'Tumekuwa na mazungumzo mazuri na yenye tija na Putin kuhusu vita vya Ukraine'- Trump

Marekani inaishawishi Urusi ikubali kumaliza mzozo na Ukraine. Rais Putin wa Urusi amesema mzozo huo utakoma kwa masharti, masharti ambayo yanakosolewa na Ukraine.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Dinah Gahamanyi & Asha Juma & Mariam Mjahid

  1. 'Kuzuiwa kuingia Angola ni shambulizi dhidi ya Diplomasia na Demokrasia Afrika'- Masoud

    a

    Chanzo cha picha, ACT

    Kundi la vyama vya upinzani barani Afrika kupitia Jukwaa la Demokrasia Afrika (PAD), limetaja kitendo cha serikali ya Angola kuwazuia wanasiasa wakuu wa upinzani kutoka barani kote kuingia nchini humo ni shambulizi dhidi ya demokrasia

    Katika taarifa yao ya pamoja, limesema kitendo cha Mamlaka za Angola kuzuia karibu viongozi wakubwa wa upinzani karibu 40 kutoka nchi zaidi ya 20 ni kampeni ya kimfumo na ya kijinga ya kushambulia na kudhoofisha maendeleo kuelekea demokrasia na uwajibikaji barani Afrika.

    Viongozi hao walizuiwa katika uwanja wa ndege wa Luanda, wilipowasilia kushiriki katika mjadala wa siku nne wa Jukwaa la Demokrasia Afrika, yaliyoandaliwa na Taasisi ya The Brenthurst Foundation, ambayo yalianza Machi 13 na yatakamilika Machi 16.

    Baadhi ya viongozi waliozuiwa hapo jana, kunyanganywa hati zao za kusafiria na wengine kuzuiwa kwa zaidi ya masaa 9 kwenye uwanja huo wa ndege, ni pamoja na Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud, ambaye amelaani kitendo hicho.

    'Kitendo kile ni shambulio dhidi ya Diplomasia na Demokrasia Afrika', alisema Masoud.

    Mbali na kiongozi huyo ambaye ni mwenyekiti wa chama cha upinzani cha ACT Wazalendo Tanzania, alikuwepo pia rais wa zamani wa Botswana, Ian Khama, Waziri mkuu wa zamani wa Lesotho Moeketsi Majoro, rais wa zamani wa Colombia, Andrés Pastrana Arango na wapinzani wengine 24 ambar walishikiliwa kwa saa 9 kwenye uwanja huo.

    Wapinzani wengine waluozuiwa ni pamoja na mwenyekiti wa chama kikuu cha Upinzani Tanzania, CHADEMA, Tundu Lissu, Kiongozi wa upinzani Uganda, Robert Kyagulanyi (Bbobi Wine), na Seneta wa Nairobi, Edwin Sifuna.

    Wapo waliozuiwa kwa muda na kurudishwa katika nchi sao, kabla ya bade kuruhusiwa kuingia nchini humo.

    Mamlaka za Angola zinasema, kilichotokea ni masuala ya uhamiaji zikigusia kuhusu utaratibu wa vibali vya kuingia nchini humo vilivyopaswa kufuata utaratibu wa sheria.

  2. 'Tumekuwa na mazungumzo mazuri na yenye tija na Putin kuhusu vita vya Ukraine'- Trump

    s

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais Donald Trump wa Marekani anapongeza 'mijadala yenye tija' kati ya nchi yake na Urusi kuhusu vita ya Ukraine.

    Katika chapisho lake kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social, Donald Trump alisifu "majadiliano mazuri na yenye tija" kati ya Urusi na Marekani hapo jana. Hata hivyo anaonya maelfu ya wanajeshi wa Ukraine "wamezingirwa kabisa" na jeshi la Urusi, akisema wako katika "hali mbaya sana na dhaifu".

    Pia alifichua kuwa alimwomba Putin "alinde maisha yao", na kuongeza: "Haya yatakuwa mauaji ya kutisha" kwa kiwango "hayajaonekana tangu Vita vya Pili vya Dunia".

