Wanawake nchini Iran wazuiwa kuhudhuria mechi kati ya Iran na Syria

Fans of Syria pose during the FIFA World Cup 2018 qualifying soccer match between Iran and Syria at the Azadi stadium in Tehran, Iran, 5 September 2017

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Wanawake wa Syria waliruhusiwa kuingia uwanjani

Wanawake nchini Iran walizuiwa kuingia uwanja wa kitaifa ambapo timu ya taifa ya nchi hiyo ilikuwa ikicheza mechi ya kufuzu kombe la dunian dhidi ya Syria licha ya wao kuwa na tiketi.

Wanawake hao walikusanyika nje ya uwanja wa Azadi mjini Tehran kulalamika wakati waliamrishwa kuondoka, huku wanawake raia Syria wakiruhusiwa kuingia uwanjani bila tatizo lolote baada ya kuonyesha paspoti zao.

Wanawake wamepigwa marufuku ya kuhudhuria mechi za kandanda ya wanaume nchini Iran.

Wanawake kadha walikuwa wamenunua tiketi kwa njia ya mtandao wiki moja mapema kabla ya mechi.

Supporters of Syria cheer for their team during the FIFA World Cup 2018 qualification football match between Iran and Syria at the Azadi Stadium in Tehran on 5 September

Chanzo cha picha, AFP/Getty Images

Maelezo ya picha, Karibu mashabiki 200 wa Syria walisafiri kwenda Iran

Lakini shiriko la kandanda nchini Iran lilisema kuwa tiketi hizo ziliuzwa kimakosa na kuahidi kuwarejeshea pesa wanawake ambao walikuwa tayari wamezinunua.

Wale waliokuwa na tiketi hata hivyo waliamua kuelekea uwanjani jana Jumanne wakitaka kujaribu ikiwa wangeruhusiwa kuingia.

"Hawakuturuhusu kuingia, walitupiga picha na kuchukua video na kutishia kutukamata. Kisha wakakusanya tiketi zetu na kuzichukua. shabiki mmoja alianiska katika mtandao wa twitter.

Supporters of Iran cheer for their team during the FIFA World Cup 2018 qualification football between Syria and Iran at the Azadi Stadium in Tehran on 5 September 2017

Chanzo cha picha, AFP/Getty Images

Maelezo ya picha, Wanawake wamepigwa marufuku ya kuhudhuria mechi za kandanda ya wanaume nchini Iran.