'Wakati wa masaji ghafla alianza kuwa mkorofi'

Idadi ya watoa huduma za kukanda mwili au masaji. majumbani inaonekana kuongezeka nchini Uingereza. Lakini BBC imegundua kuwa kumekuwa na ongezeko la visa vya unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na wataalamu wa matibabu ya masaji.
Hakuna leseni inayohitajika ili kuendesha biashara ya masaji nchini Uingereza. Watu wanaitaka serikali kudhibiti biashara hii na kukomesha mashambulizi hayo.
Onyo - Baadhi ya maelezo katika habari hii yanaweza kukukera
Calum Urquhart aliona tangazo la huduma ya masaji ya mtu huyu kwenye mitandao ya kijamii na akaomba nafasi ya kupata huduma ya masaji kwa Yas (jina limebadilishwa). Alisimulia yaliyomtokea. Mwanzoni, Calum alipewa ruhusa yake rasmi kwanza. Pia alimwomba ruhusa kwanza amguse sehemu fulani za mwili wake. Lakini kabla ya yeye kujua, alianza kumfanyia vitendo vibaya.
Nadhani sikujua la kufanya katika hali hiyo. Sikujua nini kilikuwa kinanipata. Sikuamini na akili yangu ya pili ilikuwa ikiniambia nisichukuie kupita kiasi. Aliambia BBC. Lakini alianza kuogopa. Hadi wakati huo nilikuwa najua kabisa kile kinachotokea kwangu. Sikujua kama angenibaka au kuniua kwa kweli sikujua.
Yas aliripoti tukio hilo kwa polisi. Ilibainika kuwa Calum hakuwa na sifa za kufanya hivi. Hakuwa na mafunzo ya tiba ya masaji. Polisi walianzisha uchunguzi, BBC iliripoti visa vya Callum kuwanyanyasa kingono baadhi ya wateja wakati uchunguzi ukiendelea na akiwa nje kwa dhamana baada ya kukamatwa.
Callum alikamatwa mwaka jana. Aliwanyanyasa kingono wateja wanne wa kike katika jiji la Bristol. Anasema amesikitishwa na tukio hilo. Kwa sababu hakukuwa na utaratibu wa kukomesha unyanyasaji wa wanawake hawa na watu kama Calum. Yas anahisi kwamba kama kungekuwa na udhibiti mkali, angekuwa chini ya uangalizi na ukatili ungekoma.
Anapaswa kuadhibiwa kwa kile alichofanya. Sababu ya kuripoti hii ni ili asimsumbue mtu yeyote katika siku zijazo.
Ukosefu wa udhibiti
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Bonyeza hapa kujiunga
Mwisho wa Whatsapp
Kwa sasa, hakuna leseni inayohitajika kufanya mazoezi ya matibabu ya masaji nchini Uingereza. Wala hakuna hitaji la kuwa na mafunzo rasmi. Kwa hivyo mtu yeyote anayetaka anaweza kujiita mtaalamu. Masaji au mtaalamu wa massage anatakiwa kuwa amesajiliwa na ofisi ya serikali. Lakini inasemwa kwamba usajili unapaswa kufanywa kwa hiari. Wataalamu wanasema kwamba kiwango cha usajili ni cha chini sana.
Ikiwa biashara ya masaji itaanzishwa katika jumba la kibiashara, baraza la manispaa au chombo kingine katika ngazi hiyo huweka sheria na ikiwa mahali ikakutwa si salama leseni itafutwa. Lakini kama vile wataalamu wengine katika mfumo wa afya kama vile physiotherapist wanasajiliwa, kuna mahitaji yanayoongezeka kutoka kwa umma kwamba wataalamu wa masaji wanapaswa pia kusajiliwa.
BBC imefahamu kutokana na uchunguzi kwamba kumekuwa na matukio kadhaa ya ubakaji au unyanyasaji wa kijinsia na watu wanaohusika na tasnia ya masaji katika kipindi cha miaka sita iliyopita. Cha kushangaza ni kwamba hata baada ya kukamatwa kwa kosa la unyanyasaji wa kijinsia wakati wa masaji, watu hao wamebainika kurudia uhalifu wa aina ileile wanapoachiliwa.
Yas anasema kuwa tukio hilo limeathiri sana akili yake. Sikulala kwa siku kadhaa. Kwa sababu niliogopa kwamba mambo haya yangekuja katika ndoto zangu. Kwa hiyo hata sikulala. Pia nilikuwa na mashambulizi ya hofu. Na kwa sababu hii nilianza kupoteza imani ndani yangu. Kwa sababu nilimruhusu mtu huyu kuja nyumbani kwangu. Kwa hivyo nilikuwa nikijiuliza ikiwa ninaweza kumwamini mtu yeyote tena.

