongeza bajeti ya serikali kupitia mapato ya fedha za kigeni kutokana na mauzo ya katani ya viwandani.
Pata mapato kupitia ufugaji wa nyoka na kuuza nje nyama ya mbwa.
Ufisadi
Kuanzisha hukumu ya kifo inayotumika kwa watu wanaopatikana na hatia ya rushwa.
Kutovumilia rushwa.
Madeni
Lipa deni la Kenya haraka kwa mapato kutoka kwa kuhalalisha na usafirishaji wa bangi ya viwandani.
Mkopo huo utalipwa kwa awamu 30 kati ya Januari 2021 hadi Julai 2035.
Epuka madeni kwa kutumia mapato yaliyopatikana kutokana na kuhalalisha bangi ili kuongeza mapato ya serikali.
Ajira
Unda fursa za Uwekezaji na ajira kwa kuhalalisha bangi
Kawi
Tumia katani ya Viwanda kuzalisha nishati ya kibayolojia.
Kupunguza gharama ya nishati kwa kupunguza kodi na kushughulikia mzigo wa madeni.
Afya
Huduma za afya na lishe ya bure kwa wazee, walio katika mazingira magumu na wajawazito.
Boresha matibabu na udhibiti wa Alzheimer's, saratani, ugonjwa wa kupooza kwa ubongo na kifafa kwa kutumia moja ya bidhaa za katani za viwandani.
Kutanguliza utafiti na maendeleo katika kampuni za dawa zinazomilikiwa na Kenya.
Uhalifu na usalama
Kuwalipa polisi vizuri ili kupunguza rushwa.
Elimu
Wape wazazi chaguo la masomo ya nyumbani na kurahisisha mchakato wa usajili.
Boresha mfumo wa elimu wa CBC nchini Kenya.
Usambazaji wa maji
Kuboresha miundombinu ya majisafi na majitaka.
Gharama ya maisha
Tengeneza fursa za ajira na uwekezaji.
Punguza kodi na gharama ya nishati.
Chama cha Agano
Vipaumbele
Unda taasisi zitakazomaliza ubadhirifu wa fedha na kukomesha ufisadi.
Hakikisha kwamba haki za wasio na sauti na waliotengwa zinazingatiwa.
Punguzo la ushuru kwa Wakenya kusaidia kudhibiti gharama ya maisha.
Uchumi
Kupeleka bajeti kwa halmashauri za vijiji badala ya Hazina na Ikulu.
Weka mazingira mazuri kwa sekta binafsi na watu binafsi kuanzisha biashara.
Ufisadi
Fanya ripoti za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kuwa ushahidi wa msingi wa matumizi mabaya ya ofisi na msingi wa kuwashtaki watumishi wa umma walio wafisadi
Kesi zote za ufisadi zitashughulikiwa ndani ya miezi mitatu.
Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa kupewa mamlaka ya kuendesha mashtaka.
Madeni
Majadiliano kwa lengo la kupanga upya ulipaji wa deni na wakopeshaji.
Tumia fedha zilizopatikana kutokana na shughuli za kifisadi kulipa madeni ya nje.
Kurejesha fedha zilizofichwa nje ya nchi ili kusaidia kulipa deni la nje .
Ajira
Tekeleza sheria ya maudhui ya humu nchini kwa kuongeza kiwango cha juu cha kandarasi zinazotolewa kwa makampuni ya kigeni hadi zaidi ya $8.5 milioni (Ksh1 bilioni).
Punguzo la kodi kwa makampuni yanayoajiri wanawake na vijana.
Kuharakisha utekelezaji wa mpango wa Kanda Maalum ya Kiuchumi ili kuhimiza wageni,makampuni ya kuanzisha viwanda vya utengenezaji nchini Kenya.
Kawi
Kusaidia matumizi ya nishati ya jua nje ya gridi ya taifa.
Kufanya nishati kuwa bei nafuu kwa kushughulikia rushwa katika sekta ya nishati.
Afya
Unda tume ya kitaifa ya afya ili kudhibiti kupanda kwa gharama za afya.
Kutoa ruzuku kwa michango ya Mfuko wa Kitaifa wa Bima ya Afya kwa kila familia Kenya.
Uhalifu na usalama
Kuboresha maisha na mazingira ya kazi ya polisi.
Fanya vikosi vya usalama kuwa vya kisasa ili kuendana na uhalifu wa kisasa.
Punguza msongamano wa magereza na kuboresha hali ya maisha na kazi ya maafisa wa magereza
Elimu
Kuanzisha kipengele cha maadili katika mtaala.
Elimu ya bure katika ngazi zote.
