Takwimu ligi kuu England: Ryan Sessegnon na chipukizi wanaojikita na kung'aa

A picture of fireworks above the Millennium Dome

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Ryan Sessegnon ni miongoni mwa vijana wanao ng'ara katika ligi kuu England

Iwapo una zaidi ya miaka 25 basi huenda ukajihisi mkongwe...

Watoto waliozaliwa milenia hii wanaonekana kujikita na kudhihirisha umuhimu wao katika ligii kuu England.

BBC Sport imetathmini takwimu muhimu kutoka kwa timu kuu wikendi hii.

Watoto wa Milenia wamewasili

Y2K - Manjonjo kama alivyosema msanii wa taarab ya Rusha Roho Khadija Kopa Tanzania - kirusi cha kompyuta kilichotabiriwa kusababisha ghasia ( Hakikufanikiwa) wasanii wa hip hop kama Britney Spears

na kadhalika yote haya yanakumbusha kuingia kwa milenia mpya. Lakini hiyo ni kama wewe u mzee kutosha kuyafahamu au kuyakumbuka haya.

Mchezaji wa Fulham mwenye miaka 18 Ryan Sessegnon hakumbuki. Kwasababu alizaliwa 2000.

Ryan Sessegnon scores for Fulham against Cardiff

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Ryan Sessegnon (kushoto) aliichezea Fulham kwanza mnamo 2016

Mchezaji huyo wa kimataifa wa timu ya wachezaji walio chini ya umri wa miaka -21 ya England aliteleza na kufunga bao la pili wikendi hii dhidi ya Cardiff . Licha ya kwamba bao hilo halikuwa na uzito vile maana mwisho mechi ilimalizika kwa Fulham kufungwa 4-2, alifanikiwa kuwa mchezaji wa kwanza aliyezaliwa mwaka 2000 kuwahi kufunga katika timu kuu ya England.

Sessegnon ni mojawapo ya wachezaji wanane waliozaliwa katika milenia hii kuwahi kucheza katika ligi kuu ya England.

Na mchezaji huyo asiyekosekana katika mechi za Fulham msimu huu ina maanisha hakuna mchezaji mwingine aliyezaliwa 2000 amewahi kucheza zaidi katika ligi kuu ya England kama yeye...

line

Hatahivyo, Sessegnon na Foden bado wako mbali na mchezaji mwingine chipukizi wa England ambaye ameweka historia ya milenia.

Jadon Sancho amekuwa mchezaji wa kwanza wa kimataifa aliyezaliwa katika miaka ya 2000 alipocheza kwa mara ya kwanza dhidi ya Croatia wiki iliyopita.

Fulham forward Ryan Sessegnon

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mchezaji wa kiungo cha mbele wa Fulham Ryan Sessegnon

Mchezaji huyo mwenye miaka 18 alitoka Manchester City kujiunga na Borussia Dortmund mwaka jana na anapata faida kwa kujumuishwa katika kikosi cha kwanza katika ligi ya Ujerumani Bundesliga.

Sancho ameichezea timu hiyo kuu ya Ujerumani mara 20, inayomaanisha ni mchezaji mmoja pekee aliyezaliwa milenia hii - mchezaji wa kiungo cha kati wa Juventus Moise Kean, aliyekuwa kwenye mkopo huko Verona msimu uliopita - aliye na uzoefu mkubwa katika ligi tano kubwa za Ulaya.

line

Sessegnon aliibuka kuwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi wa Fulham alliyeifungia timu hiyo katika Primia Ligi akiwa na miaka 18 na siku 154 .

Lakini bado hajafuzu kuwa katika orodha ya wafungaji 10 bora walio wadogo katika historia ya mashindano hayo.