Tetesi za soka Ulaya Jumatano 01.05.2019: Pogba, De Ligt, Silva, Chilwell, Sessegnon

Chanzo cha picha, Getty Images
Real Madrid haijajiandaa kumlipa mshahara wa £290,000 kwa wiki kiungo wa kati wa Man United Paul Pogba na kwamba mchezaji huyo atalazimika kuchukua kiwango cha chini iwapo anataka kujiunga na miamba hiyo ya Uhispania. (ESPN)
Beki wa Ajax Matthijs de Ligt, 19, anataka kujiunga na mwenzake Frenkie de Jong katika klabu ya at Barcelona msimu ujao lakini Ajenti Mino Raiola angependelea mchezaji huyo kujiunga na Man United , Juventus ama Bayern Munich. (Mundo Deportivo)

Kiungo wa kati wa Manchester City Bernardo Silva, 24, anasema kwamba hajafikiria kuondoka katika ligi ya Premia , licha ya ripoti zinazomuhusisha na mabingwa wa Uhispania Barcelona. (Manchester Evening News)
Arsenal wameambiwa watalazimika kulipa kitita cha £17.2m ili kumsaini mshambuliaji wa PSG ,21, Christopher Nkunku . (Evening Standard)
Manchester City haitamwania beki wa kushoto wa Leicester City na Uingereza Ben Chilwell, 22, kwa sababu wanawamiliki wachezaji mbadala Benjamin Mendy na Oleksandr Zinchenko. (Manchester Evening News)

Tottenham wanaongoza harakati za kumsajili kijana wa Fulham Ryan Sessegnon, ambaye pia anazivutia klabu za Paris St-Germain, Juventus na Borussia Dortmund baada ya klabu hiyo kushushwa daraja kutoka ligi ya Premia. (Evening Standard)
Inter Milan inajianda kumnunua beki wa Man United Matteo Darmian, 29, kurudi Itali , huku klabu hiyo ya Uingereza ikiwa tayari kumuachilia kwa chini ya dau la £9m. (Gazzetta dello Sport, via the Sun)
Kiungo wa kati wa Chelsea aliyeko katika mkopo katika klabu ya AC Milan Tiemoue Bakayoko, 24, anataka kurudi katika uwanja wa Stamford Bridge - na kutoongeza kandarasi yake na mabingwa hao wa Setrie A baada ya kurushiwa maneno ya kibaguzi nchini Itali. (La Republicca, via the Sun)

Mkufunzi wa klabu ya Rangers Steven Gerrard anamtaka mshambuliaji wa Watford Andre Gray, 27, kuongoza kikosi chake kuwania taji la ligi ya uskochi msimu ujao na klabu hiyo ya ibrox itajaribu kumnunua kwa mkopo. (The Herald)
Mkufunzi wa West Ham Mauricio Pellegrini amemtaja beki wa kati wa klabu ya Alaves Guillermo Maripan, 24, na beki wa kushoto wa Olympiakos Leonardo Koutris, 23, kama mchezaji wanayemlenga kuimarisha safu ya ulinzi (Football.London)

Chanzo cha picha, Getty Images
Beki wa Crystal Palace Mamadou Sakho, 29, amesema kuwa huenda akaondoka katika klabu hiyo baada ya kusema kwamba anataka kucheza soka ya vilabu bingwa Ulaya(Telefoot, via Croydon Guardian)
Newcastle inataka kumsaini mshambuliaji wa Venezuela mwenye umri wa miaka 19 Jan Carlos Hurtado - ambaye amepokea sifa kutoka kwa mchezaji wa zamani wa klabu hiyo Faustino Asprilla - kutoka kwa timu ya Argentina Gimnasia. (Newcastle Chronicle)
TETESI ZA SOKA JUMANNE

