Milipuko Uganda: Watu 6 wafariki katika milipuko Kampala

Chanzo cha picha, Photoshot
Polisi nchini uganda wamethibitisha kwamba takriban watu sita wamefariki katika milipuko iliyotokea mjini Kampala mapema leo.
Shirika la habari la Reuters linanukuu kituo cha televisheni cha ndani juu ya idadi ya vifo.
NTV Uganda imesema Meya wa Kampala Salim Uhuru ndiye chanzo cha habari za vifo vya watu wawili vilivyoripotiwa hapo awali
Ripota wa NTV alisema aliona sehemu za mwili zikiwa zimetapakaa katika eneo moja la mlipuko huo:
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
Majengo ya ofisi yalitikisika wakati milipuko hiyo ilipoanza, baadhi ya mashahidi wameiambia BBC.
Gazeti la Daily Monitor limesambaza video ya magari yakiungua nje ya jengo la bima baada ya mlipuko huo:
Haijulikani ni watu wangapi wamejeruhiwa.
Mwezi uliopita, milipuko miwili tofauti nchini humo iliua watu wawili. Mmoja ulimuua mhudumu katika baa na mwingine, mshambuliaji wa kujitoa mhanga ambaye alikuwa ameingiza vilipuzi kwenye basi.
Mamlaka nchini humo zimeshutumu milipuko hiyo ya Oktoba dhidi ya kundi la waasi wa Kiislamu lenye makao yake makuu nchini Uganda, DR Congo, Allied Democratic Forces.
Takriban watu 50 wamekamatwa, na wengine kushtakiwa mahakamani, tangu matukio hayo ya hivi majuzi.












