Bango lililoandikwa kwa Kichina Nairobi lazua mdahalo

Chanzo cha picha, HISANI
Bango la matangazo ambalo lilikuwa limeandikwa kwa Kichina na kuweka katika barabara kuu ya Mombasa kwenda Nairobi limeharibiwa na watu wasiojulikana.
Bango hilo liliharibiwa baada ya Wakenya mtandaoni kulalamika kuhusu tangazo hilo lililokuwa limeandikwa kila kitu kwa Kichina.
Ni nambari za simu ambazo zilikuwa zimeandikwa kwa herufi za Kilatini ambazo ziliweza kusomeka.

Wakenya mtandaoni walilalamika ni vipi bango hilo 'lisiloeleweka' na wenyeji liliidhinishwa kuwekwa kwenye barabara hiyo bila kutafsiriwa kwa Kiingereza au Kiswahili.
Baadhi waliwaomba maafisa wakuu serikali wawasaidie kutafsiri:
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2
Mtangazaji huyu alisema matangazo yanafaa kuwa kwa Kiingereza na Kiswahili na kupendekeza liondolewe.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 3
Baadhi hata hivyo walitetea bango hilo wakisema huenda aliyeliweka aliwalenga Wachina pekee.
Miongoni mwa waliolalamika ni Shirikisho la Watumizi wa Bidhaa na Huduma Kenya (Cofek).
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 4

Nani aliweka tangazo hilo?
Tangazo hilo liliwekwa na kampuni ya ujenzi ya Yunnan International.

Tangazo hilo lilisema nini?
Tafsiri iliyofanywa na Idhaa ya Kichina ya BBC inaonesha linasema:
Yunnan International
Kituo cha huduma zote za ujenzi
- Uanakandarasi
- Masuala ya wafanyakazi
- Bidhaa za ujenzi
- Utengenezaji wa bidhaa
- Utengenezaji wa chuma
- Huduma za usalama
- Matangazo
- Ukarabati na utunzaji
- Mnara wa maji na uhifadhi wa maji
Nambari ya simu ya moja kwa moja: 0708 848 008
Kampuni ya kuaminika na ya kusifika
Yenye kufanya kazi kwa utaalamu na njia bora zaidi
Huduma ya kiwango na ubora wa juu

Baadhi ya Wakenya mtandaoni waliingiza utani:
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 5












