Shinikizo yazidi kwa Rais Biden kujibu mashambulizi ya wanamgambo wa Iran

Haijabainika ni umbali gani Marekani inaweza kufika, lakini hali hiyo ni ukumbusho wa kile kilichotokea baada ya mashambulizi ya Desemba 2019, wakati wanamgambo wa Iraq waliporusha makombora kwenye kambi ya Marekani huko Kirkuk, na kumuua mwanakandarasi wa Marekani.

Moja kwa moja

Asha Juma and Abdalla Seif Dzungu

  1. Shinikizo yazidi kwa Rais Biden kujibu mashambulizi ya wanamgambo wa Iran

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Joe Biden

    Haijabainika ni umbali gani Marekani inaweza kufika, lakini hali hiyo ni ukumbusho wa kile kilichotokea baada ya mashambulizi ya Desemba 2019, wakati wanamgambo wa Iraq waliporusha makombora kwenye kambi ya Marekani huko Kirkuk, na kumuua mwanakandarasi wa Marekani.

    Baada ya shambulio hilo, Marekani ililipiza kisasi kwa kufanya mashambulizi makubwa ya anga kwenye kambi ya wanamgambo kwenye mpaka wa Iraq na Syria, na kuua wanachama 25.

    Mazishi yao yalizua maandamano ya wanamgambo wa Shia wanaoiunga mkono Iran na wafuasi wake, ambao walivamia ubalozi wa Marekani mjini Baghdad.

    Msururu huu wa matukio ulichangia pakubwa katika uamuzi wa Rais wa zamani Donald Trump kumuua mmoja wa makamanda wakuu wa Walinzi wa Mapinduzi ya Iran (IRGC), Jenerali Qasem Soleimani.

    Marekani na Iran zimesema mara kwa mara katika miezi michache iliyopita kwamba hazitaki kusambaa kwa vita zaidi katika eneo hilo.

    Bila shaka kutakuwa na mahesabu mengi na uwezekano wa kubadilishana ujumbe nyuma ya pazia kati ya Tehran na Washington, lakini kilichotokea katika Mnara wa 22 kinafanya iwe vigumu zaidi kwa Marekani kusitisha majibu yake kwa "washukiwa wa kawaida tu".

    Swali linabaki, je, Marekani itafanya kitu sawa wakati huu shinikizo linapozidi kwa utawala wa Biden kuijibu moja kwa moja Iran kama muungaji mkono wa makundi haya?

  2. Uanachama wa ANC wa rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma wasimamishwa

    .

    Chanzo cha picha, AFP

    Maelezo ya picha, Jacob Zuma

    Chama tawala nchini Afrika Kusini cha African National Congress (ANC) kimeamua kumsimamisha kama mwanachama wake Rais wa Jacob Zuma, tovuti za habari za ndani zinanukuu vyanzo vya ANC ambavyo havikutajwa majina.

    Uamuzi huo ulichukuliwa na bodi kuu ya uongozi ya ANC, kamati kuu ya kitaifa, kufuatia tangazo la Bw Zuma mwezi uliopita kwamba atafanya kampeni kwa chama kipya, Umkhonto we Sizwe (MK), katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa baadaye mwaka huu, News24 na TimesLive zimeripoti.

    Bw Zuma alisema atasalia kuwa mwanachama wa ANC lakini "utakuwa usaliti" kufanya kampeni kwa ANC ya Rais wa sasa Cyril Ramaphosa.

    Bw Zuma amehutubia mikutano kadhaa ya Umkhonto we Sizwe, ambayo ina maana ya mkuki wa taifa, na ni jina sawa na tawi la zamani la ANC.

    Pia hutumia kifupisho sawa, MK.Hapo awali ANC iliapa kuchukua hatua za kisheria kuzuia chama kipya kutumia jina hilo.

    Bw Zuma alijiuzulu kama kiongozi wa ANC baada ya kumalizika kwa mihula yake miwili mwaka wa 2018.

    Mgombea aliyempendelea alipoteza kinyang'anyiro cha uongozi wa chama kwa kushindwa na Bw Ramaphosa.

    Bw Zuma kisha alilazimika kujiuzulu kama rais wa Afrika Kusini takriban miezi miwili baadaye kufuatia shinikizo kubwa kutoka ndani ya ANC. Bw Zuma alifungwa 2021 kwa kudharau mahakama baada ya kukataa kutoa ushahidi mbele ya jopo lililokuwa likichunguza ufisadi wakati wa uongozi wake.

