Songkran: Thailand inaadhimisha tamasha la kibudha kwa vita vya maji

Watu wa Bangkok katika vita vya maji

Chanzo cha picha, EPA

Wathailand wanasherehekea mwaka huu kwa tamasha la Songkran , unaofahamika pia kama mwaka wa Wabudha

Tamasha hilo ambalo hufanyika kati ya tarehe 13 na 15 Aprili nchini Thailand, pia husherehekewa katika maeneo mengine kama Laos, Cambodia and Myanmar.

Songkran hujulikana mara kwa mara kama kama vita vikubwa vya maji duniani.

Picha kutoka kote nchini Thailand zinaonyesha umati mkubwa wa watu wakishiriki sherehe hizo.

Siku hiyo ya mapumziko zamani ilikuwa ikiadhimishwa kwa wanafamilia kuimwagia maji sanamu ya Budha.

Watu wakimwagia manukato sanamu ya Buddha

Chanzo cha picha, EPA

Katika picha hii, watu wanainyunyizia maji sanamu ya Budha.

Zamani kurusha maji kulimaanisha kuosha mikosi ya mwaka uliopita.

Watu na ndovu wakichezea maji wakati wa tamasha la maji la Songkran.

Chanzo cha picha, Reuters

katika picha hii (juu) ndovu na watu wanaonekana wafukiza maji.

Watu wakicheza na maji kwa kutumia bastola za maji kuadhimisha tamasha la maji

Chanzo cha picha, Reuters

maelfu kwa maelfu ya watalii huenda thailand kila mwaka , hususan katika mji wa Bangkok na miji mingine kushuhudia tamasha la Songkran.

Watu wakimwagia manukato sanamu ya Buddha

Chanzo cha picha, EPA

Mshiriki akitumia bunduki ya maji kuadhimisha mwaka wa kibudha , unaofahamika nchini humo kama Songkran, mjini Bangkok tarehe 13 Aprili 2019.

Chanzo cha picha, AFP

Watu wengi hushiriki wakiwa wamevalia nguo zenye rangi mbali mbali za kuvutia katikasherehe hizi. Katika picha hii (chini) mvulana mdogo ameketi kwenye mabega ya mtu huku akicheza na maji akifyatua maji.

Mtot mdogo wa kiume akiwa kwenye mabega ya mtu huku akiwa ameshikilia bunduki ya maji

Chanzo cha picha, Reuters

Tarehe 15 Aprili, siku ya kwanza ya mwaka wa Thailand , watu hukusanyika katika mahekalu kutoa chakula na nguo mpya kwa watawa kama sadaka.

Washiriki wakitupa maji kwenye gari la mpita njia

Chanzo cha picha, AFP

katika picha hii (chini) watu wakimpiga maji mtu ambaye amelala chale sakafuni.

Watu wakimpiga maji mtu aliyelala chale sakafuni

Chanzo cha picha, Reuters

Picha zote zina hakimiliki