    Kwa upande wake Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky anamkosoa Putin kwa kuweka masharti ambayo 'yanarefusha' mchakato wa kusitisha mapigano. Katika dakika chache zilizopita, Rais Zelensky amesisitiza kwamba kurejea kwa wafungwa pamoja na usitishaji vita wa siku 30 "bila masharti" ni hatua mbili "za haraka" ambazo zinaweza kusogeza Ukraine karibu na "amani ya haki na ya kudumu".

    Katika chapisho kwenye mtandao wa X, rais wa Ukraine anaikosoa Urusi kwa "kuweka kwa makusudi masharti ambayo yanatatiza na kuondoa mchakato". Maoni yake yalifuatia mkutano wake na Kardinali Pietro Parolin, katibu wa Jimbo la Holy See.

  3. Mahakama yaamuru utawala wa Trump kuwarejesha kazini wafanyikazi waliowasimamisha kazi

    GG

    Chanzo cha picha, Reuters

    Majaji wawili wa Mahakama tofauti nchini Marekani wameamuru mamlaka za serikali kuwarejesha kazi wafanyikazi waliosimamishwa kazi mwezi jana na utawala wa Trump.

    Kwa mfano Carlifornia, Jaji William Alsup alitaja kufutwakwa wafanyikazi hawa kama unafiki wa kimpango unaonuia kupunguza wafanyakazi wa serikali.

    Uamuzi wake ambao ulifuatwa na wa mahakama ya Maryland unagusa wafanyakazi waliosimamishwa kazi katika idara kama vile ya ulinzi , Kawi, Hazina ya kitaifa na masuala mngine ya msingi.

    IIdara ya ahakama imesema kufutwa kazi kwa wafanyakazi hao n i kwa misingi y amiongozi licha ya kuwa ya maamuzi kutoka kwa Afisi ya kusimamia wafanyikazi nchini humo (OPM)

    BBC imetafuta maoni ya afisi ya OPM ambayo husimamia maslahi ya wafanyikazi wa seikali ambao wamekuwa wakimulikwa hata zaidi wakati huu Trump anaporejea madarakani.

    Akijibu uamuzi wa kwanza, msemaji wa Ikulu ya White House Karoline Leavitt alimshutumu Jaji Alsup kwa "kujaribu kunyakua mamlaka ya kuajiri na kufukuza kutoka kwa tawi la mtendaji kinyume na katiba". Alisema kuwa mamlaka yapo kwa Rais na "majaji wa mahakama ya wilaya pekee hawawezi kutumia vibaya mamlaka ya mahakama nzima kuzuia ajenda ya rais".

    "Utawala wa Trump utapigana mara moja dhidi ya amri hii ya kipuuzi na isiyo ya kikatiba," aliongeza.

    Jina la Elon Musk halikutajwa wakati wa kesi ya California, lakini amepewa jukumu na Rais Trump kupunguza wafanyikazi wa shirikisho kupitia Idara ya Ufanisi wa Serikali - au Doge.

    Ikulu ya White House imekanusha kuwa Musk ndiye kiongozi wa shirika hilo la DOGE , ingawa Trump alimtaja hivyo wakati wa hotuba yake ya Bunge la Congress wiki iliyopita.

    Soma pia:

  4. Waasi wadhibiti Ofisi ya Meya katika mji muhimu wa Ethiopia huku kukiongezeka wasiwasi wa vita kuzuka

    gg

    Chanzo cha picha, Amensisa Ifa / BBC

    Aundi la waasi la chama cha kisiasa kikuu cha kaskazini mwa Ethiopia ya Tigray kimeteka ofisi za meya na chombo cha habari cha redio cha mkoa huo, Mekelle, kukiwa na hofu ya kuzuka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe.

    Haya yanajiri kufuatia mvutano wa madarakani ndani ya Wanamgambo wa Tigray People's Liberation Front (TPLF), ambapo kumezua taharuki kwa kurejea uhalifu wa vita.

    Mkaazi mmoja wa Mekelle ameiambia BBC kuwa watu wameharakisha kutoa pesa walizokuwa wamehifadhi kwa benki wakihofia hali ya usalama kuzorota zaidi.

    Siku ya Jumanne ,kundi hilo liliteka eneo la Adigrat, mji wa pili mkuu wa Tigray.

    Getachew Reda, Rais wa utawala wa mpito wa Tigray, amelishutumu kundi pinzani, linaloongozwa na Debretsion Gebremichael, kwa kujaribu kumwondoa madarakani kwa nguvu.

    Getachew alikua kiongozi wa Tigray kufuatia makubaliano ya amani ya 2022 ambayo yalimaliza miaka miwili ya mzozo katika eneo hilo, ambayo iliua takriban watu 500,000.

    Debretsion Gebremichael hapo awali alikuwa kiongozi wa eneo hilo lakini katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, uhusiano ulidorora na mtu aliyechukua nafasi yake.

    Siku ya Alhamisi, wanachama wa mrengo wa Debretsion wakiandamana na wanajeshi waliojihami walichukua udhibiti wa kituo cha redio cha Mekelle FM na ofisi ya meya wa jiji hilo.

    Milio ya risasi ilisikika usiku wa kuamkia leo huko Adi-Gudem, mji ulio karibu na Mekelle, wakati vikosi vya waasi vilipojaribu kuteka jengo la serikali.

    Vikosi hivyo vimeripotiwa kumkamata meya wa mji huo na kuchukua udhibiti wa ofisi hiyo.

    Getachew amewasimamisha kazi majenerali watatu wa Kikosi cha Ulinzi cha Tigray, akishutumu kundi pinzani kwa kujaribu kuvuruga eneo hilo.

    Nchi kadhaa zikiwemo Marekani, Uingereza na Umoja wa Ulaya zimeonya kuhusu mvutano huo unaozidi kuongezeka, zikisema lazima "Vita visizuke tena".

    Siku ya Alhamisi, Ufaransa ilitoa wito kwa raia wake huko Tigray "kuhifadhi vifaa vya dharura na kuchukua tahadhari kubwa". Katika taarifa, Umoja wa Afrika ulisema unafuatilia matukio ya Tigray kwa "wasiwasi mkubwa".

    Soma pia:

  5. Kinda wa Arsenal Myles Lewis-Skelly, aitwa kikosi cha England, Rashford arejeshwa

    a

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Myles Lewis-Skelly,

    Mshambuliaji wa Aston Villa Marcus Rashford ametajwa kwenye kikosi ambacho ni cha kwanza cha Thomas Tuchel kama meneja wa timu ya taifa ya England. Rashford aliichezea England mara ya mwisho katika mechi ya kirafiki dhidi ya Brazil mnamo Machi 2024 lakini amekuwa na kiwango kizuri tangu ajiunge na Villa kwa mkopo kutoka Manchester United mnamo Januari.

    Mlinzi wa Newcastle Dan Burn na Myles Lewis-Skelly wa Arsenal wameitwa wa mara ya kwanza kwenye kikosi cha England, ambacho kinaanza kampeni ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2026, kwenye Uwanja wa Wembley wiki ijayo dhidi ya Albania na Latvia.

    Tuchel hajamuita kikosini kiungo kinda nota wa Arsenal, Ethan Nwaneri, lakini amemrejesha mtu mzima, kiungo wa Ajax Jordan Henderson katika kikosi chake cha wachezaji 26. Henderson, 34, alicheza mechi yake ya kwanza katika timu ya taifa chini ya meneja wa mwisho asiye Mwingereza - Fabio Capello - mnamo 2010 na alishiriki mara ya mwisho dhidi ya Malta mnamo Novemba 2023.

    s

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Rashford

    Kikosi kamili cha England

    Makipa: Dean Henderson (Crystal Palace), Jordan Pickford (Everton), Aaron Ramsdale (Southampton), James Trafford (Burnley)

    Mabeki: Dan Burn (Newcastle United), Levi Colwill (Chelsea), Marc Guehi (Crystal Palace), Reece James (Chelsea), Ezri Konsa (Aston Villa), Myles Lewis-Skelly (Arsenal), Tino Livramento (Newcastle United), Jarell Quansah (Liverpool), Kyle Walker (AC Milan, mkopo kutoka Manchester City)

    Viungo: Jude Bellingham (Real Madrid), Eberechi Eze (Crystal Palace), Jordan Henderson (Ajax), Curtis Jones (Liverpool), Cole Palmer (Chelsea), Declan Rice (Arsenal), Morgan Rogers (Aston Villa)

    Washambuliaji: Jarrod Bowen (West Ham United), Phil Foden (Manchester City), Anthony Gordon (Newcastle United), Harry Kane (Bayern Munich), Marcus Rashford (Aston Villa, kwa mkopo kutoka Manchester United), Dominic Solanke (Tottenham Hotspur)

  6. Msafara wa Rais Kenya wagonga na kuua raia wa Uingereza

    Edgar Charles Frederick aligongwa kwenye Barabara ya Ngong yenye shughuli nyingi ya Nairobi

    Chanzo cha picha, AFP

    Maelezo ya picha, Edgar Charles Frederick aligongwa kwenye Barabara ya Ngong yenye shughuli nyingi ya Nairobi

    Raia wa Uingereza mwenye umri wa miaka 79 Edgar Charles Frederick amegongwa na kuuawa na gari iliyokuwa miongoni mwa msafara wa Rais wa Kenya Wiliam Ruto jijini Nairobi siku ya Alhamisi.

    Maafisa wa polisi wamethibitisha kukamatwa kwa dereva wa gari hilo lililomgonga mtu huyo ambapo halikusimama baada ya kutşkea kwa ajali hiyo.

    Uchunguzi wa kina umeanzishwa huku dereva huyo akitarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka dhidi yake.

    Fredrick alikuwa nchini Kenya kumtembelea mpwa wake anayeishi nchini humo kabla ya kupatikana na mkasa huo. Familia yake tayari imefahamishwa kuhusu kifo chake.

    Ubalozi wa Uingereza umedokeza kuwa unafuatilia tukio hilo kupata taarifa zaidi.

    Video ambazo zimesambaa mitandaoni zimeonyesha mwanaume huyo akiwa amelala barabarani karibu na soko la Ngong, kisha baadaye akafunikwa na shuka ambalo hutumiwa na jamii ya maasai.

    Msemaji wa polisi nchini Kenya Michael Muchiri amesema gari hilo lilikuwa ni la usimamizi wa mkoa na lilikuwa likisindikiza msafara wa Rais ambaye amekuwa akifanya ziara za kukutana na wananchi jiji la Nairobi.

    Soma pia:

  7. Kukamatwa kwa Duterte kunatoa imani kubwa kwa ICC

    xcv

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Kukamatwa kwa aliyekuwa kiongozi wa Ufilipino, Rodrigo Duterte, kumetajwa kuwa hatua kubwa na ya wakati kwa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), ambayo inakabiliana na vikwazo kutoka kwa Marekani na uchunguzi wa tuhuma za unyanyasaji wa kingono dhidi ya mwendesha mashtaka wake.

    Duterte alikamatwa siku ya jumatano huko Manila kufuatia hati iliyotolewa na ICC na kupelekwa mjini The Hague.

    Atapelekwa mahakamani kwa mara ya kwanza siku ya Ijumaa.

    "Haya ni mabadiliko makubwa kwa sasa kuhusiana na uaminifu wa mahakama," alisema Danya Chaikel, mwakilishi wa shirika la haki za binadamu FIDH.

    Waendesha mashtaka katika mahakama ya kudumu ya kivita wanamshutumu Duterte mwenye umri wa miaka 79 kwa kuunda na kuvipatia silaha vikosi vya vinavyohusishwa na mauaji ya maelfu ya watumiaji na wauzaji wa madawa ya kulevya wakati wa utawala wake.

    Duterte, akizungumza katika video iliyochapishwa katika mitandao ya kijamii, alisema aliwajibika kikamilifu katika "vita dhidi ya dawa za kulevya."

    Mawakili wa mashtaka katika ICC wanakusudia kumfungulia mashtaka ya uhalifu dhidi ya ubinadamu kwa mashambulizi dhidi ya raia.

    Soma Pia;

  8. Mahakama Kuu nchini Kenya yabariki kung'olewa kwa Gavana Mwangaza wa Meru

    gg

    Mahakama kuu ya Kenya imeamua kuwa Bunge la Seneti nchini Kenya ilifuata sheria katika utaratibu wa kumng’oa mamlakani Gavana wa kaunti ya Meru Kawira Mwangaza.

    Mahakama hiyo imetupilia mbali madai yake kuwa kung’atuliwa kwake mamlakani hakukufuata sheria ikitaja kuwa alishindwa kuwashilisha ushahidi wa kutosha kujitetea.

    ‘’ Mahakama hii imekuta kuwa ombi lililowasilishwa haikuwa na msingi na kuifuta.Notisi ya gazeti rasmi iliyochapishwa tarehe 21 mwezi Agosti 2024 kumuondoa mamlakani Gavana wa Meru imeidhinishwa,’’ hakimu Bahati Mwamuye aamua.

    Mahakama hiyo pia iliagiza utaratibu wa katiba ufuatwe kuhusu kujazwa kwa pengo lililoachwa kulingana na muda unaofaa.

    Zaidi ya hayo, Mahakama imesema Seneti haikukiuka uamuzi wa mahakama wakati wa kung’atuliwa kwa Gavana wa Meru.

    Mwangaza alidai kuwa bunge la seneti lliendelea kujadili na kuamua kumuondoa madarakani licha ya mahakama kusitisha mchakato huo.

    ‘’ Bunge la Seneti halingeweza kukiuka maagizo ya mahakama ambayo hayakuwasilisha kama ilivyohitajika,’ uamuzi ulisema.

    .Mahakama imesema iwapo Mwangaza angetaka kusitisha mchakato wa kuondolewa kwake mamlakani angefuata utaratibu hitajika.

    Na kuhusu ukusanyaji maoni ya umma, Mahakama imekiri kuwa ni kigezo cha katiba lakini ikaelezea kwa kina kuwa mchakato huo hufanyika katika ngazi ya kaunti na sio katika ngazi ya bunge la Seneti.

    Mahakama haikupata ushahidi wowote kwamba alinyimwa muda wa kuzungumza na ilibainisha kuwa timu yake ya wanasheria haikuleta pingamizi lolote kuhusu muda uliotengwa kwa ajili ya utetezi wake.

    Kwa hivyo, ilihitimisha kuwa mahitaji ya utaratibu wa mashtaka yametimizwa.

    Hii ilikuwa ni mara ya tatu kwa Mwangaza kung'olewa madarakani kufikia Seneti tangu achaguliwe afisini Agosti 2022.

    Kesi ya kwanza ya mashtaka ilisikilizwa na kuamuliwa na kamati, lakini ya pili na ya tatu ilikwenda kwa njia ya kikao.

    Mashtaka dhidi ya gavana huyo wa kike yalikuwa kama vile matumizi mabaya ya mamlaka na ubadhirifu wa rasilimali za kaunti.

    Tangu kuchaguliwa kwake, Gavana Mwangaza amekuwa akivutana na wawakilishi wadi na viongozi wengine wa kaunti ya Meru huku akidai yanayomsibu ni taasubi za kiume ambazo anazitaja zimekolea kaunti ya Meru.

    Hadi sasa, haijajulikana ikiwa Gavana Mwangaza atakata rufaa dhidi ya uamuzi huo au la.

    Soma pia:

  9. Rais wa Syria atia saini azimio la katiba itakayotumiwa kipindi cha mpito

    gg

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais mteule wa Syria Ahmed al-Sharaa ametia Saini katiba ya uamuzi ambayo itakuwa ikifuatwa katika kipindi hiki cha mpito cha miaka mitano.

    Saini hiyo ikiwa na maana kuwa nchi ya Syria itakuwa ikifuata sheria za kiislamu.

    Kulingana na nakala hiyo imesema kuwa Uislamu ndio dini ya Rais, kama vile katiba ya awali ilivyokuwa na kufuata sharia za kiislamu ni "chanzo kikuu cha sheria", badala ya "chanzo kikuu", kulingana na kamati iliyobuni azimio hiyo.

    Pia katiba hiyo imegawanya mamlaka na uhuru wa mahakama na imetoa hakikisho la kutekeleza haki za wanawake, uhuru wa kujieleza na uhuru wa vyombo vya habari.

    Katiba hiyo pia imepatia Rais mamlaka ya kutangaza hali ya dharura.

    Na kuhusu bunge la wananchi, bunge mpya itakuwa na jukumu la kutunga sheria, theluthi mbili ya wabunge watateuliwa na kamati iliyoidhinishwa na Rais na theluthi moja itachaguliwa na Rais moja kwa moja.

    Kupitia azimio hili la Syria, wabunge hawawezi kumuondoa Rais madarakani na pia Rais hana mamlaka ya kumfuta mbunge kazi.

    Mamlaka ya kiutendaji itakuwa ni ya Rais mteule kipindi hiki cha mpito.

    Hata hivyo mamlaka inayoongozwa na wakurdi inayotawala Kaskazini Mashariki mwa Syria imekosoa vikali azimio ya katiba, ikidai, inaenda kinyume na uhalisia wa Syria wa kuwepo kwa jamii mseto.’’

    Haya yakijiri Marekani na Ulaya imekuwa ikisita kutoa vikwazo vya misaada walivyoviweka wakati wa utawala wa Assad hadi pale watahisi serikali mpya itaunda serikali jumuishi na kulinda walio wachache Syria.

    Soma pia:

  10. Mtoto, 8, aliyebakwa afariki dunia na kusababisha maandamano Bangladesh

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mtoto wa miaka minane ambaye alibakwa nchini Bangladesh amefariki dunia kutokana na majeraha aliyopata siku ya Alhamisi, na kusababisha maandamano makubwa kote nchini humo.

    Msichana huyo alibakwa alipomtembelea dadake mkubwa katika jiji la Magura, kulingana na kesi iliyowasilishwa na mamake.

    Mume wa dada huyo mkubwa mwenye umri wa miaka 18, pamoja na wazazi wake na kaka yake, walikamatwa na kuwekwa rumande.

    Usiku wa kuamkia Alhamisi, baada ya kusikia taarifa za kifo cha mtoto huyo, kundi la watu wenye hasira walikenda kwenye nyumba inayodaiwa kutokea tukio hilo na kuiteketeza kwa moto.

  11. Sudan yapiga marufuku bidhaa zote zinazoingia kutoka Kenya

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Wizara ya Biashara na Ugavi ya Sudan imepiga marufuku mara moja bidhaa zote zinazoingizwa nchini humo kutoka Kenya ikisema kuwa ni kutokana na suala la wasiwasi wa usalama wa kitaifa juu ya Kenya kuunga mkono vikosi vya Rapid Support Forces (RSF), wanachokishtumu kwa kujaribu kuanzisha serikali mbadala.

    ‘’Uagizaji wa bidhaa zote zinazoingia kutoka Kenya kupitia bandari zote, vivuko na viwanja vya ndege utasimamishwa kuanzia leo hadi siku isiyojulikana,’’ Agizo hilo lilitiwa saini na kaimu Waziri wa Biashara Omar Ahmed Mohamed.

    Sudan ilitangaza kuwa itachukua hatua kali dhidi ya serikali ya Kenya kwa kukaribisha vikosi vya RSF jijini Nairobi kufanya mkutano wao.

    Hata hivyo, Kenya ilijitetea kuwa haijakiuka Mkataba wa Umoja wa Mataifa, misingi ya Umoja wa Afrika wala Mkataba wa kuzuia uhalifu wa Kimbari kama inavyodaiwa na Sudan.