    Kwa sasa anakabiliwa na mashtaka tofauti ya ufisadi kuhusu mkataba wa silaha ambao serikali ilijadiliana.

    Alikuwa kiongozi mkuu wa ANC wakati huo, lakini si rais.Mara kwa mara amekanusha makosa yoyote, akisema alikuwa mwathirika wa uwindaji wa wachawi wa kisiasa.

  3. Nyimbo mpya ya msanii Nay wa Mitego kutoka Tanzania 'Wapi Uko' yazua mjadala Kenya

    .

    Chanzo cha picha, Nay wa Mitego

    Maelezo ya picha, Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Nay wa Mitego

    Wakenya wameachwa vinywa wazi kufuatia wimbo wa rapa kutoka Tanzania, Emmanuel Elibariki, maarufu Nay wa Mitego, uliozungumzia kuhusu nchi isiyojulikana.

    Wimbo huo wa “Wapi huko” unaangazia taifa` fulani linaloandamwa na uongozi mbovu, rushwa, njaa na ukosefu wa fursa za ajira kwa vijana wake.

    Katika wimbo huo, Nay anasimulia jinsi nchi inavyoonekana kuwa nzuri na yenye mafanikio mbele ya ulimwengu, lakini watu wake wanateseka chini ya viongozi wazembe, vijana wake wanasota kwenye umasikini na wasichana wake sasa wameingia kwenye pesa kuliko mapenzi.

    Zaidi ya hayo, rapa huyo anawachana vijana kwa kuwatafuta akina kina mama wenye fedha, kuzungumza Kiingereza kizuri na kujigamba jinsi nchi yao ilivyo bora kuliko majirani zao, lakini nyumbani kwao hawana hata umeme.

    Wimbo huo kufikia sasa umeibua mjadala kwenye Twitter, huku Wakenya wakitofautiana iwapo mwimbaji huyo anawalenga, au anaangazia tu matatizo yanayoikumba nchi yake.

    Conrad Kulo mmoja alisema: "Tanzania inatupika kihalisi. Jirani hana unga, hana umeme, ni kingereza tu slur sasa imepikwa studio, na niwaambie Maina, William Ruto lazima aende.

    "Hata hivyo, mtumiaji wa X Mwabili Mwagodi alitofautiana naye akisema Nay analenga tu uongozi wa Tanzania.

    "Ni mambo ambayo Wakenya hawajaelewa kabisa kwamba Ney wa Mitego anakejeli uongozi wa Tanzania kwa kuibeza Kenya bado Tanzania ndiyo imeingia shimoni.

    Mwanamume anayejiita jina la Elon’s Musk anasema kwamba siamini msanii wa Tanzania ndiye anayeweza kuja kuelezea shida zilizopo Kenya kwasababu wasanii wa Kenya wana mambo mengi kichwani

    Hivi ndio jinsi Wakenya walivyosema kuhusu wimbo huo:

    Ruka X ujumbe, 1
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe, 1

    Ruka X ujumbe, 2
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe, 2

    Ruka X ujumbe, 3
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe, 3

  4. RSF ya Sudan inasema ilidungua ndege zisizo na rubani zilizotengenezwa na Iran

    Kundi la wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF) nchini Sudan linasema kuwa limeidungua ndege isiyo na rubani iliyotengenezwa na Iran inayodaiwa kuwa ya jeshi la Sudan wakati mapigano yakiendelea kati ya vikosi hivyo viwili katika mji mkuu Khartoum na maeneo mengine.

    Kundi hilo lilisema kwenye mtandao wa X (zamani wa Twitter) siku ya Jumatatu kwamba "limepata ushindi mkubwa asubuhi ya leo, kwa kufanikiwa kukamata na kuangusha ndege isiyo na rubani inayoendeshwa na Jeshi la Sudan (SAF) na wafuasi wake wenye msimamo mkali kutoka kwa utawala wa zamani".

    "Ndege hiyo, iliyotambuliwa kama ya Mohajer-6 ya Iran, inawakilisha ndege ya tatu kama hiyo isiyo na rubani hivi karibuni iliyopunguzwa shukrani kwa juhudi kubwa za wanajeshi wetu jasiri.

