Kwa picha: Maisha ya kiongozi wa zamani wa Usovieti Mikhail Gorbachev

Mikhael

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mikhail Gorbachev aliishi maisha yake marefu zaidi ya utotoni akifanya kazi katika mashamba ya jumla na familia yake kusini mwa Urusi

Mikhail Gorbachev, mwanaume ambaye aliendelea na hatimaye kuwa mmoja wa wanasiasa wenye ushawishi mkubwa zaidi katika karne ya 20, alizaliwa katika hali ya umasikini tarehe 2 Machi 1931 katika jimbo la Stavropol rkusini mwa Urusi

wazazi wake wote walifanya kazi katika mashamba ya pamoja na utoto wake Gorbachev alifanya kazi hiyo pamoja na wavunaji akiwa na umri wa kubalehe.

G

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mikhail Gorbachev (mwisho kulia) akiwa na wanafunzi wenzake darasani mwaka 1947. Alikwenda kusoma sheria katika Chuo kikuu cha taifa cha Moscow

Wakati anasoma katika Chuo kikuu cha Kitaifa cha Moscow, alikutana na mke wake, Raisa, na kuwa mjumbe wa chma cha kikomunisti . Baada ya kuhitimu, alirejea Stavropol na kuanza kupanda kwa haraka vyeo katika Chama cha kikomunisti.

G

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Gorbachev alimuoa mke wake Raisa katika mwaka 1953. Baada ya kifo cha mke wake, aliandika kwamba maisha yake yamepotea "ni maana ya kimsingi"

Katika mwaka 1985, kiongozi wa Usovieti Konstantin Chernenko alifariki mwaka mmoja tu baada ya kuingia mamlakani , na Mikhail Gorbachev ambaye alikuwa kijana zaidi akawa kiongozi wa USSR.

Wakati ule, uchumi wa Muungano wa Usovieti ulikuwa mashakani kuweza kuhimili kasi ya Marekani, na Gorbachevtafuta suluhu mbili kuu. Alisema nchi inahitaji "perestroika" - au mpango mpya - na zana yake ya kukabiliana nao ni "glasnost" - uwazi .

Silaha yake nyingine ya kukabiliana na mkwamo wa mfumo wa uchumi ni demokrasia. kwa mara ya kwanza kulikuwa na uchaguzi huru katika bunge la watu.

G

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Gorbachev katika congresi ya 27 ya chama cha Kikomunisti cha Usovieti katika mwaka 1986, kongamano la kwanza la viongozi wa Kikomunisti taliloliongoza baada ya kuingia mamlakani mwaka uliotangulia.

Gorbachev pia alitaka kumaliza Vita Baridi, ambavyo vilikuwa vinaigharimu nchi yake mamilioni ya dola kila mwaka ili kuendeleza kasi ya ukuaji wa haraka wa matumizi ya jeshi la Marekani.

Katika mwaka 1985, alikutana na rais wa Marekani Ronald Reagan kwa mazungumzo kuhusu kuweka ukomo wa uzalishaji wa makombora ya nyuklia na kuanzisha upya mahusiano ya kidiplomasia baina ya mataifa hayo yenye nguvu zaidi .

Pia alimaliza vita vya muda mrefu vya Usovieti katika Afghanistan, ambavyo vilikuwa vimegharimu maisha ya maelfu ya watu tangu Moscow ilipoingilia kuunga mkono serikali ya kisopale katika mwaka 1979.

G

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Ronald Reagan na Mikhail Gorbachev wakisaini mkataba kuhusu vikosi vya nyuklia vinavyotumia makombora ya masafa marefu - Intermediate-Range katika mwaka 1987.

Makubaliano hayo yaliwezesha kusitishwa kwa utumiwaji wa maelfu ya makombora.

Huku mageuzi yake yalikuwa maarufu miongoni mwa viongozi wa Magharibi, USSR ilianza kugawanyika taratibu chini ya uongozi wake , na katika usiku wa kuamkia Krismasi mwaka 1991, Gorbachev alikubali kuvunjwa kwa Muungano wa Usovieti.

Gorbachev aliendelea kuwa na jukumu la kuwa mzungumzaji wa masuala ya Urusi na ya kimataifa, lakini alisifiwa sana nje ya nchi kuliko nyumbani.

G

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mikhail Gorbachev akiwa pamoja na Papa John Paul II mjini Vatican. Kiongozi wa Katoliki alikuwa mpinzani wa wazi wa Ukomunisti na ushawishi wa Usovieti

Alipatwa na pigo la kibinafsi mwaka 1999, wakati Rais alipofariki kwa saratani ya damu . Uwepo wake wa wakato wowote kando na mumewe ulionyesha sura ya ubinadamu katika mageuzi ya kisiasa.

Baada ya Vladimir Putin kuingia katika mamlaka ya dunia, Gorbachev alikuwa mkosoaji wa wazi, akimshutumu kuendesha utawala wa ukandamizaji.

G

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Gorbachev aligeuka na kuwa mkosoaji mkali wa Rais Vladimir Putin katika miaka yake ya mwisho, ambaye alimshutumu kuendesha utawala wa ukandamizaji

Gorbachev alifariki mjini Moscow huku Urusi ikiivamia Ukraine, operesheni ambayo baadhi wanasema ni jaribio la Putin la kujenga upya ushawishi wa Usovieti .

G

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mikhail Gorbachev alifariki 30 Augusti 2022, akiwa na umri wa miaka aged 91