    "Msimamo wa Kenya uko wazi: tunatoa nafasi ya mazungumzo, bila kuchukua upande wowote, kwa sababu tunaamini katika uwezo wa mazungumzo ya amani kutatua mizozo ya kisiasa," ilisema taarifa ya Kenya.

    Kenya ambayo imekosolewa kwa kuruhusu RSF ilisema lengo lake ni kutoa fursa kwa vikosi vya RSF pamoja na mashirika ya kiraia ya Sudan kujadili na kutafuta njia ya kurudisha utawala wa kiraia nchini Sudan.

    ‘’Tuna imani kwamba watu wa Sudan wataweza kupata suluhu ya haraka na endelevu kwa mgogoro huu,’’ tamko la serikali ya Kenya ilieeleza.

    Soma zaidi:

  12. Hakimu wa UN apatikana na hatia ya kumlazimisha mwanamke kufanya kazi kama mtumwa

    h

    Chanzo cha picha, PA Media

    Maelezo ya picha, Lydia Mugambe ni jaji wa Umoja wa Mataifa na Mahakama Kuu

    Jaji wa Umoja wa Mataifa amepatikana na hatia ya kumlazimisha msichana kufanya kazi kama mtumwa.

    Waendesha mashtaka walisema Lydia Mugambe "alitumia nafasi ya hadhi yake" kumzuia kufanya kazi ya kudumu huku akimlazimisha kufanya kazi kama mjakazi wake na kukuwahudumia watoto bure.

    Mzee huyo mwenye umri wa miaka 49, ambaye pia ni jaji wa Mahakama Kuu nchini Uganda, alipatikana na hatia ya kula njama kuwezesha utekelezaji wa uvunjaji wa sheria ya uhamiaji ya Uingereza, kurahisisha safari kwa nia ya unyonyaji, kulazimisha mtu kufanya kazi, na kula njama ya kumtisha shahidi.

    Atahukumiwa katika Mahakama ya Oxford mnamo Mei 2.

    Soma zaidi:

  13. DRC: Kesi ya maafisa wakuu watano wanaohusishwa na kutekwa kwa mji wa Goma imeanza

    .

    Chanzo cha picha, Moise Niyonzima / EPA

    Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo imeanza kesi ya maafisa watano wakuu wa jeshi na polisi katika mji mkuu Kinshasa.

    Maafisa hao wanalaumiwa kwa jiji la Goma, mji mkuu wa mkoa wa Kivu Kaskazini uliotekwa na M23 mnamo mwezi Januari.

    Wanajeshi watatu na makamishna wawili wa polisi walikuwa wamefanya kazi kwa karibu na Gavana wa Jeshi la Kivu Kaskazini, katika DRC ya Mashariki kabla ya mji huo kuanguka mikononi mwa waasi wa M23.

    Katika mahakama kuu ya jeshi, maafisa hao watano walishtakiwa kwa woga. Mwendesha mashtaka wa kijeshi alidai hatua zao zilisababisha upotezaji wa vifaa vya jeshi, na dhuluma zilizofanywa na wanajeshi.

    Ufunguzi wa kesi hiyo ilikuwa moja kwa moja kwenye Runinga ya kitaifa, lakini mahakama kuu ya jeshi ilitangaza kwamba kesi iliyobaki itakuwa nyuma ya pazia, kuzuia kuenea kwa siri za ulinzi na usalama.

    Maafisa wa Jeshi ni Meja Jenerali Alengbia Nzambe ambaye aliongoza mkoa wa 34 wa North-Kivu, Brigadier Jenerali Danny Yangba, ambaye alikuwa mshauri mwandamizi wa jeshi anayesimamia shughuli za intelijensia ya usalama, na agizo la umma; na Brigadier General Papy Lupembe, ambaye aliongoza Brigade ya 11 kutoka mji wa Sake hadi Kitchanga, huko kaskazini-kivu.

    Maafisa wa polisi ni Romuald Ekuka, Naibu wa Polisi-Gavana wa Mkoa wa Kivu Kaskazini na Eddy MuKUna, kamishna msaidizi wa Idara.

    Bado hawajatoa lolote.