    Licha ya mafanikio haya, tunaendelea kukabiliwa na changamoto," iliongeza.Jeshi bado halijazungumza lolote kuhusu tukio hilo.

    Vyombo vya habari vya ndani vimeripoti kuongezeka kwa mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za jeshi dhidi ya vituo vya RSF mjini Khartoum na miji ya karibu ya Omdurman na Bahri.

    Jeshi limeongeza mashambulizi ya anga dhidi ya RSF katika wiki za hivi karibuni huku mapigano yakiendelea nchini humo kwa mwezi wa tisa.

  5. Maaskofu wa Afrika ni 'kesi maalum' kuhusu baraka za wapenzi wa jinsia moja - Papa

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Papa Francis

    Papa Francis amesema maaskofu wa Kiafrika ni "kesi maalum" kuhusiana na upinzani wao kwa uamuzi wake wa kuruhusu baraka kwa wapenzi wa jinsia moja.

    Lakini alibaki na uhakika kwamba hatua kwa hatua kila mtu atahakikishiwa na tamko la Kanisa.

    Katika mahojiano na gazeti la Italia, Papa alisema viongozi wa makanisa ya Afrika na wafuasi wao wanaona mapenzi ya jinsia moja kutoka kwa mtazamo wa kitamaduni kama "kitu kibaya".

    Alisema hati mpya ya mwezi uliopita, Fiducia Supplicans, ilikusudiwa "kuunganisha na sio kugawanya".

    Papa Francis alisema hajali kuhusu wahafidhina kujitenga na Kanisa Katoliki kutokana na mageuzi yake, akisema kuwa mazungumzo ya mgawanyiko yanaongozwa na kile alichokiita "makundi madogo ya itikadi".

  6. Kwanini Marekani ina kambi nyingi za kijeshi Mashariki ya kati?

    Kambi hiyo ambayo ilipigwa katika shambulio baya la ndege zisizo na rubani eneo la kaskazini-magharibi mwa Jordan ni mojawapo ya zaidi ya makumi ya kambi ambapo wanajeshi wa Marekani wanafanya kazi kote Iraq, Jordan na Syria.

    Katika miezi ya hivi karibuni, kambi hizi - kuanzia ukubwa wa kituo cha kijeshi kama vile Mnara wa 22 ulioshambuliwa Jordan, hadi kituo cha anga cha Al Asad magharibi mwa Iraq - zimeshambuliwa na wanamgambo waliofunzwa, kufadhiliwa na kupewa vifaa na Iran.

    Kuna takriban wanajeshi 3,000 wa Marekani walioko Jordan, mshirika mkuu wa Marekani, na 2,500 nchini Iraq - kwa mwaliko wa serikali ya Iraq kama sehemu ya muungano unaoongozwa na Marekani ili kuzuia kuibuka tena kwa kundi la kijihadi la Islamic State, ambalo bado uwepo huko baada ya kuhamishwa mnamo 2017.

    Pia kuna takriban wafanyakazi 900 wa Marekani nchini Syria, rasmi wapo kwa ajili ya kumuunga mkono mshirika wake anayepinga IS, Vikosi vya Kidemokrasia vya Syria vinavyoongozwa na Wakurdi katika eneo la kaskazini-mashariki mwa Syria.

    Serikali ya Syria inapinga uwepo wa Marekani katika nchi yake, ikiiita kuwa ni uvamizi.

    Marekani pia ina kambi nyingi zaidi katika eneo la Mashariki ya Kati, zikiwemo kambi tatu kuu za anga katika Ghuba na bandari ya Bahrain ambayo inatumika kama makao makuu ya Kikosi cha Wanamaji cha Marekani na Meli ya Tano ya Marekani.

  7. Video: Tazama meli kubwa zaidi ya watalii duniani inapoondoka Bandari ya Miami

    Maelezo ya video, Tazama meli kubwa zaidi ya watalii duniani

    Meli kubwa zaidi duniani ya watalii imefunga safari kutoka Miami, Florida, katika safari yake ya kwanza.Meli hiyo yenye urefu wa mita 365 (futi 1,197) ina ghorofa 20 na inaweza kubeba abiria 7,600.

    Inamilikiwa na Royal Caribbean Group.

    Meli hiyo inaendelea na safari yake ya siku saba ya kupitia visiwa kadhaa Lakini wanamazingira wanaonya kuwa meli hiyo inayotumia gesi itavujisha gesi hatari ya methane angani.

