Kwa picha: Kimbunga Debbie nchini Australia
Kimbunga kwa jina Debbie kimekumba eneo la kaskazini mashariki mwa jimbo la Queensland na kusababisha mvua kubwa eneo hilo.
Maelfu ya watu wamehamishwa huku wengi wakitafuta hifadhi katika makao ya muda.
Moja ya maeneo yaliyoathiriwa ni la Airlie Beach eneo maarufu kwa watalii ambalo limegeuka na kuwa mahame kufuatia kuwasili kwa kimbunga hicho.

Chanzo cha picha, EPA
Baadhi ya majengo yaliharibiwa.

Chanzo cha picha, EPA
Miti mikubwa iling'olewa na upepo mkali wa kimbunga hicho.

Chanzo cha picha, EPA
Wakaazi wa maeneo karibu na pwani wakiwemo wale walio mji wa Ayr wamehamishwa.

Chanzo cha picha, AFP/Getty Images
Watoto walibaki nyuma huku shule zikifungwa wakati wa dharura hiyo.

Chanzo cha picha, AFP/Getty Images
Idara ya utabiri wa hali ya hewa nchini Australia, Jumanne jioni ilionyesha kimbuna eneo la Queensland.

Chanzo cha picha, Australia BOM
Mtandao unaofuatia hali ya hewa wa WindyTV nao ulionyesha kimbunga hicho.

Chanzo cha picha, WindyTV
Siku ya Jamatatu mawingu ya kimbunga hicho yalionekana katika anga ya Ayr.

Chanzo cha picha, AFP/Getty Images
Picha za Satellite : Australian Bureau of Meteorology.