Paris St-Germain inafikiria kumnunua kipa wa Manchester United davdi De Gea kwa dau la £90m huku kipa huyo wa Uhispania mwenye umri wa miaka 28 akitarajiwa kulipwa £450,000 kwa wiki na mabingwa hao wa Ufaransa. (Star)
Manchester United inajiandaa kumnunua kipa wa Atletico Madrid mwenye umri wa miaka 26 Jan OBlack. (ESPN)
Mchezaji wa zamani wa Man United na Uingereza Rio Ferdinand amekutana na naibu afisa mkuu mtendaji Ed Woodward ili kuzungumzia kuhusu kuwa mkurugenzi wa michezo katika klabu hiyo (Mail)
Winga wa Bournemouth na Uskochi Ryan Fraser, 25, anajiandaa kuondoka katika klabu hiyo mwisho wa msimu huu kwa kuwa anataka kujiunga na klabu ya juu (Mirror)
Real Madrid wako tayari kumuacha kiungo wa kati wa Norway mwenye umri wa miaka 20 Martin Odegaard ajiunge na Ajax kwa mkopo wa miaka miwili. (Mail)

Chanzo cha picha, Getty Images
Chelsea na Manchester United wanachunguza hali ya mshambuliaji wa PSG na Uruguay mwenye umri wa miaka 32 Edinson Cavani, ambaye anataka kujiunga na ligi ya Uingereza.(Calciomercato)
Liverpool inajiandaa kumpatia Alex Oxlade-Chamberlain kandarasi mpya hadi 2023 - siku chache tu baada kiungo huyo wa kati mwenye umri wa miaka 25 kurudi baada ya jeraha la muda mrefu. (Mirror)
Inter Milan inaendelea na mazungumzo ya kutaka kumsaini beki wa Brazil Danilo, 27, kwa dau la £18m kutoka Manchester City. (Mail)

Wolves watajaribu tena kumsaini beki wa Sweden mwenye umri wa miaka 24 Victor Lindelof kutoka Manchester United, baada ya kufeli kumsaini mwisho wa msimu uliopita. (Teamtalk)
Beki wa Ajax na Uingereza Matthijs de Ligt, 19, anatabiri kwamba huenda asigharimu zaidi ya dau alilonunuliwa mchezaji mwenza Frenkie de Jong, aliyenunuliwa na Barcelona kwa dau la £65m, huku uvumi unaozunguka hatma yake ukiendelea.. (Mirror)
Beki wa kulia wa klabu ya Nice na Algeria Youcef Atal, 22, ni miongoni mwa wachezaji wanaolengwa na Chelsea mwisho wa msimu huu iwapo Fifa itaondoa marufuku ya uhamisho wa klabu hiyo. (Telegraph)
Real Madrid imefanya mazungumzo na klabu ya Lyon kuhusu uhamisho wa kiungo wa kati Tanguy Ndombele. (AS)

Beki wa West Ham, 20, na Uingereza Reece Oxford anakaribia kuandikisha mktaba wa kudumu na klabu ya Bundesliga Augsburg kwa thamani ya £8m. (Sky Sports)
Wachezaji wa Arsenal wameshangazwa na mbinu anazotumia kocha wao mpya Unai Emery wakati wa msururu wa matokeo mabaya wa klabu hiyo. (Telegraph)
Mshambuliaji wa Barcelona na Ghana Kevin-Prince Boateng, 32, anasema kuwa angeichezea Man United kwa miaka 10 iwapo angepata motisha (Goal)
Beki wa Brazil Dani Alves, 35, anafikiria hatma yake katika klabu ya Paris St-Germain kufuatia kufungwa na klabu ya Rennes katika fainali ya kombe la Ufaransa. (RMC)

Kipa wa Barcelona na Uholanzi Jasper Cillessen, 30, amethibitisha kwamba ataondoka katika katika klabu hiyo ya Uhispania ili kushiriki mechi nyingi (Marca)
Kipa wa Manchester United Dean Henderson - ambaye yuko kwa mkopo katika klabu ya Sheffield United - anatarajiwa kuanza mazungumzo kuhusu hatma yake ya Old Trafford lakini atataka kusalia katika uwanja wa Bramall Lane msimu ujao. (Express)
TETESI ZA SOKA JUMATATU

