Super League: Ivory Coast ndio itakayoathiriwa zaidi iwapo marufuku ya Fifa itathibitishwa

Ivory Coast ndio timu ya Afrika itakayoathiriwa ikiwa wachezaji wa Ligi mpya ya Ulaya inayopendekezwa (ESL) watapigwa marufuku kucheza soka ya kimataifa.
The Elephants wana wachezaji wao watano wa kikosi cha kwanza katika vilabu ambavyo vimesema vinataka kushiriki katika ligi mpya ya ESL - Serge Aurier akiwa Tottenham; Nicolas Pepe wa Arsenal; Franck Kessie wa AC Milan; na wachezaji wa Manchester United Eric Bailly na Amad Diallo.
Mohamed Salah wa Misri, Riyad Mahrez wa Algeria na Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon pia watakosa mechi hizo ikiwa shirikisho la soka duniani Fifa litatekeleza onyo yake ya hapo awali kwamba wachezaji wote watakaojitokeza kwenye ESL watapigwa marufuku kwenye mashindano ya kimataifa kama Kombe la Dunia.
Kama ilivyo sasa jumla ya timu 13 za Afrika zitawapoteza wachezaji wake
Kufikia sasa vilabu 12 bora barani Ulaya vimekubali kujiunga na ESL, zikijumuisha sita kutoka Ligi Kuu ya England - Arsenal, Chelsea, Liverpool, Manchester City, Manchester United na Tottenham.
vilabu hivyo vya Ligi Kuu vitajiunga na AC Milan, Atletico Madrid, Barcelona, Inter Milan, Juventus na Real Madrid.

Senegal inaweza kupoteza wachezaji watatu -mshambuliaji wa Liverpool Sadio Mane, kipa wa kwanza Edouard Mendy wa Chelsea, na Moussa Wague - wa Barcelona, ingawa kwa sasa anaichezea kwa mkopo PAOK Salonika ya Uigiriki.
Liverpool:
- Mohamed Salah - Misri
- Sadio Mane - Senegal
- Naby Keita - Guinea
- Joel Matip - Cameroon
- (Taiwo Awoniyi - Nigeria - kwa mkopo Union Berlin)
Chelsea:
- Edouard Mendy - Senegal
- Hakim Ziyech - Morocco
- (Baba Rahman - Ghana - kwa mkopo PAOK Salonika)
- (Victor Moses - Nigeria - kwa mkopo Spartak Moscow)
Manchester City:
- Riyad Mahrez - Algeria
Manchester United:
- Eric Bailly - Ivory Coast
- Amad Diallo - Ivory Coast
Tottenham Hotspur:
- Serge Aurier - Ivory Coast
Arsenal:
- Pierre-Emerick Aubameyang - Gabon
- Thomas Partey - Ghana
- Nicolas Pepe - Ivory Coast
- Mohamed El Neny - Egypt
AC Milan:
- Ismael Bennacer - Algeria
- Franck Kessie - Ivory Coast
Atletico Madrid:
- Geoffrey Kondogbia - Central African Republic
Barcelona:
- (Moussa Wague - Senegal - kwa mkopo PAOK Salonika)
Inter Milan:
- Achraf Hakimi - Morocco
Juventus:
- Hamza Rafia - Tunisia (Katika kikosi cha chipukizi cha Juve)
Real Madrid:
- Hakuna