Programu za Afya zimefanyika kwa njia kubwa na kuifanya iwe rahisi sana kuweka nafasi ya masaji majumbani. Wateja wanaweza kuomba nafasi kwa wataalamu wa masaji kuja majumbani mwao kwenye programu inayoitwa Urban.
Taylor (jina limebadilishwa) kila mara amekuwa akipendelea kupata masaji kutoka kwa mfanyabiashara wa kike anapoweka nafasi kupitia programu. Lakini alipotaka masaji ya misuli Oktoba 2019, hakukuwa na mtaalamu wa kike kwenye programu husika. Badala yake kulikuwa na wataalamu wa kiume ambaye alikuwa mamia ya maoni mazuri aliyokutwa ameandikiwa kwenye ukurasa wake ndani ya program. Wengine waliipa kazi yake alama ya nyota tano.
Nilidhani watu wengi walikadiria kazi ya mtu huyu vizuri. Anaweza pia kufanya kazi yangu ya masaji vizuri. Kwa hivyo Taylor aliweka miadi na mfanyabiashara huyo. Mtaalamu alikuja kwa wakati uliowekwa. Lakini baada ya muda, Taylor alianza kuhisi kuwa kila kitu hakikuwa sawa.
Wakati mtaalamu huyo mwenye ujuzi sana anafanya masaji, hakuna sehemu ya mwili iliyokuwa ikionekana lakini mtu huyu aliondoa taulo kwenye kiuno changu.
Kisha akaanza kunishika sehemu za siri bila ruhusa yangu. Kisha akaninyanyasa. Niliganda. Niliogopa ni nini kingine angefanya ikiwa ningekataa. Nilipomzuia kufanya haya yote, hakunisikiliza.
Aangua kulia
Alitoka nyumbani na mimi nikaanza kulia. Nilijifungia ndani ya nyumba. Taylor aliripoti tukio hilo kwa Kampuni ya Urban App na polisi. Polisi baadaye walifunga uchunguzi wa kesi hiyo kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa kutosha.
Kampuni ya Urban app ilisema kuwa mtu huyo ataondolewa kwenye huduma mara moja. Lakini wiki mbili baadaye, Taylor aligundua kuwa wasifu wake kwenye programu uliku bado upo na anafanyakazi.

Taylor aliambiwa kwamba jina lake lisingeonekana mara tu hitilafu ya kiufundi itakapotatuliwa, lakini BBC ilipothibitisha hilo, wasifu wa mfanyabiashara huyo ulikuwa bado unatumika miaka mitatu baadaye.
BBC iliuliza Kampuni ya Urban App kuhusu hili. Kampuni hiyo ilisema kuwa wasifu wa mtu huyo umeondolewa kabisa.
Wasifu wake unaweza kuonekana lakini wateja hawataweza kuweka miadi yake. Huduma ya wasifu imesimamishwa kwa wateja kufuatia malalamiko ya Taylor.
Mwanamke alibakwa na mtaalamu wa masaji kutoka kampuni ya mjini Cosmin Tutoach ambaye alipata nafasi kupitia programu hiyo. Alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela.
Kampuni ya programu ya Urban ilieleza kwamba ikiwa unataka kufanya kazi kama mtaalamu wa masaji, lazima upitie mchakato mkali sana wa uthibitishaji. Mwaka 2019, mfumo wa ukaguzi wa DBS ulitekelezwa. Kampuni hiyo ilisema kuwa kuna malalamiko kuhusu baadhi ya miadi. Kampuni pia ilifafanua kuwa kila malalamiko yanachukuliwa kwa uzito mkubwa na kufanyiwa kazi mara moja.
Kulingana na Yvonne Blake mwakilishi wa kitaalamu wa Baraza Kuu la Tiba za Masaji, kutokana kanuni za sasa, mtu yeyote anaweza kuanza kufanya kazi kama mtaalamu wa masaji bila uthibitisho wowote.
Blake amekuwa kama shahidi muhimu katika kesi ya unyanyasaji wa kijinsia. Mtu yeyote anaweza kuandika sifa zake. Wanahisi kwamba kuwe na mfumo wa kuangalia uhalisia wa habari hizo.
Tuliwasiliana na wafanyikazi wa serikali wanaofanya kazi katika idara za afya na viwanda kuhusu udhibiti wa tasnia hii. Lakini tuligundua kuwa kuna mkanganyiko juu ya nani hasa anahusika.
Akizungumza na BBC, msemaji huyo wa serikali alisema kuwa visa vya unyanyasaji wa kijinsia ni vya kutisha. Alitoa wito kwa waathirika kushiriki katika shughuli zinazotoa msaada wa suala hili. Polisi watachukua hatua dhidi ya watu wanaofanya unyanyasaji wa kijinsia kwa jina la masaji, lakini ikiwa kituo cha masaji sio salama, leseni iliyotolewa kwa kituo hicho inapaswa kufutwa.
Caroline Noakes, Mbunge wa Conservative ambaye anaongoza Kamati ya Wanawake na Usawa, ametaka hatua kali zaidi zichukuliwe katika kesi za unyanyasaji wa kijinsia kwa jina la masaji.
Kampuni ya Urban App imesema iwapo kutakuwa na udhibiti mkali kuhusu sheria na uhakiki wa tasnia ya masaji, tutaikaribisha.
Taylor alisema kwamba ni vigumu sana kwangu kutoka katika kumbukumbu hii chungu. Tukio hili lilinibadilisha. Mzigo wa tukio hili lisilofaa utabaki kichwani mwangu. "Sitawahi kuondoa nyakati hizo mabegani mwangu," Taylor alisema.















