Watanzania wasikitishwa na kifo cha mtoto wa Muna Love, Patrick Dickson Tanzania

Chanzo cha picha, @patdasmartboy
Mtoto wa msanii wa Filamu za Bongo na Mjasiriamali, Rose Alphonce maarufu kama 'Muna Love' ameaga Dunia.
Mtoto Patrick Dickson ambaye alikua na umaarufu sana katika mitandao ya kijamii amefariki jana Julai 3, 2018 nchini Kenya alipokuwa akipatiwa matibabu.
Patrick alianza kuugua tangu mwaka 2016, ambapo alisumbuliwa zaidi na maradhi ya mguu hali iliyo mpelekea kushindwa kutembea.
Kuanzia hapo Patriki alilazwa na kufanyiwa upasuaji mara kadhaa kwa lengo la kutafuta suluhu ya afya yake.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa Instagram ujumbe, 1
Mwaka 2017 Patrick alirejea tena na kuonekana akiwa na afya nzuri japo alikuwa akichechemea mguu mmoja.
Aliweka wazi kuwa ameokoka kwa kurusha video akihubiri neno la Mungu, pia alionekana na wasanii mbali mbali wa muziki wa injili kama vile Joel Lwaga, Chris Shalom na Jimmy Psalmist.
Siku chache zilizopita taarifa zili zagaa mitandaoni kuwa kuwa Patrick amezidiwa na kulazwa katika hospitali iliyopo Nairobi nchini Kenya.
Haipatikani tena
Tazama zaidi katika FacebookBBC haihusiki na taarifa za kutoka mitandao ya nje.Mwisho wa Facebook ujumbe
Taarifa za kuugua kwake zilisambaa katika kurasa mbali mbali za mitandao ya kijamii na wengi wakimuombea apone haraka.
Lakini jana wafuasi wake waligubikwa na simanzi baada ya taarifa za kifo chake kusambaa.
Wasanii na watu mbali mbali ndani na nje ya Tanzania wamerusha salamu za za kumwombea Patrick apumzike kwa amani.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa Instagram ujumbe, 2
Mpaka sasa kupitia mitandao ya kijamii watanzania mbali mbali waliopo ndani na nje ya nchi wanahamasishana kuchanga fedha ili kumsaidia mama yake aweze rejesha mwili wa Patrick Tanzania kwaajili ya mazishi.
Patrick maarufu kama Patda smart boy, ni mtoto mwenye vipaji mbali mbali kama vile mwigizaji na mwana mitindo.
Miongoni mwa wanaouzungumzia msiba huu wanasema watamkumbuka Patrick kwa ujasiri wake, kuhubiri neno la Mungu pia utanashati wake namna alivyokua akivaa na kupendeza.
Patrick alifahamika na wengi na kupata wafuasi zaidi ya laki na ishirini na nne katika mtandao wa Instagram pekee.














