Mwanamuziki XXXTentacion auawa kwa kupigwa risasi Florida, Marekani

XXXTentacion

Chanzo cha picha, Shutterstock

Muda wa kusoma: Dakika 2

Mwanamuziki wa nyimbo za rap Marekani XXXTentacion, ambaye alipata umaarufu kwa haraka kupitia albamu zake mbili ameuawa kwa kupigwa risasi akiwa na miaka 20.

Alikuwa anaondoka kwenye duka la kuuza pikipiki kusini mwa Florida Jumatatu pale mtu mwenye bunduki alipomfyatulia risasi.

Polisi katika tarafa ya Broward wanasema XXXTentacion, ambaye jina lake Jahseh Onfroy, alikimbizwa hospitalini lakini akathibitishwa kufariki.

Alikuwa mara nyingi akielezwa kama mmoja wa wanamuziki wa rap wenye kuzua utata zaidi.

Alikuwa pia amekabiliwa na mashtaka ya kumshambulia mpenzi wake.

Rapa huyo, ambaye alipata umaarufu kwa kupakia nyimbo zake katika mtandao wa SoundCloud, alikuwa anatazamwa na wengi kama kielelezo cha mtu kufanikiwa kupitia kipaji chake.

Wapenzi wa muziki wake na wanamuziki nyota wa hip-hop wamekuwa wakituma salamu za rambirambi kuomboleza kifo chake.

Liwali wa tarafa hiyo amesema Onfroy alikuwa anaondoka kwenye duka hilo muda mfupi kabla ya saa kumi alasiri pale washukiwa wawili waliokuwa na silaha walipofika kwake.

Rapper XXXTentacion, also known as Jahseh Dwayne Onfroy

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Albamu ya karibuni ya mwanamuziki huyo ilianza ikiwa kwenye orodha ya nyimbo 200 bora Marekani

Mmoja wao anadaiwa kumpiga risasi kabla ya wote wawili kukimbia eneo la tukio Deerfield Beach, takriban maili 43 (69km) kaskazini mwa Miami wakitumia gari aina ya SUV la rangi nyeusi.

Wachunguzi wanasema huenda kilikuwa kisa cha wizi wa mabavu.

Video iliyopakiwa kwenye mitandao ya kijamii ilimuonesha mwanamuziki huyo akiwa amelala ndani ya gari lake baada ya kupigwa risasi.

XXXTentacion attends BET Hip Hop Awards 2017

Chanzo cha picha, Thaddaeus McAdams/FilmMagic/Getty

Maelezo ya picha, Waliotuma rambirambi zao ni pamoja na Kanye West na J Cole

Mmoja wa walioshuhudia ameambia tovuti ya TMZ kwamba milio kadha ya risasi ilisikika nje ya duka hilo.

Rapa huyo, ambaye nyimbo zake ni pamoja na SAD! na Moonlight, zilipata umaarufu sana baada yake kutoa albamu yake ya kwanza kwa jina 17 Agosti mwaka jana.

Alitoa albamu nyingine kwa jina ? ambao ilianza ikiwa kwenye chati ya nyimbo 200 maarufu mwezi Machi na nyimbo za albamu hiyo zilikuwa zimesikizwa mara milioni mia kadha mtandaoni.

Alizungumzia mambo kama vile mfadhaiko na msongo wa mawazo na alisifiwa na baadhi ya wanamuziki nyota wa rap.

Lakini uimbaji wake ulikumbwa na utata, huku akituhumiwa kwa makosa ya kuwashambulia na kuwapiga watu.

XXXTentacion

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, XXXTentacion alihudhuria sherehe ya kutoa tuzo za Hip Hop za BET

Alikuwa anakabiliwa na mashtaka 15 ya kuwashambulia watu kufikia wakati wa kifo chake, shtaka moja likiwa la kumpiga mwanamke mja mzito.

XXXTentacion alikulia katika maisha ya dhiki na alifukuzwa shuleni kwa sababu ya kupigana, lakini alielekeza nguvu zake na ghadhabu kwenye muziki.

Kufikia Oktoba, alikuwa ametia saini mkataba wa muziki uliodaiwa kuwa wa dhamani ya $6 milioni (£4.5m).

Presentational grey line

Kanye West amesema: "Sikukwambia jinsi ulivyonihamasisha ulipokuwa hapa nasi."

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Presentational white space

Mchezaji soka wa Liverpool na England Daniel Sturridge amesema leo ni "siku ya huzuni kwa muziki."

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Rapa J Cole pia ametuma salamu zake za rambirambi.