Mchezaji bora zaidi Afrika kutangazwa

Aubameyang

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Aubameyang alishinda tuzo ya mwaka 2015

Mchezaji bora zaidi Afrika mwaka 2016 wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) atatangazwa leo jioni.

Wanaoshindania tuzo hiyo ni kiungo wa kati wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, winga wa Algeria Riyad Mahrez na winga wa Senegal Sadio Mané.

Mohamed Salah wa Misri na Islam Slimani wa Algeria walikuwa kwenye orodha ya wachezaji watano bora lakini wakashindwa kufika kwenye orodha ya wachezaji watatu bora.

Kwa tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika, kwa wachezaji wa ligi za mataifa ya Afrika, kipa wa Uganda Goal Keeper anashindana na mshambuliaji wa ZImbabwe Khama Billiat na iungo wa kati wa Zambia Rainford Kalaba .

Mshindi atatangazwa mjini Abuja, Nigeria saa 22.30 saa za Afrika Mashariki.

Aubameyang, Mahrez, Mane

Chanzo cha picha, CAF/Twitter

Wanaoshindania Tuzo ya Mchezaji Bora Afrika

  • Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon & Borussia Dortmund)
  • Riyad Mahrez (Algeria & Leicester City)
  • Sadio Mané (Senegal & Liverpool)
Ongango na Kalaba

Chanzo cha picha, CAF

Wanaoshindania Tuzo ya Mchezaji Bora Afrika (Ligi za Afrika)

  • Denis Onyango (Uganda & Mamelodi Sundowns)
  • Khama Billiat (Zimbabwe & Mamelodi Sundowns)
  • Rainford Kalaba (Zambia & TP Mazembe)

Washindi wa awali wa Tuzo ya Mchezaji Bora Afrika

2015: Pierre-Emerick Aubameyang

2014: Yaya Toure

2013: Yaya Toure

2012: Yaya Toure

2011: Yaya Toure

2010: Samuel Eto'o

2009: Didier Drogba

2008: Emmanuel Adebayor

2007: Frederic Kanoute

2006: Didier Drogba

2005: Samuel Eto'o

2004: Samuel Eto'o

2003: Samuel Eto'o

2002: El Hadji Diouf

2001: El Hadji Diouf

2000: Patrick Mbomba

1999: Nwankwo Kanu

1998: Mustapha Hadji

1997: Victor Ikpeba

1996: Nwankwo Kanu

1995: George Weah

1994: Emmanuel Amunike

1993: Rashidi Yekini

1992: Abedi Pele