  8. Wanamgambo wa Iran wakiri kuhusika na shambulio dhidi ya Marekani

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Kundi la wapiganaji wanaosaidiwa na Iran ladai kuhusika na Shambulio dhidi ya Marekani

    Kundi la Islamic Resistance nchini Iraq limesema ndilo lililohusika na shambulio hilo kwenye kambi ya Marekani karibu na mto Jordan na Syria.

    Kundi hilo liliibuka mwishoni mwa 2023 na lina wanamgambo kadhaa wenye uhusiano na Iran wanaofanya kazi nchini Iraq.

    Pia limedai litatekeleza mashambulizi mengine dhidi ya vikosi vya Marekani katika wiki za hivi karibuni.

    Katika taarifa yake kundi la Islamic Resistance limesema lililenga vituo vitatu vya Marekani nchini Syria na Jordan - Shaddadi, Rukban na Tanf, pamoja na kituo cha mafuta cha Israel katika bahari ya Mediterania.

    Iran imekanusha kuwa ilihusika na mashambulizi hayo, ikisema "haikuhusika katika maamuzi ya makundi ya upinzani".

    Rais wa Marekani Joe Biden alijibu mashambulizi hayo akisema kuwa Marekani "itawawajibisha wale wote waliohusika kwa wakati na namna tutakavyochagua".

  9. Shida ya Biden ni jinsi ya kulipiza kisasi

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Rais Joe Biden

    Huu ni mfumo wa Iran. Wamefadhili na kutoa mafunzo kwa wanamgambo wanaofanya kazi katika eneo hilo, ikiwa ni pamoja na Iraq na Syria.

    Maadui wa Iran wanawachukulia kama mtandao wa magaidi, lakini Iran inawachukulia kama ulinzi wake ambao unaweza kuwapiga maadui zao.

    Na bado inakataliwa. Wanakanusha kuwa hawakuhusika na shambulio hilo kwenye kambi ya Marekani.

    Marekani haikubali hilo. Kwa hivyo shida ya Rais Biden sasa ni jinsi ya kulipiza kisasi, nani apige na wapige wapi.

    Kushambulia ardhi ya Iran kutachochea hali, kwa hivyo labda hawataki kufanya hivyo, lakini wanaweza kujaribu kufanya kitu katikati kinachofanya kazi.

    Swali kubwa kuhusu hilo ingawa: Je, Marekani inaweza kuzuia mashambulizi kwa kurudisha nyuma kwa nguvu? Au itaongeza tu ongezeko hili thabiti ambalo tunaona katika eneo lote?

  10. Habari za hivi punde, Tunachojua kufikia sasa kuhusu mzozo mpya wa Iran na Marekani

    Shambulio la ndege zisizo na rubani katika kituo cha Marekani karibu na mpaka wa Syria na Jordan liliua wanajeshi watatu wa Marekani na kujeruhi makumi ya wengine.

    • Marekani inawashutumu wanamgambo wanaoiunga mkono Iran kwa kuhusika na shambulio hilo, ambalo linadhaniwa lilifanyika katika makao ya kambi ya Marekani.
    • Joe Biden ameapa kwamba Marekani "itajibu" kwa wakati. Baadhi ya Warepublican wanatoa wito kwa mashambulizi makubwa ya kulipiza kisasi kama kizuizi
    • Iran imekanusha kuwa ilihusika na shambulio hilo, ikizitaja tuhuma kuwa "hazina msingi" na kusema "haikuhusika katika maamuzi ya vikundi vya upinzani".
    • Mbali na waliouawa, maafisa wa Marekani walisema kuwa wengine 34 wamejeruhiwa. Wanane walihamishwa kwa matibabu nje ya msingi, na wengine wako katika hali mbaya lakini thabiti
    • Jordan ililaani shambulio hilo na kusema inaendelea kushirikiana na Marekani kulinda mpaka na kupambana na ugaidi.
    • Uingereza iliitaka Iran kuzuia mashambulizi hayo, kama Waziri Mkuu Rishi Sunak alivyosema: "Tunalaani kabisa kile kilichotokea katika siku chache zilizopita."
  11. Waasi wa Houthi wadai kurusha kombora jengine kwenye meli ya kivita ya Marekani

    .