Walimu wawezeshwe kidijitali kufanya kozi za kujiongeza masomo
Usambazaji wa maji
Maeneo kame kupokea maji ya bomba kwa ajili ya umwagiliaji.
Kuondoa tozo dhidi ya vifaa vyote vya kuvuna maji ya mvua.
Kukuza upandaji miti upya.
Gharama ya maisha
Msamaha wa jumla wa 50% kwa PAYE kwa Wakenya wote.
Kenya Kwanza Alliance
Vipaumbele
Tenga $427 milioni (Ksh50 bilioni) kila mwaka ili kutoa mikopo kwa biashara ndogo ndogo na za kadri kwa njia rahisi na inayotegemeka
Kurekebisha Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili kubadilisha mchango kwa familia/nyumba badala ya watu binafsi.
Mtandao wa bure ndani ya miaka mitano.
Uchumi
Komesha ushuru unaorudiwa
Fanya leseni ya biashara na eneo kuwa haki.
Weka sera thabiti ya ulinzi wa huduma za kifedha ili kuwalinda Wakenya dhidi ya wakopeshaji walaghai.
Ufisadi
Kuzipa uhuru taasisi zinazohusika na vita dhidi ya rushwa.
Taarifa za wafanyabiashara wanaofanya biashara na serikali kuwekwa wazi.
Shirikiana na nchi nyingine kusaidia kurejesha mali zilizoibiwa.
Madeni
Kuimarisha uwezo wa serikali wa kukopesheka kutoka nje na kuongeza upatikanaji wa mikopo nafuu, na kuacha vyanzo vya mikopo vya ndani kwa sekta binafsi.
Ajira
Wekeza kwenye kilimo ili kutengeneza ajira zaidi.
Anzisha Kituo cha Maendeleo ya Biashara cha MSME katika kila kata na bustani ya viwanda.
Kuanzisha kituo cha ukuzi wa biashara katika kila taasisi ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi.
Kawi
Weka mfumo wa kisheria wa kulinda hazina ya uimarishaji wa mafuta.
Unda vivutio vya kupitishwa kwa mifumo ya usafiri wa umma ya umeme katika miji na miji yote.
Kuharakisha maendeleo ya rasilimali ya kawi ya mvuke
Afya
Huduma ya afya ya msingi inayofadhiliwa kikamilifu.
Kuanzisha mfuko wa kitaifa wa magonjwa sugu.
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wa lazima.
Uhalifu na usalama
Imarisha uangalizi wa polisi na kuteua mchunguzi atakayezingatia ukiukwaji wa haki za binadamu kwa vijana.
Bima ya maisha kwa maafisa wa polisi iwapo watafariki wakiwa kazini.
Mfuko wa hisani wa kuchangia familia za maafisa walioaga dunia na wagonjwa mahututi.
Elimu
Lipia mafunzo ya ualimu kazini.
Tathmini mfumo wa sasa wa maendeleo ya kitaaluma kulingana na mitihani.
Kupunguza pengo la sasa la upungufu wa walimu 116,000 ndani ya miaka miwili ya kifedha.
Usambazaji wa maji
Maji yatapewa kipaumbele kwa ruzuku ya mradi/ufadhili wa masharti nafuu.
Hamisha mwelekeo kutoka kwa mabwawa makubwa hadi kwenye miradi ya maji ya kijamii huku msisitizo ukiwa katika kuvuna na kurejeleza
Gharama ya maisha
Kuongeza tija ya kilimo ili kupunguza gharama ya maisha.
Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.
End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?
Ukiukaji wa sheria
Rais wa taifa amelaumiwa kwa kukiuka amri za mahakama bila kujali athari zake kwa umma na swala zima la utiifu wa raia kwa sheria za nchi kwa mfano, licha ya mahakama kuamuru zaidi ya mara kumi kwamba Wakili Dkt. Miguna Miguna ni raia wa Kenya na kwamba angepaswa kurejeshewa cheti chake cha uraia wa Kenya na aruhusiwe kurejea Kenya, hilo limepuziliwa mbali hadi leo, kadhalika, rais na serikali yake alikataa kuwateua majaji fulani licha ya kwamba kisheria, huo uwezo haukuwa wake bali wa tume ya kuwaajiri majaji yaani "Judicial Service Commission".
Kuhusu ugatuzi, - licha ya kwamba huduma ya afya imeamriwa na katiba kuwa huduma ya serikali gatuzi, Rais and serikali amekatalia huduma hii na kukwamilia bajeti nzima ya Wizara ya afya Nairobi. Hii ni mifano michache tu inayoonyesha kwamba, kwa ujumla, safari ya serikali hii kutimiza ahadi zake kwa raia wa Kenya imekuwa na changamoto si haba.
