Tetesi kubwa tano za soka Ulaya jioni hii (19.08.2022)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kocha wa Arsenal Mikel Arteta amesema mshambuliaji wa pembeni wa timu hiyo, Bukayo Saka, anakaribia kusainia mkataba mpya.
“Nina imani kubwa kwamba upande wetu na upande wa Bukayo tuko pamoja- kilichosalia ni kuweka kwenye maandishi tu”, alisema. (Romano via Arsenal.com)
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1
Arteta anasema pia kwa sasa klabu hiyo inajielekeza zaidi kuangalia mustakabali wa wachezaji wake kabla ya kufikiria kusajili wapya katika muda wa usajili uliobaki.
"Anapaswa kuwa mchezaji sahihi, tunataka kusajili mchezaji wa kiwango cha juu, sio mchezaji tu."

Chanzo cha picha, Getty Images
Kiungo wa Real Madrid, Casemiro asubuhi leo amewaaga wachezaji wenzake wa klabu hiyo baada ya kukubali kujiunga na Manchester United. Kocha wa Madrid, Carlo Ancelotti amethibitisha pia asubuhi kwamba Mbrazil huyo anakaribia kuondoka Bernabéu. (Skysport)
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2
Mtendaji mkuu wa Borussia Dortmund Hans-Joachim Watzke amepuuzilia mbali taarifa kwamba klabu hiyo inaweza kumsajili Cristiano Ronaldo.
Kufuatia taarifa zilizotolewa na gazeti la BILD la Ujerumani lililosema kwamba Dortmund wanaweza kumsajili mshambuliaji huyo wa Manchester United, Watzke alisema: “nampenda, ukweli ni wazo zuri - kumuona Cristiano akicheza Signal Iduna Park. Lakini hakuna mkataba wowote tulioingia, kwa maana hiyo tuache kuzungumzia hilo." (Sky sport football)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kocha wa NewcastleEddie Howe imeiambia Real Madrid isahau kuhusu jaribio lake la kumsajili Bruno Guimaraes kutoka Tyneside kufuatia tetesi kwamba imeelekeza nguvu kumsajili.
Mbrazil huyo mwenye miaka 24, alisajiliwa kwa ada ya £40m mwezi Januari akitokea Lyon, akionekana kama mbadala wa kiungo wa Madrid, Casemiro anayeelekea Manchester United.

Chanzo cha picha, Getty Images
End of Unaweza kusoma pia













