Dereva aliyeruhusu nyani kuendesha basi afutwa kazi India

Chanzo cha picha, YouTube
Dereva wa basi nchini India amefukuzwa kazi baada ya kumruhusu nyani aendeshe badi lake,
Dereva huyo anafutwa licha abiria hata moja kati ya abiria 30 au zaidi waliokuwa kwenye basi hiyo kutolalamika.
Hata hivyo wakati video ya nyani huyo aliyekuwa ametulia huku akiwa usukani kusambaa mitandaoni, waajiri wa dereva huyo walichukua hatua.
Maisha ya abiria hayawezi kuwekwa hatarini kwa kuruhusu nyani kushika usukani, msemaji alisema.
Hata hivyo hatua hiyo wa waajiri kumfuta dereva haijawafurahisha watumiaji wa mitandao waliofurahishwa na video hiyo.
"Vizuri sana, kwa nini mmufute. Angepewa onyo na aambiwe asirudie, mmoaj aliandika katika twitter.
Kisa hicho kilitokea siku ya Jumatatu kwa mujibu wa idara ya usafiri wa barabarani ambayo ilikuja kufahammu kuhusu kisa hicho wakati video hiyo ilanza kusambaa.
Kwa mujibu wa walioshuhudia, nyani alipanda gari na abiria mwingine lakini akakataa kuketi nyuma bali mbele ya basi.
Dereva M Prakash, ambaye alionekana kutotilia maanani sana suala hilo, alimruhusu nyania kuketi kwenye usukani huku wakiendelea na safari.
Kulingana ripoti nyania alifika kituo chake akashuka na kumuacha dereva akiendelea na safari yake.