Chanzo cha picha, Rex Features
Wachezaji wa Manchester United wanataniana 'hadharani" kuhusu tetesi za uhamisho wa Paul Pogba kwenda Real Madrid.
Pogba, 26, ameonekana akiwatania wenzake kuwa anataka kujiunga na Real Madrid. (AS - in Spanish)
Mchezaji nyota wa Chelsea Eden Hazard amepigwa picha akiwa amevalia jezi mpya ya mazoezi ya klabu hiyo.
Hatua hiyo imewapa matumaini mashabiki wa Blues kwamba Hazard ambaye pia ni kiungo kimataifa wa Ubelgiji atasalia Stamford Bridge msimu ujao. (Express)

Chanzo cha picha, Getty Images
Ubelgiji inamfuatilia Thorgan Hazard, ambaye ni ndugu ya Eden, na inasema kuwa kiungo huyo wa miaka 26 amekubali kujiunga na Borussia Dortmund na kwamba anasubiri klabu yake ya sasa Borussia Monchengladbach kuidhinisha uhamisho wake. (VTM Nieuws - in Dutch)
Kipa Joe Hart, 32, yuko huru kuondoka Burnley kwa uhamisho bila malipo msimu huu wa joto, huku vilabu kadhaa vya Ligue 1 vikionesha azma ya kutaka kumsajili. (Mail)

Chanzo cha picha, Getty Images
Meneja wa Leicester City Brendan Rodgers amesema kuwa klabu hiyo itafanya kila iwezalo kuhakikisha inampampatia mkataba wa kudumu kiungo wa kati wa Monako Youri Tieleman, 21, msimu ujao. (Mirror)
Kiungo wa kati wa Foxe James Maddison ametoa wito kwa klabu yake kumsaini kiungo huyo wa kimataifa wa Ubegiji. (Leicester Mercury)
Kocha wa Chelsea Maurizio Sarri anapigiwa upatu kuchukua nafasi ya Gennaro Gattuso katika klabu ya AC Milan. (Evening Standard)

Chanzo cha picha, Getty Images
Manchester United imeungana na Liverpool katika kinyang'anyiro cha kusaini mshambuliaji wa Lille na Ivory Coast Nicolas Pepe, 23 ambaye thamani yake inakadiriwa kuwa paini milioni 60. (Express)
Kiungo wa kati wa Croatia Ivan Rakitic, 31, amesema kuwa atasalia Barcelona hadi mkataba wake wa sasa utakapokamilika mwaka 2021. (Marca)
Nicolas Otamendi ataondoka Manchester City msimu huu, na tayari West Ham na Wolves wanataka kumsaini mlinzi huyo wamiaka 31. (Star)

Chanzo cha picha, Reuters
Mpango wa Chelsea msimu ujao ni huenda ukaathiriwa na marufuku ya usajili wa wachezaji Fifa dhidi yao. (Evening Standard)
Bournemouth wanapania kumsajili beki wa nyuma na kati wa West Brom Dara O'Shea, 20, amabaye amekuwa akichezea klabu ya daraja la pili Exeter City. (Mail)
Kipa wa Barcelona na Uholanzi Jasper Cillessen, 30, amesema kuwa anataka kuondoka Nou Camp msimu huu baada ya kushindwa kumuondo Marc-Andre ter Stegen. (Ziggo Sport, via Marca)
Tetesi Bora Jumapili
Juventus wanataka kumregesha Pogba,Turin lakini watalazimika kuwauza wachezaji watatu muhimu ili wawaeze kumnunua mchezaji huyo wa Manchester United raia wa Ufaransa kwa kima cha pauni milioni 130.(Guadian)

Chanzo cha picha, Reuters
Mabingwa hao wa Italia pia huenda wakajaribu kuipiku Paris St-Germain katika kinyang'anyiro cha usajili wa kipa wa United,28, David de Gea. (Le10 Sport in French)
PSG imeipatia Juventus ofa ya euro milioni 70 kumunua kiungo wa kati Miralem Pjanic, 29 , lakini miamba hao wa Ligi ya serie A wanataka euro milioni 100. (Corriere dello Sport-in Italian)