Hata hivyo, mgalla muue lakini haki yake mpe! Serikali hii ilijizatiti kujenga barabara za lami kilomita elfu kumi nchini, japo maeneo fulani ya taifa yamefaidika mno kuliko mengine katika nyanja hii.
Barabara tajika mno ni ile inayotoka karibu na uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta hadi mtaa wa Westlands (Expressway).
Pili, katika hospitali za serikali za Ugatuzi, hospitali hizo zimeimarishwa na kupewa mitambo ya kisasa, ikiwemo mashine za kutibu saratani.
Vile vile, kupitia kwa mama taifa, Margaret Kenyatta, mpango wa kuwafikishia kina mama wajawazito huduma za matibabu umefanya makubwa katika kuokoa akina mama wanaojifungua. Mpango huu uliitwa "Beyond Zero Campaign, ukiwa na lengo la kuhakikisha kwamba hakuna hata mama mmoja mjamzito atakayeaga dunia kwasababu ya ukosefu wa matibabu ya kujifungua.
Huduma hizi ambazo ni za bure kujifungua kina mama zimewafikia kina mama wengi na hili limeimarisha hali nzima ya afya ya kina mama, japo kwa viwango vidogo .
Katika usafiri, reli ya kisasa, maarufu "SGR" imejengwa kutoka Mombasa hadi Nairobi na kurahisisha, pakubwa, usafirishaji watu na mizigo.
Serikali imeng'ang'ana katika usafishaji wa mitaa ya mabanda duni katika miji mikuu ya taifa, hususan Nairobi katika mitaa ya Kibra, Korogocho, Mathare na Nyalenda kule Kisumu. Katika mitaa hiyo, taa zimewekwa, barabara kupanuliwa na mitaro ya maji machafu pamoja na uzoaji taka kuimarsihwa. Hili limeleta hali bora ya usalama na maisha afadhali katika mabanda hayo.
Aidha, katika mitaa kadhaa, ujenzi wa nyumba za bei nafuu umefanyika japo kwa mwendo wa aste aste, kwa mfano katika mtaa mdogo wa Soweto, mtaani Kibra, nyumba mia nane kumi na mbili zimejengwa na kupewa wakaaji wa mtaa huo, kwa malipo ya pole na madogo madogo.
Marekebisho na uimarishaji wa uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta umefanywa kwa kiwango kikubwa. Marekebisho haya sasa yanawezesha uwanja huu kupokea wasafiri milioni 7.5 kutoka kwa kiwango cha awali cha wasafiri milioni 2.5. Hili limewezesha uwanja huu kuimarisha utalii na biashara zinginezo nchini Kenya na kwa hivyo kuimarisha uchumi wa Kenya kwa kiwango fulani.
Kuanzishwa kwa vituo vya kupeleka huduma za serikali karibu na raia maarufu "Huduma Centres" kumesaidia serikali kufikisha huduma zake karibu na raia. Hili limewapunguzia dhiki wanananchi katika kutafuta huduma muhimu za serikali.
Viwango vya stima nchini vimeimarishwa kupitia mradi wa kufikisha stima katika kila nyumba ya mkenya kwa jina "last mile connectivity". Kiwango cha stima cha "325 megawatts" kimeongezwa katika nyaya za stima Kenya kutoka kituo cha Olkaria 1 na 2 na 20MW kutoka vilima vya Ngong
Maelezo ya picha, Uhuru kenyatta na Raila Odinga
Kuvunjika kwa uhusiano wa rais na naibu wake
Kwa ujumla, ni vigumu kutoa uamuzi fika iwapo kupigwa kumbo Naibu Rais William Ruto kumechangia kudhibiti au kudhoofisha uwezo wa serikali ya Jubilee kutimiza au kutotimiza ahadi zake.
Hata hivyo, Dkt. Ruto mwenyewe amenukuliwa mara si moja akidai kuwa asingelisukumwa kando ya serikali aliyoibuni kwa mikono yake, ahadi zote zingetimizwa. Amemlaumu rais Kenyatta pamoja na aliyekuwa Waziri mkuu Kenya, Bwana Odinga kwa kile anachokiona kisirani cha 'handisheki na mzaliwa wake BBI'.
Kwake yeye Dkt. Ruto, laiti wangesalia pamoja kama Uhuruto, serikali ingelitimza hata yale ambayo haikuweza kutimiza katika hatamu yao ya kwanza (2013-2017)
Yote tisa, la kumi ni kwamba, Serikali ya Jubilee, japo ilijaribu kutimiza ahadi zake, kwa sasa uchumi umedorora na hali si hali tena -gharama ya maisha imewazonga raia wa kawaida.