    Chanzo cha picha, bbc

    Maelezo ya picha, kombora

    Kundi la waasi la Houthi nchini Yemen linadai kuwa lilirusha kombora katika meli ya kivita ya Marekani katika Ghuba ya Aden Jumapili jioni.

    Msemaji wa kijeshi Yahya Sarea alisema katika taarifa yake kwamba vikosi vya wanamaji vya kundi linaloungwa mkono na Iran vililenga meli ya USS Lewis B Puller, meli ya jukwaa la safari ya simu iliyotumwa katika eneo hilo kusaidia meli ya tano ya Marekani.

    Operesheni hiyo ilikuwa sehemu ya "hatua za kijeshi katika ulinzi wa Yemen, uthibitisho wa uamuzi wa kuunga mkono watu wanaodhulumiwa wa Palestina", aliongeza.

    Hakukuwa na maoni ya mara moja kutoka kwa jeshi la Marekani.

    Waasi wa Houthi wamefanya mashambulizi kadhaa ya ndege zisizo na rubani na makombora dhidi ya meli za wafanyabiashara na majini katika Bahari Nyekundu na Ghuba ya Aden tangu katikati ya Novemba kujibu vita vya Israel na Hamas katika Ukanda wa Gaza.

    Marekani ilisema mwezi Januari itawateua tena Wahouthi na kuwataja kuwa "magaidi wa kimataifa".

    Siku ya Ijumaa, meli ya kivita ya USS Carney ilirusha kombora la kutungua meli lililorushwa na Houthis katika Ghuba ya Aden, kulingana na jeshi la Marekani Na siku ya Jumamosi, meli ya kivita ya Uingereza HMS Diamond iliangusha ndege isiyo na rubani iliyokuwa ikilenga katika Bahari ya shamu, wizara ya ulinzi ya Uingereza ilisema.

  12. Sudan Kusini: Watu wenye silaha wavamia wanakijiji katika eneo lenye utajiri wa mafuta linalozozaniwa

    .

    Watu wenye silaha wamewashambulia wanakijiji katika eneo lenye utajiri wa mafuta la Abyei linalozozaniwa na Sudan na Sudan Kusini, na kusababisha vifo vya takriban watu 52, akiwemo askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa, huku 64 wakijeruhiwa, afisa wa eneo hilo alisema Jumapili.

    Sababu ya shambulio hilo Jumamosi jioni haikujulikana mara moja lakini inashukiwa kuzunguka mzozo wa ardhi, Bulis Koch, waziri wa habari wa Abyei, aliambia The Associated Press katika mahojiano ya simu kutoka Abyei.

    Ghasia mbaya za kikabila zimekuwa za kawaida katika eneo hilo, ambapo wana kabila la Twic Dinka kutoka Jimbo jirani la Warrap wako katika mzozo wa ardhi na Ngok Dinka kutoka Abyei kuhusu eneo la Aneet, lililo mpakani.

    Washambuliaji katika ghasia za Jumamosi walikuwa vijana wenye silaha kutoka kabila la Nuer ambao walihamia jimbo la Warrap mwaka jana kwa sababu ya mafuriko katika maeneo yao, Koch alisema.

    Mzozo wa kijeshi wa Sudan unakaribia Sudan Kusini na Abyei, mjumbe wa Umoja wa Mataifa ameonya.

    Katika taarifa yake, Kikosi cha Usalama cha Muda cha Umoja wa Mataifa cha Abyei (UNISFA) kimelaani ghasia hizo.

    Sudan na Sudan Kusini zimetofautiana kuhusu udhibiti wa eneo la Abyei tangu makubaliano ya amani ya mwaka 2005 yalipomaliza miongo kadhaa ya vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya kaskazini na kusini mwa Sudan.

    Sudan na Sudan Kusini zote zinadai umiliki wa Abyei, ambayo hadhi yake haikutatuliwa baada ya Sudan Kusini kuwa huru kutoka kwa Sudan mwaka 2011.

    Soma zadi:

  13. Sudan Kusini yapiga marufuku pombe ya kienyeji maarufu lakini iliyo hatari sana

    .

    Chanzo cha picha, Nichola Mandil/BBC

    Maelezo ya picha, Bia hiyo maarufu kama "Makuei Gin" inasemekana kuwa na uraibu, haswa kwa vijana.

