Wakurdi 30,000 Ujerumani waandamana dhidi ya Erdogan

Maandamano ya Wakurdi, wakibeba bendera yenye picha ya kinara mkuu wa PKK, aliyefungwa jela Abdullah Ocalan

Chanzo cha picha, BORIS ROESSLER/DPA VIA AP

Maelezo ya picha, Maandamano ya Wakurdi, wakibeba bendera yenye picha ya kinara mkuu wa PKK, aliyefungwa jela Abdullah Ocalan

Zaidi ya wakurdi wa Uturuki wapatao elfu thelathini wamefanya maandamano katika mji wa Frankfurt nchini Ujerumani, dhidi ya Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan.

Waandamanaji hao walikusanyika kutoka miji yote nchini Ujerumani, kabla ya kufanyika kwa - Nowruz, sherehe za maadhimisho ya mwaka mpya kwa Wakurdi.

Wametoa wito wa kuwepo kwa demokrasia nchini Uturuki, na wamesema HAPANA kwa shughuli za kura ya maoni ya kuongeza nguvu ya Rais, ambazo zimeandaliwa kufanyika nchini Uturuki mwezi ujao, .

Baadhi yao walipeperusha bendera huku wakibeba picha ya kiongozi wa kivita wa wakurdi aliyefungwa gerezani, Abdullah Ocalan.

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameikashifu vikali Ujerumani

Chanzo cha picha, AFP/GETTY IMAGES

Maelezo ya picha, Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameikashifu vikali Ujerumani

Msemaji wa Bwana Erdogan, amelaani mkutano huo na kuilaumu Ujerumani kwa upendeleo, kwa kukubalia mkutano huo kufanyika.

Baadhi ya miji kadhaa nchini Ujerumani, yalikataa kuwaruhusu mawaziri wa Uturuki kuwahutubia raia wa Uturuki walioko nchini humo.