Wafahamu baadhi ya viongozi wa dunia wanaotetea Uislamu licha ya kutokuwa Waislamu

Justin Trudeau rai'sul wasaaraha Canada

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Justin Trudeau waziri mkuu wa Canada

Justin Trudeau waziri mkuu wa Canada

Waziri mkuu wa Pakistan anasema atavipa kipaumbele vita dhidi chuki dhidi ya Uislamu. Rais Imran Khan hutumia akaunti yake ya Twitter na hotuba zake kupambana na maoni dhidi ya Uislamu .

Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na malalamiko ya kuongezeka kwa chuki dhidi ya Uislamu, hususan katika mataifa ya magharibi.

Katika baadhi ya maeneo , Waislamu wamekuwa wakiangaliwa kama magaidi.

Hatahivyo, kuna viongozi wengi ambao sio Waislamu ambao wamekuwa wakiwatetea Waislamu na Uislamu, wakiwemo viongozi wenye nguvu duniani.

Wafuatao ni baadhi ya vongozi wa dunia ambao sio Waislamu ambao wamekuwa wakiwalinda Waislamu dhidi ya chuki dhidi ya Uislamu.

Justin Trudeau

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Justin Trudeau

Justin Trudeau

Waziri Mkuu wa Canada Trudeau ni mmoja wa viongozi kadhaa wa Magharibi ambaye amepinga wazi chuki dhidi ya Uislamu.

Mwaka 2020 Trudeau alisema kwamba chuki dhidi ya Uislamu "haikubaliki" na aliapa kuhakikisha nchi yake ni salama kwa waislamu.

"Bila shaka chuki dhidi ya Uislamu na ubaguzi havina nafasi katika Canada," alisema Trudeau.

Aliongeza kuwa, " Tnahitaji kumaliza chuki hii na kuifanya jamii yetu kuwa ya amani na Waislamu nchini Canada."

Alikuwa akizungumza baada ya shambulio dhidi ya msikiti katika mji wa Quebec nchini humo.

JacindaArdern

Jacinda Ardern

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Jacinda Ardern

Shambulio la vifo katika msikiti katika Christchurch, New Zealand, liliwashitua wengi.

Lakini jibu kutoka kwa Waziri mkuu wa New Zealand Jacinda Ardern lilisifiwa kwa kiasi kikubwa. Bi Ardern alionyesha huruma kwa Waislamu wan chi hiyo na kuelezea kusikitishwa san ana kile kilichotokea.

Alivaa hijabu alipokutana na Waislamu na akasema washambuliaji hawakutoka New Zealand. Shambulio katika msikiti wa Christchurch liliwauwa waumini wa Kiislamu 50 katika msikiti.

Vladimir Putin

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Vladimir Putin

Vladimir Putin

Rais wa Urusi Vladimir Putin ni mmoja wa viongozi ambao sio Waislamu ambaye amesikika mara kwa mara kuwalinda Waislamu.

Hupinga vikali matusi dhidi ya Mtume Muhammad (sws) na chuki dhidi ya Uislamu.

Katika hotuba aliyoitoa mwezi Disemba mwaja jana, Rais Putin alisema kwamba matusi dhidi ya Mtume Muhammad hayawezi kuelezewa "uhuru wa kujieleza".

Kumtusi Mtume Muhammad ni "ukiukaji wa uhuru wa kidini na kukiuka utakatifu wa Waislamu," aliongeza.

Unaweza pia kusoma:

Brack Obama

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Brack Obama

Barack Obama

Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama pia alizungumza wazi dhidi ya chuki dhidi ya waislamu wakati alipokuwa madarakani kama rais.

Aliwalinda Waislamu nchini Marekani dhidi ya ubaguzi wa kidini.

Aliwatolea wito Wamarekani wakati ule kupambana dhidi ya chuki kwa Waislamu

"Waislamu nchini Marekani ni Rafiki zetu, wafanyakazi wenzetu, mashujaa wetu wa michezo-na ndio, ni wanawake na wanaume katika jeshi letu ," alisema Obama.