    Mamlaka katika jimbo la Ikweta ya Kati nchini Sudan Kusini imepiga marufuku uuzaji wa bia maarufu baada ya watu kadhaa kufariki baada ya kunywa pombe hiyo ya kienyeji.

    Royal Gin, maarufu kama "Makuei Gin" inasemekana kuwa na uraibu, haswa kwa vijana.

    Inadhaniwa kuwa unywaji wake uliongezeka wakati wa sherehe za Krismasi na Mwaka Mpya, na kusababisha vifo vya idadi isiyojulikana ya watu.

    "Nimepiga marufuku bia hii nyekundu, Royal Gin inayoitwa 'Makuei'. Hakuna mtu anayepaswa kuiuza wala kuinywa kwa sababu inaua vijana wengi," Gavana wa jimbo la Central Equatoria Emmanuel Adil Anthony alisema Jumapili.

    “Vijana wengi wanapolewa huwapiga mama zao kwa mapanga,” aliongeza.

    Kanisa la Kianglikana katika mji mkuu, Juba, limemtaka gavana huyo kuhakikisha marufuku hiyo inatekelezwa.

    Bia hiyo ilipewa jina la utani la Waziri wa Habari Michael Makuei mnamo 2019, ambaye anasemekana kuwa waziri mzungumzaji zaidi nchini Sudan Kusini.

    Mwaka jana, waziri alitoa wito wa kupigwa marufuku kwa bia hiyo na kutaka kiwanda kinachoizalisha kifungwe.

    Pia unaweza kusoma:

  14. Iran yakanusha kuhusika na shambulizi la ndege zisizo na rubani na kuua wanajeshi watatu wa Marekani

    .

    Chanzo cha picha, PLANET LABS/AP

    Iran imekanusha kuhusika na shambulio la ndege isiyo na rubani kwenye kituo cha kijeshi cha Marekani karibu na mpaka wa Jordan na Syria na kusababisha vifo vya wanajeshi watatu wa Marekani.

    Marekani ililaumu shambulio hilo dhidi ya "makundi ya wapiganaji wenye itikadi kali wanaoungwa mkono na Iran" ambayo pia yamesababisha makumi ya watu kujeruhiwa.

    Rais wa Marekani Biden aliapa kulipiza kisasi na kusema: "Tutajibu."

    Ni mara ya kwanza kwa shambulio kuua wanajeshi wa Marekani katika eneo hilo tangu shambulizi la Hamas la tarehe 7 Oktoba dhidi ya Israel.

    Kumekuwa na mashambulizi mengine kwenye kambi za Marekani katika eneo hilo, lakini kabla ya Jumapili hakukuwa na vifo vilivyoripotiwa kutokea, kulingana na jeshi la Marekani.

    Haijabainika ni nani aliye nyuma ya shambulio hili la hivi punde.

    Bw Biden alisema Marekani "itawawajibisha wale wote waliohusika kwa wakati na kwa njia tunayochagua".

    Iran ilikanusha shutuma za Marekani na Uingereza kwamba inaunga mkono makundi ya wanamgambo wanaolaumiwa kwa shambulizi hilo.

    "Madai haya yanatolewa kwa malengo mahususi ya kisiasa ili kubadili hali halisi ya eneo," msemaji wa wizara ya mambo ya nje Nasser Kanaani alisema, kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la IRNA la Tehran.

    Ikulu ya White House ilisema Bw Biden aliarifiwa Jumapili asubuhi juu ya shambulio hilo na Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lloyd Austin na maafisa wengine.

    Soma zaidi:

  15. Kilichodhaniwa kuwa chuma chakavu chaua watoto wa shule kaskazini-mashariki mwa Nigeria

    Takriban watu sita, baadhi yao wakiwa watoto wa shule, wameuawa kaskazini-mashariki mwa Nigeria kwa kilipuzi ambacho walikidhania kuwa ni chuma chakavu.

    Polisi na maafisa wa eneo hilo katika jimbo la Borno walisema mlipuko huo ulitokea katika jengo la shule ya Kiislamu siku ya Jumamosi.

    Ripoti zinasema wanafunzi mara nyingi hukusanya na kuuza chuma kwa jamii za wenyeji.

    Licha ya kupigwa marufuku kwa tabia hiyo, utafutaji wa vyuma chakavu bado ni jambo la kawaida katika eneo hilo linalokumbwa na ghasia za Kiislamu.

