Muhammadu Buhari: Maisha ya rais wa zamani wa Nigeria katika picha

Muhammadu Buhari sits in front of a Nigerian flag and signs that say United States Institute of Peace. He wears a black top, black cap and glasses.

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    • Author, Wedaeli Chibelushi
    • Nafasi, BBC News
  • Muda wa kusoma: Dakika 5

Maisha ya Muhammadu Buhari yaliangazia mabadiliko makubwa ya kisiasa nchini Nigeria katika miongo mitano iliyopita - na mara nyingi alijipata katikati ya matukio.

Rais huyo wa zamani wa Nigeria, ambaye alifariki Jumapili akiwa na umri wa miaka 82, alikua kiongozi wa kijeshi wa nchi hiyo baada ya mapinduzi, aliwahi kufungwa jela na utawala mpya wa kijeshi, kabla ajipange upya miongo kadhaa baadaye kushinda urais katika uchaguzi wa kidemokrasia.

Mara nyingi alipigwa picha akiwa amevaliamiwani nyeusi au miwani kubwa, yenye fremu nyeusi, kofia ya kitamaduni ya zanna na tabasamu kubwa, ambayo ilikuwa sehemu kubwa ya maisha ya Buhari yaliyoangaziwa hadharani.

A black and white photo shows Buhari wearing a suit and tie and standing besides King Gustaf and Sheikh Yamani

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Buhari - katika picha hii ya 1977 alikuwa na Mfalme wa Uswidi Sweden Carl XVI Gustaf na Sheikh Ahmed Zaki Yamani wa Saudi Arabia mwaka 1977 - alianza taaluma yake ya kijeshi punde alipotoka shule.

Wakati pich ahii ilipopigwa, Buhari alikuwa mepiga hatua nakupandishwa che hadi kuwa kamanda wa kijeshi wa kikanda.

Miaka kadhaa baadaye, mwaka1983, wanajeshi walimpindua rais Shehu Shagari aliyekuwa madarakani wakati huo .

Buhari, wearing a military uniform, stands at the back of an open top vehicle. Three other men in military gear are also in the car, which appears to be in an arena.

Chanzo cha picha, Sygma via Getty Images

Ingawa Buhari alishikilia nafasi ya kiongozi wa kijeshi, alipinga madai kwamba alipanga mapinduzi hayo, akisema kuwa aliwekwa madarakani na makamanda wa ngazi ya juu ambao walitaka mti atakayeshikilia nafasi hiyo kwa niaba yao. Hata hivyo madai ya Buhari kuwa na jukumu katika mapinduzi hayo ya kijeshi yaliibuka.

Baada ya kuongoza kwa mkono wa chuma kwa takriban miaka miwili, kukabiliana vikali dhidi ya ufisadi na ukiukwaji mbalimbali wa haki za binadamu, Buhari mwenyewe aliondolewa madarakani. Utawala mpya wa kijeshi ilimweka chini ya kizuizi cha nyumbani kwa miaka mitatu.

Mwaka 2003, baada ya kujitenga na siasa kwa miongo kadhaa, Buhari aliamua kutafuta nafasi nyingine ya kuongoza nchi.

Wakati huo, aliomba nafasi ya juu kupitia uchaguzi wa kidemokrasia - akigombea kupitia chama cha All Nigerian Peoples Party (ANPP).

Buhari, his running mate Chuba Okadigbo and Chairman of the All Nigerian Peoples Party Don Etiebet, smile and raise their joined hands above heads.

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Katika picha hii anaonekana (upande wa kulia) akiwa na mgombea mwenza wake Chuba Okadigbo (kushoto) pamoja na mwenyekiti wa ANPP Don Etiebet.

Buhari alishindwa uchaguzi huo na Olusegun Obasanjo mwaka 2003, na alijaribu tena kuwania urais mwaka 2007 na 2011 lakini hakufanikiwa.

Licha ya kushindwa huko aliendelea kujiimarisha kisiasa na kupata uungwaji mkono wa vijana kwa ahadi ya kukabiliana na ufisadi na ukosefu wa usalama.

Young protesters are in action on the streets of Kano - one holds a picture of Buhari aloft, a couple of others wield bits of wood. Grey smoke billows in the background.

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

At a packed rally, supporters clamour to touch Buhari, who stands above the crowd, smiling. He wears a blue top and blue hat.

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

A woman poses next to a poster of a smiling Buhari. She wears a grey top written "APC" and "Buhari".

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

An APC campaign billboard bears the words "we will defeat Boko Haram #EveryNigerianCounts". The words are accompanied by a picture of a soldier, in military fatigues, carrying a gun.

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Buhari alipata maarufu mkubwa katika eneo la kaskazini mwa Nigeria alikozaliwa

A makeshift figure of Buhari, bearing the words "Sai Baba Inshallah", stands in the middle of a dusty road. A motorbike zooms past.

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Katika bango lililo na picha yake katika mji wa Kaduna wakati wa uchaguzi wa mwaka 2015, linasomeka: wanyeji watampigia kura "Baba" tu ikimuashiria Buhari.

Buhari hatimaye alishinda uchaguzi wa 2015, na kumuondoa rais aliyekuwa madarakani wakati huo Goodluck Jonathan.

Aliandikisha historia ya kuwa kiongozi wa kwanza wa upinzani kuibuka mshindi katika uchaguzi mkuu.

Muhammadu Buhari, wearing a white long-sleeved top and a white cap, raises a mobile phone to his ear.

Chanzo cha picha, Red Media Africa

Baada ya hatimaye kuchukua hatmu ya uongozi, muhula wa kwanza wa Buhari ulikumbwa na msukosuko. Uchumi wa nchi ulidorora kwa mara ya kwanza katika muongo mmoja na mizozo ya usalama ikaongezeka.

Wakati mke wa Buhari - katika picha hapo chini - alipokosoa utawala wake hadharani, rais alionyesha kughadhabishwa kwake na kauli hiyo na kumjibu mke wake kuwa jukumu lake ni la jikoni.

Buhari akisimama kando ya mke wake.

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Licha ya kukabiliwa na changamoto katik amhula wake wa kwanza, Buhari alichaguliwa tena mwaka 2019.

Kama rais wa mojawapo ya mataifa ya Afrika yenye uchumi mkubwa , alisafiri duniani kote, akihudhuria mikutano ya hadhi ya hali ya juu na kukutana na wakuu wenzake wa nchi.

Buhari and Queen Elizabeth are pictured in conversation, smiling together. The Queen wears a blue suit jacket on top of a pink top, while Buhari wears a black jacket, white shirt and patterened hat.

Chanzo cha picha, John Stillwell/Getty Images

Buhari alilakiwa na Malkia Elizabeth katika mkutano wa viongozi wa Jumuiya ya Madola mnamo 2015.

Barack Obama is pictured, out of focus, looking at Buhari, who is speaking and staring straight ahead.

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Mapema mwaka wa 2015, alikaribishwa Ikulu ya White House na Rais wa wakati huo wa Marekani Barack Obama.

Donald Trump and Muhammadu Buhari - both in formal dress - in discussions while walking past some columns at the White House.

Chanzo cha picha, Getty Images

Na mnamo 2018, Buhari alikuwa kiongozi wa kwanza kutoka eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara kukutana na Rais Donald Trump huko Washington.

Mnamo 2015, Buhari alizuru India kwa mkutano wa kilele wa India na Afrika na akalakiwa na Waziri Mkuu Narendra Modi.

Chanzo cha picha, Hindustan Times via Getty Images

Maelezo ya picha, Mnamo 2015, Buhari alizuru India kwa mkutano wa kilele wa India na Afrika na akalakiwa na Waziri Mkuu Narendra Modi.

Kufuatia kifo chake, katika kliniki moja mjini London, Buhari anakumbukwa na baadhi ya watu kama mtu aliyevunja ahadi zake za kampeni na kuponda upinzani.

Kwa wengine, alikuwa bingwa wa utaratibu ambaye alijaribu kila awezalo kufiki amalengo yake katikati ya mfumo usiofanya kazi wa kisiasa.

Katika kumuenzi mpinzani wake wa zamani, Jonathan alimuelezea Buhari kama mtu ambaye "alijitolea katika kujitolea kwake kwa wajibu wake na alitumikia nchi kwa tabia na hisia kubwa ya uzalendo".

A person displays a newspaper carrying a headline reporting Muhammadu Buhari's death. Three men appear in the background of the image, out of focus.

Chanzo cha picha, Reuters