Gavana wa zamani wa DRC atiwa nguvuni kwa tuhuma za ubadhilifu wa mali ya umma

Mutubuana

Chanzo cha picha, AtouMatubuana/Twitter

Maelezo ya picha, Kagana wa zamani wa Kongo Central alionekana akikokotwa na polisi kwenye mitaa ya mji wa Kinshasa, hukukundi la watu wakifuata nyuma wakati alipokamatwa
Muda wa kusoma: Dakika 2

Gavana wa zamani wa Jimbo la Kongo Central katika Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Atou Matubuana amekamatwa Jumamosi mjini Kinshasa.

Mahakama ya mwanzo ilikuwa tayari imetoa kibali cha kumkamata (arrest warrant) ,

Gavana huyu ambaye alikuwa anaongoza jimbo la Kongo Central ambalo limekuwa miongoni mwa majimbo yaliochangia pakubwa katika mfuko wa serikali, alitumiwa na mkaguzi mkuu wa maswala ya fedha kwa ubadhirifu wa mamilioni ya pesa. Kwa takriban miezi minne iliyopita, Bw Matubuana alifahamishwa kuhusu tuhuma dhidi yake lakini alishindwa kujisalimisha kwenye mahakama.

Maafisa wa polisi wa mahakama ambao hawakuwa wamevalia sare za kazi, walionekana kwenye video wakimkokota kwa nguvu Bwa Mutubuana kwenye mitaa, huku umati wa watu ukiwafuata nyuma.

Video ya tukio hilo imesambazwa na watu mbali mbali kwenye mitandao ya kijamii:

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Taasisi ya ukaguzi wa fedha za umma nchini Congo/Kinshasa (IGF) ilibaini ubadhilifu wa mali ya umma dhidi ya gavana huyo, baada ya kufanya ukaguzi katika jimbo la Kongo Central na ilikuwa tayari imechukua hatua za kisheria dhidi yake.

Ripoti ya afisa wa polisi wa mahakama katika alimhusisha Gavana Atou Matubuana Nkuluki na uadhilifu wa pesa za DRC 6,116,626,205(sawa na dola 3,058,313 , ambazo baadhi yake zilitolewa benki bila nyaraka kutoka kwa mfuko wa kusaidia shuguli za maendeleo ya kiuchumi, kijamii , sayansi na utamaduni , mfuko wa kukabiliana na majanga asilia na ajali, na pesa za usafi.

Mkuu wake wa wafanyakazi , Nzeza zi Ngeti, hakuwahi kuhamishwa tangu ufichuzi wa IGF ulipofayika.

Watu wengine waliotajwa kuhusiana na sakata hiyo ni pamoja na Mhasibu mkuu wa umma wa jimbo, naibu gavana, na Katibu binafsi wa gavana ambaye hajulikani alipo.