  16. Tukio la Ng'ombe kumuua mfanyikazi wa seneta lazua gumzo Kenya

    .

    Chanzo cha picha, DUNCAN MOORE

    Fahali anayemilikiwa na seneta wa Kenya amemuua mtu anayemtunza katika kaunti ya magharibi ya Kakamega, na kuzua taharuki na huzuni katika eneo hilo.

    Ng'ombe huyo wa thamani, anayeitwa Inasio, aligeuka na kuwa mkali na kumuua Kizito Moi, ambaye amekuwa akiwafunza fahali kwa zaidi ya miaka 20, Seneta wa kaunti ya Kakamega Boni Khalwale, mmiliki wa fahali huyo alisema.

    Mwili wake uliokuwa na majeraha makubwa kichwani, shingoni, tumboni na mgongoni uligunduliwa Jumapili asubuhi.

    Seneta huyo alisema alimuua fahali huyo kwa mkuki kulingana na mila za jamii ya Waluhya. Kisha nyama hugawanywa kati ya wanakijiji.

    Bw Khalwale alisema ni nadra kwa wanyama kugeuka na kuwadhuru wanaowatunza, na kwamba kisa cha mwisho kama hicho kilitokea eneo hilo takriban miaka 30 iliyopita.

    Fahali huyo mwenye umri wa miaka mitano, aliyekuwa na uzani wa kilo 120, alikuwa ametawazwa hivi majuzi kuwa bingwa.

    Seneta huyo amekuwa akiandaa mashindano ya kupigana ya mafahali, maarufu sana magharibi mwa Kenya, ambapo maelfu ya wenyeji mara nyingi hujitokeza kushuhudia tukio hilo.

    Wamiliki wa mafahali walioshinda kama Bw Khalwale wanachukuliwa kuwa mashujaa.

    Soma zaidi:

  17. Malkia wa urembo asakwa nchini Nigeria kwa tuhuma za ulanguzi wa dawa za kulevya

    .

    Chanzo cha picha, National Drug Law Enforcement Agency

    Mamlaka nchini Nigeria imetangaza kuwa malkia wa zamani wa urembo anasakwa kwa madai ya kuhusika na ulanguzi wa dawa za kulevya.

    Aderinoye Queen Christmas, anayejulikana pia kama Malkia Oluwadamilola Aderinoye, anasemekana kuwatoroka maofisa wa Shirika la Kitaifa la Kupambana na Dawa za Kulevya (NDLEA) walipovamia makazi yake huko Lagos wiki jana.

    Shirika la kupambana na unyanyasaji wa dawa za kulevya katika taarifa lilisema uvamizi huo ulifuata "intelijensia" ya kuaminika kwamba malkia huyo wa zamani wa urembo alihusika katika dawa haramu.

    "Zilizopatikana kutoka nyumbani kwake wakati wa msako ulioshuhudiwa na maafisa wanaohusika na masuala ya mali ni pamoja na gramu 606 za Canadian Loud, aina ya bangi, mizani ya kielektroniki, idadi kubwa ya plastiki zinazopakiwa dawa," taarifa hiyo iliongeza.

    Mshukiwa huyo alikuwa Miss Commonwealth Nigeria Culture 2015/2016 na mwanzilishi wa Queen Christmas Foundation.

    Bado hajatoa maoni yake kuhusu tuhuma hiyo.

    Mshukiwa mwingine, ambaye alikuwa akirejea kutoka Brazil wiki jana, pia alikamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Murtala Muhammed kwa kumeza vidonge 60 vya kokeini, shirika hilo lilisema.

    Pia unaweza kusoma:

  18. Kucheza ala ya muziki ni kuzuri kwa afya ya ubongo nyakati za uzeeni - utafiti

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Kucheza ala ya muziki au kuimba kunaweza kusaidia ubongo kuwa na afya katika uzee, watafiti wa Uingereza wanapendekeza.

    Kufanya mazoezi na kuimba muziki kunaweza kusaidia kudumisha kumbukumbu nzuri na uwezo wa kutatua kazi ngumu, utafiti wao unasema.

    Katika ripoti yao, iliyochapishwa katika Jarida la Kimataifa la Geriatric Psychiatry, wanasema muziki unapaswa kuzingatiwa kama sehemu ya mtindo wa maisha kudumisha ubongo.

