Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 03.05.2019: Hazard, Mata, Sessegnon, Wan-Bissaka, Danilo

Chanzo cha picha, Getty Images
Real Madrid inaamini kwamba itamsaini kungo wa Chelsea na raia wa Ubelgiji Eden Hazard, 28, punde tu msimu huu unapokwisha. (Marca)
Manchester United imemuongezea kiungo wa kati wa Uhispania Juan Mata, kandarasi ya mwaka mmoja huku ikiahidi kumuongezea tena mwaka mmoja wa ziada na inatumai kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 atasalia katika klabu hiyo. (Manchester Evening News)
Mchezaji wa Fulham Ryan Sessegnon, 18, anatarajia kujiunga na Tottenham mwisho wa msimu huu . (Mail)

Beki wa Crystal Palace Aaron Wan-Bissaka, 21, anasisitiza kuwa atasalia katika klabu hyo msimu ujao licha ya kuivutia klabu ya Manchester United. (London Evening Standard)
Beki wa Manchester City na Brazil Danilo, 27, amekubali kuandikisha mkataba wa kati ya miaka minne na mitano katika klabu ya Inter Milan ulio na thamani ya Yuro 3.5m kwa mwaka. (Gazetta dello Sport, via Manchester Evening News)
Beki wa Ajax na Uholanzi Matthijs de Ligt, 19, ana hamu ya kujiunga na klabu neyngine licha ya mazungumzo ya kuhamia Barcelona. (Mirror)

Atletico Madrid wamewasiliana na mchezaji wa Manchester City Nicolas Otamendi kuhusu uhamisho wa beki huyo wa Argentina mwenye umri wa miaka 31. (AS)
Manchester United inashindana na Juventus kumsaini beki wa Benfica na Ureno Ruben Dias, 21. (Record, via Manchester Evening News)
Arsenal imemuongeza beki wa Getafe Djene katika orodha yao ya wachezaji inayowamezea mate mwisho wa msimu huu . (Marca, via Mirror)
Qatar inafikiria kuhusu ushirikino wao na klabu ya Ufaransa Paris St-Germain baada ya klabu hiyo kufeli kupiga hatua zozote katika kombe la vilabu bingwa pamoja na matokeo mabaya katika fainali ya kombe la Ufaransa. (Le Parisien, via AS)

Crystal Palace na Burnley itamsaini winga wa Cardiff na Uingereza Josh Murphy, 24, iwapo klabu hiyo itashushwa daraja la ligi kuu ya Uingereza . (Football Insider, via Wales Online)
Mkufunzi wa Everton Marco Silva amepongeza tabia ya kiungo wa kati wa Senegal Idrisa Gueye, 29, ambaye alinyimwa uhamisho wa kuelekea Paris St-Germain mwezi Januari. (Liverpool Echo)
Winga wa Liverpool Ryan Kent, 22, aliyepo katika mkopo katika klabu ya Rangers, amethibitisha hamu yake kuondoka katika klabu ya Anfield , huku klabu hiyo ya Uskochi ikiwa na hamu ya kumsaini kwa kandarasi ya kudumu. (Express)

Mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich hana hamu ya kuiuza klabu hiyo licha ya uvumi unaomuhusisha Muingereza tajiri Sir Jim Ratcliffe. (ESPN)
Mchezaji wa Chile Guillermo Maripan, 24, ambaye analengwa na West Ham, hatauzwa na Alavez mwisho wa msimu huu . (AS, via Inside Futbol)
Mkufunziwa zamani wa Everton, Manchester United na West Ham David Moyes angepenedelea kuifunza klabu badala ya timu ya taifa huku kukiwa na uvumi wa meneja huyo kuifunza timu ya taifa la Uskochi ama klabu ya Celtic. (Talksport
TETESI ZA SOKA ALHAMISI

Chanzo cha picha, Getty Images
Kiungo wa kati wa Tottenham Christian Eriksen, 27, amekubali kujiunga na Real Madrid japo hajasaini mkataba. (AS)
Menyekiti wa Spurs Daniel Levy huenda akaitisha pauni milioni £128 kumuuza kiungo huyo wa kimataifa wa Denmark. (Mirror)
Manchester United wameongeza juhudi za kuwanunua wachezaji wawili wa Urenos - mshambuliaji wa Benfica Joao Felix, 19, na kiungo wakati Bruno Fernandes, 24. (London Evening Standard)
Real nao huenda wakasubiri hadi mwaka 2020 kumsaini Eriksen kwa uhamisho wa bure. (Sun)

Chanzo cha picha, Getty Images
Mlizi wa zamani wa United Rio Ferdinand amefanya mazungumzo ya kina na klabu hi ya Old Trafford kuhusu hatua ya kufanyia marekebisho safu ya ufundi ambayo imemfurahisha naibu mwenyekiti mkuu Ed Woodward huku akipigiwa upatu kuwania wadhifa wa mkurugenzi wa kiufundia. (Manchester Evening News)
Meneja Ole Gunnar Solskjaer anatarajiwa kumteu Mike Phelan kama mkurugenzi wa kwanza wa kiufundi. (Times - subscription required)
Kiungo wa kati wa Arsenal na Ujerumani Mesut Ozil, 30, anasisitiza kuwa anaridhia kuwa katika klabu hiyo na kwamba anatazamia kuendelea kuwa nao msimu ujao. (Sky Sports)

Chanzo cha picha, Getty Images
Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino huenda akakabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa vilabu vingine vya Uingereza katika soko la uhamisho wa wachezaji msimu huu wa joto. (Telegraph)
Kiungo wa kati wa Chelsea na Ubelgiji katika kikosi cha wachezaji wa chini ya miaka 21 Charly Musonda, an matumaini ya kurejea klabu ya Vitesse msimu ujao. (Inside Futbol)
Manchester United wako tayari kumjumuisha katika kikosi cha kwanza mlinzi wa England Axel Tuanzebe, ambaye yuko Aston Villa kwa mkopo. (Mail)

Chanzo cha picha, Getty Images
Mwenyekiti wa Crystal Palace na mmiliki mwenza wa klabu hiyo Steve Parish amewahakikishia mashabiki kuwa "hatapumzika" hadi kiwango cha mchezo wao kiimarike, hali ambayo itaongeza idadi ya mashabiki katika uwanja wa Selhurst Park kutoka 26,000 hadi 34,000. (London Evening Standard)
Mlinzi wa zamani wa Arsenal abriel Paulista, 28, ambaye anajiandaa kukutana na klabu yake ya zamani katika nusu fainalii ya ligi ya Europa na anasisitiza kuwa hana chochote cha"kuthibitishia" Gunners. (Independent)
Tetesi Bora Jumatano
Real Madrid haijajiandaa kumlipa mshahara wa £290,000 kwa wiki kiungo wa kati wa Man United Paul Pogba na kwamba mchezaji huyo atalazimika kuchukua kiwango cha chini iwapo anataka kujiunga na miamba hiyo ya Uhispania. (ESPN)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kiungo wa kati wa Manchester City Bernardo Silva, 24, anasema kwamba hajafikiria kuondoka katika ligi ya Premia , licha ya ripoti zinazomuhusisha na mabingwa wa Uhispania Barcelona. (Manchester Evening News)