    Wakati M23 inaendelea kukamata miji zaidi katika mkoa wa mashariki wa majimbo ya Kaskazini na Kusini, maafisa wa ulinzi na usalama wanalaumiwa kwa kuacha silaha, risasi, pamoja na wanajeshi waliojeruhiwa.

    Mwisho wa Februari, wanajeshi 55 walihukumiwa kifo baada ya kupatikana na hatia na mahakama ya kijeshi ya Butembo kwa woga, uporaji na upotezaji wa vifaa vya jeshi.

    Soma zaidi:

  14. Wataalamu wa Umoja wa Mataifa waishutumu Israel kwa unyanyasaji wa kingono na 'vitendo vya mauaji ya halaiki' Gaza

    g

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Tume ya uchunguzi inadai kuwa vikosi vya Israel vilishambulia kwa makusudi kliniki ya al-Basma IVF katika mji wa Gaza.

    Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wameishutumu Israel kwa kuzidi kutumia unyanyasaji wa kingono na kijinsia dhidi ya Wapalestina na kutekeleza "vitendo vya mauaji ya halaiki" kupitia uharibifu wa utaratibu wa vituo vya afya ya uzazi na uzazi.

    Ripoti iliyoidhinishwa na Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa inaandika madai ya ukiukaji, ikiwa ni pamoja na ubakaji, huko Gaza na Ukingo wa Magharibi unaokaliwa tangu shambulio la Hamas la 7 Oktoba 2023 lililoanzisha vita vya Israeli dhidi ya Gaza.

    Pia inasema kuharibiwa kwa wodi za uzazi huko Gaza na viinitete katika kliniki ya uzazi kunaweza kuonyesha mkakati wa kuzuia uzazi miongoni mwa kundi fulani - mojawapo ya ufafanuzi wa kisheria wa mauaji ya kimbari.

    Israel ilisema "inakataa kabisa madai hayo yasiyo na msingi".

    Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alijibu kwa hasira, na kulitaja Baraza la Haki za Kibinadamu "kikundi kisichochukia Wayahudi, kilichooza, kinachounga mkono ugaidi na kisichohusika".

    Badala ya kuzungumzia kuhusu uhalifu wa kivita unaofanywa na Hamas, alisema, ilikuwa ikishambulia Israel kwa "mashtaka ya uongo".

    Unaweza pia kusoma:

  15. Putin aweka masharti ya kusitisha mapigano Ukraine

    G

    Chanzo cha picha, EPA

    Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema kuwa anakubaliana na wazo la kusitisha mapigano nchini Ukraine, lakini "maswali" yanabakia kuhusu asili ya mapatano huku akiweka masharti kadhaa magumu.

    Rais wa Urusi alikuwa akijibu swali kuhusu mpango wa kusitisha mapigano kwa siku 30 , ambao Ukraine iliukubali mapema wiki hii baada ya mazungumzo na Marekani.

    Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alielezea jibu la Putin kwa mpango huo kama "ujanja" na kutoa wito wa vikwazo zaidi kwa Urusi.

    Wakati huo huo, Marekani iliweka vikwazo zaidi kwa sekta ya mafuta ya Urusi, gesi na benki.

    Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mjini Moscow siku ya Alhamisi, Putin alisema kuhusu pendekezo la kusitisha mapigano: "Wazo hilo ni sawa na tunaliunga mkono, lakini kuna maswali ambayo tunahitaji kujadili."

    Kusitishwa kwa mapigano kunapaswa kusababisha "amani ya kudumu na kuondoa sababu kuu za mgogoro huu," Putin alisema.

    "Tunahitaji kujadiliana na wenzetu wa Marekani na washirika," alisema. "Labda nitapigiwa simu na Donald Trump."

    Putin aliongeza: "Itakuwa vyema kwa upande wa Ukraine kufikia usitishaji vita wa siku 30.

    Unaweza kusoma;

  16. Hujambo na karibu kwa matangazo haya ya mubashara ya Ijumaa tarehe 14.03.2025, tukikuletea habari za kikanda na kimataifa