    Zaidi ya watu 1,100 wenye umri wa zaidi ya miaka 40, wakiwa na wastani wa umri wa miaka 68, walichunguzwa.

    Wanasayansi katika Chuo Kikuu cha Exeter waliona data ya utendaji wa ubongo wao kama sehemu ya utafiti mpana ambao umekuwa ukigundua jinsi akili inavyozeeka, na kwa nini watu hupata matatizo ya akili.

    Waliangalia athari za kucheza ala, kuimba, kusoma na kusikiliza muziki, na uwezo wa muziki.

    Watafiti walilinganisha data ya utambuzi ya wale walio katika utafiti ambao walijihusisha na muziki kwa namna fulani katika maisha yao, na wale ambao hawakuwahi.

    Matokeo yao yalionyesha kuwa watu waliocheza ala za muziki walinufaika zaidi, ambayo inaweza kuwa kwa sababu ya "mahitaji mengi ya utambuzi" ya shughuli hiyo.

    Kusikiliza tu muziki hakukusaidia afya ya utambuzi.

    Faida inayoonekana kwa kuimba inaweza kuwa kiasi fulani kwa sababu ya vipengele vya kijamii vinavyojulikana vya kuwa katika kwaya au kikundi, watafiti wanasema.

    "Kwa sababu tuna vipimo nyeti vya ubongo kwa ajili ya utafiti huu, tunaweza kuangalia vipengele vya mtu binafsi vya kazi ya ubongo, kama vile kumbukumbu ya muda mfupi, kumbukumbu ya muda mrefu, na kutatua matatizo na jinsi muziki unavyoweza kuathiri," lead. mwandishi Prof Anne Corbett aliambia BBC.

    "Hakika hii inathibitisha na kusisitiza kwa kiwango kikubwa zaidi kile tunachojua tayari kuhusu faida za muziki.

    "Hasa, kucheza ala kuna athari kubwa sana, na watu wanaoendelea kucheza hadi uzeeni walipata faida ya ziada," alisema.

  19. DR Congo yatinga robo fainali kwa kuibandua Misri kupitia mikwaju ya penalty

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Kipa Lionel Mpasiwa wa DR Congo alifunga penalti ya 18 katika awamu ya kusisimua ya matuta ya penalti huku Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ikitoa mshtuko wa hivi punde katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2023 kwa kuwatoa mabingwa mara saba Misri na kutinga robo fainali kufuatia sare ya 1-1 baada ya muda wa ziada.

    Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ilisonga mbele kwa mara ya kwanza kwenye fainali hizo wakati Meschack Elia alipounganisha kwa kichwa krosi ya Yoane Wissa na kuiweka timu hiyo katika nafasi ya 67 duniani kwa matokeo ya hivi punde ya kushtukiza katika mchuano ambao umeshuhudiatimu zilizotajwakuwa dhaifu zikishindavigogo wa soka barani Afrika huko Ivory Coast.

    Uongozi wao ulidumu kwa dakika tisa kabla ya Mostafa Mohamed kufunga penalti katika kipindi cha mapumziko.

    Pia unaweza kusoma:

  20. Wanajeshi watatu wa Marekani wauawa katika shambulio la ndege zisizo na rubani Mashariki ya Kati

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Wanajeshi watatu wa Marekani wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa katika shambulio la ndege isiyo na rubani kwenye kituo cha Marekani karibu na mpaka wa Jordan na Syria.

    Rais wa Marekani Joe Biden alisema shambulio hilo lilitekelezwa na "makundi ya wapiganaji wenye itikadi kali wanaoungwa mkono na Iran". Aliongeza: "Tutajibu."

    Ni mara ya kwanza kwa shambulio kuua wanajeshi wa Marekani katika eneo hilo tangu shambulio la Hamas la tarehe 7 Oktoba dhidi ya Israel.

    Jordan inasema shambulio hilo lilifanyika Syria, sio ndani ya Jordan.

    Kumekuwa na mashambulizi mengine kwenye kambi za Marekani katika eneo hilo lakini hadi sasa hakuna majeraha walioripotiwa na jeshi la Marekani.

    Haijabainika ni nani aliyetekeleza shambulio hili la hivi punde.

    Rais Biden alisema Marekani "itawawajibisha wale wote wanaohusika kwa wakati na kwa njia tunayochagua".

    Pia unaweza kusoma: