Uchaguzi wa Kenya 2022: Je ahadi za serikali ya Jubilee kwa Wakenya zimetimizwa?

.
Maelezo ya picha, William Ruto na Uhuru kenyatta wakati wa kampeni za uchaguzi wa 2013
    • Author, Alutalala Mukhwana
    • Nafasi, Mchambuzi Kenya

Mwaka wa 2013, tarehe 4 mwezi Machi , serikali mpya ya Jubilee, maarufu "Uhuruto ", ilichukua mamlaka baada ya uchaguzi mkuu.

Utawala huo mpya Uhuru Kenyatta pamoja naye Naibu Rais William Ruto, uliwapa matumaini chungu nzima wafuasi wao kwamba maisha ya Wakenya yangebadilika kuwa bora zaidi.

Wao Uhuru na mwenzake Wiilliam Ruto walionyesha ukuruba mkubwa hadharani na hilo likatia shani uhusiano wao na kuwaongezea matumaini maradufu Wakenya kuwa maisha yao yangelikuwa bora zaidi.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Kabla ya mwaka huo, kwa miaka mitatu mtawalia iliyotangulia, uchumi wa Kenya ulikua kwa viwango vya asilima 5.8,4.4 na 4.5.

Ahadi za serikali ya Jubille kwa Wakenya

Rais Kenyatta akihutubia wabunge Aprili 16 mwaka wa 2013, alianisha, ahadi za serikali yake ifuatavyo: Uongozi ulio wa haki, ukweli na uwazi, kulinda na kutetea haki na uhuru wa raia, kupambana na kumaliza ufisadi, kutekeleza na kufanikisha ugatuzi ili kutimiza katiba mpya, kazi milioni moja kwa vijana kila mwaka, uwajibikaji katika utendakazi kwa umma, barabara za lami pamoja na kusambaza nguvu za umeme na huduma za maji kwa raia wote.

Idadi kubwa ya raia wa Kenya ni vijana walio chini ya umri wa miaka thelathini na mitano, nao waliahidiwa viwanja kumi na sita kote nchini katika nyanja ya michezo, kando na nafasi za kazi milioni moja kila mwaka.

Uchaguzi Kenya 2022:Unaweza pia kusoma

Je serikali ilifanikiwa kutekeleza ahadi zake kwa Wakenya?

Chambilecho wahenga, ahadi ni deni, na dawa yake ni kulilipa. Je, serikakali ya Jubilee, kwa hatamu zote mbili sasa, imelipia ahadi zake? Je, kupigwa kumbo Naibu Rais William Ruto, kumeadhiri vipi kulipwa au kulipwa deni hili.?

Baada ya hatamu ya kwanza, mwaka wa 2017 serikali ya Jubilee ilirejeshwa mamlakani kwa awamu ya pili. Mara hii, serikali ikaahidi kwamba sasa ajenda zake zingekuwa nne: Chakula tosha kwa raia wake, nyumba na makazi kwa bei nafuu, viwanda na mwisho matibabu kwa wote kwa bei nafuu.

.
Maelezo ya picha, William Ruto na Uhuru kenyatta wakati wa kampeni za uchaguzi wa 2013

Kwa kupunguza ajenda yake, ni ishara tosha kwamba serikali ilikuwa imeshindwa kutimiza ahadi za mwaka 2013? Mathalan: Nafasi za kazi milioni moja hazikupatikana, madai ya visa vya ufisadi bado yaliripotiwa hata kwa viwango vikubwa zaidi kama vile Eurobond, sakata ya Afya House, na kadhalika.

Viwango vya riba viliruka juu zaidi hivi kwamba raia wamekuwa wakitatizika kukopa mikopo ya kujiendeleza kibiashara. Deni la umma hivi sasa limeruka hadi trilioni 8.02 ikilinganishwa na trilioni 6.7 mwezi Juni 2013 miezi mitatu tu baada ya Jubilee kuchukua usukani.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Ukiukaji wa sheria

Rais wa taifa amelaumiwa kwa kukiuka amri za mahakama bila kujali athari zake kwa umma na swala zima la utiifu wa raia kwa sheria za nchi kwa mfano, licha ya mahakama kuamuru zaidi ya mara kumi kwamba Wakili Dkt. Miguna Miguna ni raia wa Kenya na kwamba angepaswa kurejeshewa cheti chake cha uraia wa Kenya na aruhusiwe kurejea Kenya, hilo limepuziliwa mbali hadi leo, kadhalika, rais na serikali yake alikataa kuwateua majaji fulani licha ya kwamba kisheria, huo uwezo haukuwa wake bali wa tume ya kuwaajiri majaji yaani "Judicial Service Commission".

