Tetesi kubwa tano za soka Ulaya jioni hii (30.08.2022)

Frenkie de Jong

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Frenkie de Jong

Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp kuhusu kusajili kiungo anasema:

"Ni kweli, lakini muda unavyokwenda, ndio inavyozidi kuwa ngumu (kukamilisha usajili). Hatujakata tamaa. muda upo, tusipata bado ninakifurahia kikosi tulichonacho"

Frenkie de Jong wa Barecelona na Moises Caicedo wa Brighton wamekuwa wakihusishwa kutua Anfield (Klopp Presser).

Elneny

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Elneny

Arsenal watalazimika kuingia sokoni kusaka kiungo wa kukaba baada ya Mohamed Elneny kuumia kwenye mchezo dhidi ya Fulham utakaomuweka nje kwa muda mrefu. Elneny alikuwa mbadala wa kiungo namba moja Thomas Partey ambaye naye ni majeruhi.

Willian

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Willian

Fulham wanakaribia kukamilisha usajili wa winga wa zamani wa Chelsea na Arsenal Willian, kwa mkataba wa mwaka mmoja. Mbrazil huyo yuko London sasa anafanyiwa vipimo (The Athletic).

Mazungumzo yaliyo katika hatua za mwisho yanaendelea kati ya Chelsea na Barcelona kuhusu uhamisho wa Pierre Aubameyang (Romano).

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

Mwisho wa X ujumbe, 1

Antony Matheus dos Santos

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Antony Matheus dos Santos

Klabu za Ajax na Manchester United zimetoa taarifa rasmi kuhusu Antony: "Ajax na Manchester United zimekubaliana kuhusu uhamisho wa Antony Matheus dos Santos." Ada yake inafikia €100 million.

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

Mwisho wa X ujumbe, 2