Virusi vya corona: WHO yaomba Tanzania kutoa takwimu ya walioambukizwa corona

Chanzo cha picha, AFP
Shirika la Afya Duniani WHO, kwa mara nyingine tena limetoa wito kwa mamlaka nchini Tanzania kuanza kutoa takwimu za watu waliambukizwa ugonjwa wa Covid 19 likisema itasaidia kuwakinga Watanzania na wale wanaotangamana nao.
Hii sio mara ya kwanza WHO limetoa ombi hili tangu serikali ilipoacha kutoa takwimu ya maambukizi ya Covid 19 na idadi ya vifo vilivyotokana na ugonjwa huo.
Katika taarifa yake ya hivi punde kuhusu mwenendo wa Covid 19 nchini Tanzania, shirika hilo lilielelezea wasi wasi wake kuhusu idadi ya wasafiri wa Tanzania waliopatikana na kuwa na virusi vya corona.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
Huku hayo yakijiri, Waziri Mkuu wa Tanzania Kasim Majaaliwa ametoa wito kwa watu kuchukua tahadhari dhidi ya kueneza virusi vya corona kwa kuzingatia muongozo wa afya uliyowekwa ikiwa ni pamoja na kuvalia barakoa.
Bw. Majaaliwa alisema hayo katika ibada ya mazishi ya katibu mkuu kiongozi mhandisi Balozi John Kijazi aliyefariki Jumatano kutokana na ugonjwa ambao chanzo chake hakikutajwa.
Leo ni siku ya mwisho ya maombi yaliyotangazwana Rais John Magufuli kupitia ombi alilotoa kwa viongozi wa kidini kufanya ibada maalum ya kulinda nchi dhidi ya kuenea kwa virusi vya corona
Mapema mwaka jana, rais pia alitoa wito kama huo wa maombi ya siku tatu kwa taifa na baadaye kutangaza kuwa taifa limefanikiwa kukabiliana na Covid 19.