Kuhusu ugatuzi, - licha ya kwamba huduma ya afya imeamriwa na katiba kuwa huduma ya serikali gatuzi, Rais and serikali amekatalia huduma hii na kukwamilia bajeti nzima ya Wizara ya afya Nairobi. Hii ni mifano michache tu inayoonyesha kwamba, kwa ujumla, safari ya serikali hii kutimiza ahadi zake kwa raia wa Kenya imekuwa na changamoto si haba.

Hata hivyo, mgalla muue lakini haki yake mpe! Serikali hii ilijizatiti kujenga barabara za lami kilomita elfu kumi nchini, japo maeneo fulani ya taifa yamefaidika mno kuliko mengine katika nyanja hii.

Barabara tajika mno ni ile inayotoka karibu na uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta hadi mtaa wa Westlands (Expressway).

Pili, katika hospitali za serikali za Ugatuzi, hospitali hizo zimeimarishwa na kupewa mitambo ya kisasa, ikiwemo mashine za kutibu saratani.

Vile vile, kupitia kwa mama taifa, Margaret Kenyatta, mpango wa kuwafikishia kina mama wajawazito huduma za matibabu umefanya makubwa katika kuokoa akina mama wanaojifungua. Mpango huu uliitwa "Beyond Zero Campaign, ukiwa na lengo la kuhakikisha kwamba hakuna hata mama mmoja mjamzito atakayeaga dunia kwasababu ya ukosefu wa matibabu ya kujifungua.

Huduma hizi ambazo ni za bure kujifungua kina mama zimewafikia kina mama wengi na hili limeimarisha hali nzima ya afya ya kina mama, japo kwa viwango vidogo .

Katika usafiri, reli ya kisasa, maarufu "SGR" imejengwa kutoka Mombasa hadi Nairobi na kurahisisha, pakubwa, usafirishaji watu na mizigo.

Serikali imeng'ang'ana katika usafishaji wa mitaa ya mabanda duni katika miji mikuu ya taifa, hususan Nairobi katika mitaa ya Kibra, Korogocho, Mathare na Nyalenda kule Kisumu. Katika mitaa hiyo, taa zimewekwa, barabara kupanuliwa na mitaro ya maji machafu pamoja na uzoaji taka kuimarsihwa. Hili limeleta hali bora ya usalama na maisha afadhali katika mabanda hayo.

Aidha, katika mitaa kadhaa, ujenzi wa nyumba za bei nafuu umefanyika japo kwa mwendo wa aste aste, kwa mfano katika mtaa mdogo wa Soweto, mtaani Kibra, nyumba mia nane kumi na mbili zimejengwa na kupewa wakaaji wa mtaa huo, kwa malipo ya pole na madogo madogo.

Marekebisho na uimarishaji wa uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta umefanywa kwa kiwango kikubwa. Marekebisho haya sasa yanawezesha uwanja huu kupokea wasafiri milioni 7.5 kutoka kwa kiwango cha awali cha wasafiri milioni 2.5. Hili limewezesha uwanja huu kuimarisha utalii na biashara zinginezo nchini Kenya na kwa hivyo kuimarisha uchumi wa Kenya kwa kiwango fulani.

Kuanzishwa kwa vituo vya kupeleka huduma za serikali karibu na raia maarufu "Huduma Centres" kumesaidia serikali kufikisha huduma zake karibu na raia. Hili limewapunguzia dhiki wanananchi katika kutafuta huduma muhimu za serikali.

Viwango vya stima nchini vimeimarishwa kupitia mradi wa kufikisha stima katika kila nyumba ya mkenya kwa jina "last mile connectivity". Kiwango cha stima cha "325 megawatts" kimeongezwa katika nyaya za stima Kenya kutoka kituo cha Olkaria 1 na 2 na 20MW kutoka vilima vya Ngong

.
Maelezo ya picha, Uhuru kenyatta na Raila Odinga

Kuvunjika kwa uhusiano wa rais na naibu wake

Kwa ujumla, ni vigumu kutoa uamuzi fika iwapo kupigwa kumbo Naibu Rais William Ruto kumechangia kudhibiti au kudhoofisha uwezo wa serikali ya Jubilee kutimiza au kutotimiza ahadi zake.

Hata hivyo, Dkt. Ruto mwenyewe amenukuliwa mara si moja akidai kuwa asingelisukumwa kando ya serikali aliyoibuni kwa mikono yake, ahadi zote zingetimizwa. Amemlaumu rais Kenyatta pamoja na aliyekuwa Waziri mkuu Kenya, Bwana Odinga kwa kile anachokiona kisirani cha 'handisheki na mzaliwa wake BBI'.

Kwake yeye Dkt. Ruto, laiti wangesalia pamoja kama Uhuruto, serikali ingelitimza hata yale ambayo haikuweza kutimiza katika hatamu yao ya kwanza (2013-2017)

Yote tisa, la kumi ni kwamba, Serikali ya Jubilee, japo ilijaribu kutimiza ahadi zake, kwa sasa uchumi umedorora na hali si hali tena -gharama ya maisha imewazonga raia wa kawaida.